Waziri wa Afya, naomba utueleze ukweli kuhusu mlipuko wa Virusi vya Corona Tanzania

DOMBWELA

JF-Expert Member
Jan 18, 2014
757
842
Mhe Ummy Mwalimu naomba utueleze ukweli kuhusu hali halisi na huu ugonjwa wa corona hapa Tanzania ili tujihami kuliko kuficha ficha, ijapokuwa kila jambo lina athari zake!

Kama mtu wa kawaida sana nikiunganisha ninayoyaona na kuyasikia katika mazingira yangu naona tisho ni kubwa la ugonjwa huu katika nchi yetu, nitoe mfano kidogo;-

1. Wenzetu tunaoishi nao wanaotoka huko ugonjwa huu ulikoanzia asilimia kubwa yao ninaokutana nao naona wamevaa vile vya kuzuia pua na mdomo, hii kweli linaniongezea hofu kubwa sana ya uwezekano mkubwa wa ugonjwa huu kuwepo au kuingia dakika yoyote!

2. Tukio nililolisikia hapo daraja jipya la salenda kambi namba 2 ya upande wa ostabey juu mchina aliyekuwa akishukiwa na Corona katika kambi hiyo, ijapokuwa mlijitahidi kufanya kilichofanyika na kuwa ilivyosasa!.

Hayo machache na mengine ninayo yaona na kuyasikia yananiongezea hofu kubwa juu ya hili jinamizi la Corona!

Najua athari za kusema waziwazi juu ya uwepo wa corona ndani ya nchi, lakini kuongeza elimu au uelewa kwa wananchi na kuwapa updates zote juu ya jinamizi hili ni muhimu sana kuliko kukaa kimya bila kuujulisha na kuutahadharisha umma!

Kwa uchumi wetu, elimu yetu, teknolojia yetu, n.k, tukiingiliwa tutaweza? Bado naona kinga ni bora kuliko tiba, maana naona na kusikia jinsi nchi kubwa zinavyohangaika na hili jinamizi la Corona.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Alishazungumza ,we are safe.
Japokuwa uache kuzulula mda huu na kusalimia watu ovyo kwa kuwashika watu mikono..
 
Na hili la daladala kujaza hadi watu wanakosa sehemu ya kuweka mguu sijui trafiki wanafanya kazi gani, mbona Nairobi wanatekeleza utaratibu wa level seat toka kitambo sana. Katika mazingira ya mlipuko wa corona na namna daladala zinavyojaza utafikiri fuso limebeba matenga ya nyanya tutegemee tu miujiza...
 
Msijali waziri wetu wa afya hatoi viza za magonjwa ya maambukizi hovyo hovyo.
 
Kiafrika ukipewa taarifa juu ya dhahma fulani hasa hasa ugonjwa ujue tayari anaishi ndani mwetu. Ila nikutoe tu hofu ya kwamba katika kitu ambacho mzungu kakibugi kwetu sisi ni hii kitu. Katuweza kwenye Ukimwi, Kansa, Sukari.
 
Huku kwetu Kwamtogole tumeambiwa ukiona dalili usitoke kwenda hospitali, Piga simu useme ulipo, kuna watu maalum watakufuata kukupeleka eneo maalumu kwa uchunguzi na tiba.
 
Wabongo bhana.
Laiti mngekuwa mnapata access na mambo ya Usalama na Taifa lenu nadhani.
Mngeshangazwa mnoo..

Kuna kikosi kazi cha kuondoa hujuma na miripuko dizain na zaidi ya mambo mnayoyasikia.

Kama tulifanikiwa kupunguza na kuondoa tension ya Ebola sembuse hii kimafua?!

Japo Moja Ya Nchi za Africa zilizo target Tanzania yupo mwezi wa 3
Mkivuka salama basi tegemeeni kuisikia Nchi za pembeni

Virus vya Corona rasmi vitaingia Africa Kati na Mwishon mwa mwezi huu na Mwanzoni mwa mwezi wa 4
Tahadhari imeshatolewa kuwa kila mkoa utenge eneo maalum la wagonjwa wa corona...
Kwa tangazo hilo tambua tayari mkorona keshatia timu nchini

Jr
Tunasubiri kwanza watu wafe kwa makumi ndio tutatangaza uwepo wake, mkuu kama unajua kuunga dot ile taarifa ya jana ya kutenga sehemu za kuwaweka suspect kwa kila mkoa ni alert tosha kua jinamizi lishatia timu ila tunaandaliwa kisaikolojia kwanza ili kupunguza panic.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna nchi fulani ya Afrika mashariki ikitokea wamegundua uwepo wa gonjwa la Corona hiyo nchi itaficha wala haitatangaza!
 
Back
Top Bottom