Nathubutu kusema waziri wa chakula na ushirika kalala usingizi wa namna gani baada ya wananchi wake wnapouziwa mbolea za kupandia zinazosadikika ni fake, mfano dap iko ya aina mbili yaani primium mifuko yake ni ya buluu na kwa ndani ni nyeusi bei yake ni 67000 kwa mfuko na nyingine iko chapa meli kwa ndani ni nyeupe na bei yake ni 70000, tatizo langu ni kwamba nchi moja kuwa na mbolea zenye bei tofauti, je hapa kuna ubora wa mbolea hizi? Ningependa serkali itoe ufafanuzi kuokoa asilimia 80 ya watanzania wanaotegemea kilimo ili wasije wakaingia mkenge.