Waziri wa zamani, Khamis Kagasheki: Kauli ya Dk. Bashiru ningeitoa mimi nisingebaki salama!

Daimler

JF-Expert Member
Sep 11, 2018
556
973
IMG_9043.JPG


Aliyewahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii na Mbunge wa Bukoba Mjini, Balozi Khamis Kagasheki, akiongea na Mwananchi juu ya ujumbe aliouandika kwenye Akaunti yake ya Twitter, amesema hawezi kuongeza neno juu ya ujumbe alioandika.

Katika Akaunti yake, ameandika kuwa: "Nimeyaelewa vizuri sana maelezo ya Dr. Bashiru kuhusu upigaji kura wa wananchi, uhalali wa Serikali, matamshi ya Viongozi nk. ..... Maneno yale ningeyasema mimi naamini baadhi ya wanachama wenzangu wasingeniacha salama."

IMG_9042.jpg


IMG_9040.JPG


Hapa Kagasheki atakuwa anamaanisha akina nani?
Je, hajaingilia tayari integrity ya Wana-CCM wenzake kuwa wanambagua kwa kuwa yeye ni Kagasheki?
Je, hiyo inamaanisha Kagasheki anataka Dk. Bashiru ajiuzulu?
 
Wenye CCM yao wanaitaka ikiwa salama, wavamizi wanapiga tu mradi liende...

Ukweli ni kwamba Kesho ya CCM ni ngumu saana, Polisi hawawezi kuwasaidia kila siku... Mbinu ikitumika Sana huchokwa na mbinu mbadala.

Kwa oppressed huibukaa..... through learning.....

Bado kitambo kidogo....
 
Mwacheni Katibu wa chama chetu pendwa, kaamua kutoa ya moyoni kwa malengo mazuri tu ya kuleta siasa za ushindani huru. Hizo ndo siasa safi zenye raha bana. Kushindana kwa hoja ni raha sana.

Mwacheni Dr afanye reformation, na msema kweli ni mpnz wa Mungu. Tunategemea kuona siasa safi za ushindani wa hoja kama mwanzo. Kweli siasa inafanyika na watu wanafurahia kupiga kura, na kuchagua viongozi wao. Kwa sasa hata mtu anaona hamna haja ya kupiga kura maana kiongozi atakayeshinda anafahamika.

Ila ndo hivyo sasa tunakipenda chama chetu hatuwezi kuondoka, tutabanana hapa hapa, na ushindi tutashangilia. CCM HOYEE!!!
 
Dr. Bashiru yupo sahihi kabisa. Lakini hii kauli yake ikitafsiriwa kwa mapana yake inamaanisha hata matokeo yanayoonyesha "voter turnout" ya asilimia 70 na zaidi yanayotolewa na tume ya uchaguzi ni MATOKEO YA KUPIKA.

Hii kauli naona inawaunguza hadi tume ya uchaguzi. Lazima nao wahojiwe watoe msimamo wao kama kweli turn-out ni chini ya asilimia 50 kama alivyosema Dr. Bashiru.

TUJENGE KIZAZI CHA KUHOJI
 
CCM ni chama Cha kidemokrasia ndio sababu Hata Katibu Mkuu anaweza kutoa maoni yake bila ya hofu

Ingekuwa ACT, CUF Au Chadema Katibu Mkuu akosoe chama hadharan angekuwa kishafukuzwa
Hahahhahahahaha mkuu nadhani unatania. Mi nadhani kagasheki anaongea wanachama halisi wa CCM na wazamiaji.

Kagasheki anamaanisha laiti mwanachama kindakindaki angelitamka hayo Moto wake sijui; labda kingefata barua ya onyo. Ila Sasa katamka mteuliwa
 
Back
Top Bottom