Mimi siamini kama hao wabunge wa EAC wanaenda huko Bungeni hawajui kitu gani wanachoenda kuongea na kama ni kweli basi kuna mamtaizo makubwa nchi hii siyo tu kujua sera gani za nchi za kuzitetea katika hilo bunge.
Hakika hata mimi nashindwa kuamini hili jambo. Yaani watu waliochaguliwa na wabunge wenzao wanasema kwenye kadamnasi kuwa kila mbunge anajiongelea kivyake vyake kwenye mambo yanayohusu taifa? Kama ni kweli, it is a big shame. Hivi litakuwa ni kosa la nani. He! Kama hakuna msimamo wa pamoja katika kujibu hoja tutegemee nini jamani Watz? Hii ni hatari kwa mustakabali wa nchi. Je, alaumiwe nani?