Waziri wa uchukuzi tafutia ufumbuzi tatizo la usafiri wa mabasi ya mwendokasi

lingamba lidodi

JF-Expert Member
Nov 15, 2018
964
1,137
Heri ya mwaka upya2019. Wakati inajengwa miundombinu ya mwendokasi,tulitegemea kuondokana na kero ya usafiri kwenye jiji la Dars s msaalam. Serikali ikazuwia daladala kupita na kufika baadhi ya maeneo.

Tofauti na tulivyotegemea,sasa hivi usafiri wa mwendokasi umekuwa kero mpaka wakazi wa Dar wamekumbuka daladala zao. Ili upande mwendokasi ni lazima ujitoe ufahamu,huko ndani watu wanajazana mithiri ya mihongo ikisafirishwa kutoa mkuranga.

Ni lazima uwe na nguvu za kupanda na kushuka. Kwa wale walioshauriwa na madaktari kufanya mazoezi kwa ajili ya kuondoa mafuta mwilini,mwendokasi inawafaa sana,maana siyo kutoa jasho tu bali kumwagika jasho.

Ni vizuri serikali kupitia wizara yenye dhamana iangalie jinsi ya kuufanya usafiri huu kuwa wa kisasa zaidi na matumizi yake yawe bora yenye heshima na staha kwa mtanzania. Usafiri hata wa Nguruwe una nafuu!

ONGEZENI BASI WATU WAKAE LEVEL SEAT, KAMA PESA HAZIPO RUHUSUNI DALADALA KWENYE NJIA MLIZOZUWIA.

Lakini kwa hali ya sasa usafiri wa mwendo kazi unamzalilisha mtanzania. Nawasilisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa mawazo yangu nafikiri madereva wengi wa mwendokasi wametoka kwenye kuendesha daladala wengi wao wanasahau kama wako kwa ajili ya kutoa huduma kwa wakazi wa Dar na viunga vyake utakuta gari inapita kituo basi liko tupu na kituoni wamejaa abiria kibao sasa unajiuliza huko anakokwenda anakimbilia nini?.kuanzia saa 3 mwisho wa vituo kama ferry na kimara utakuta mabasi wameyapaki madereva wanapiga story wakati kituoni abiria wamejaa wanaudhi sana hawa jamaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ili kupunguza matatizo ya UDART mambo mawili ni short run yafanyike:

1. Iruhusiwe kampuni nyingine moja au mbili kutumia miundombinu ya UDART ku-operate services na ishindane na UDART
2. Daladala za kawaida ziruhusiwe ku- operate in parallel na mabasi yanayotumia miundo mbinu ya mwendo kasi
 
Waziri ana muda huo.. inavyo onekana wameshwa wekwa kwapani na Simon group.

Haiezekani malalamiko yote haya hadi leo wasiwe wamepata operator mpya na kubadili mfumo wa ukusanyaji na ulipaji operator

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Heri ya mwaka upya2019. Wakati inajengwa miundombinu ya mwendo kasi,tulitegemea kuondokana na kero ya usafiri kwenye jiji la Dars s msaalam. Serikali ikazuwia daladala kupita na kufika baadhi ya maeneo. Tofauti na tulivyotegemea,sasa hivi usafiri wa mwendo kazi umekuwa kero mpaka wakazi wa Dar wamekumbuka daladala zao. Ili upande mwendokasi ni lazima ujitoe ufahamu,huko ndani watu wanajazana mithiri ya mihongo ikisafirishwa kutoa mkuranga. Ni lazima uwe na nguvu za kupanda na kushuka. Kwa wale walioshauriwa na madaktari kufanya mazoezi kwa ajili ya kuondoa mafuta mwilini,mwendokasi inawafaa sana,maana siyo kutoa jasho tu bali kumwagika jasho. Ni vizuri serikali kupitia wizara yenye dhamana iangalie jinsi ya kuufanya usafiri huu kuwa wa kisasa zaidi na matumizi yake yawe bora yenye heshima na staha kwa mtanzania. Usafiri hata wa Nguruwe una nafuu! ONGEZENI BASI WATU WAKAE LEVEL SEAT, KAMA PESA HAZIPO RUHUSUNI DALADALA KWENYE NJIA MLIZOZUWIA.. Lakini kwa hali ya sasa usafiri wa mwendo kazi unamzalilisha mtanzania. Nawasilisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hawa mawaziri wanajua mambo ya kujenga tu miundo mbinu ,hawana hata chembe ya upeo wa uchukuzi yaani vyombo vya usafirishaji.Mwendo kasi ni majibu ya upeo wao.Its a failed state on that matter.
 
Mwendokasi tuu hizi za ardhini zinawashinda za hapo angani sijui ni miujiza gani haswa watu wanategemea aisee!!
 
Ili kupunguza matatizo ya UDART mambo mawili ni short run yafanyike:

1. Iruhusiwe kampuni nyingine moja au mbili kutumia miundombinu ya UDART ku-operate services na ishindane na UDART
2. Daladala za kawaida ziruhusiwe ku- operate in parallel na mabasi yanayotumia miundo mbinu ya mwendo kasi


Mkuu, miundombinu ni mali ya DART siyo UDART
 
Back
Top Bottom