NALIA NGWENA
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 10,206
- 12,723
Mh waziri (Ndubalo) huu siyo muda wa kutishia mashabiki wa Simba na Yanga Sc katika utani wao wa Jadi ulioota mizizi kwa miaka 80+ mpaka kwani utaonekena Kama Unawapangia namna ya kuishi.
NALIA NGWENA niliposikia kauli yako nilipatwa na ukakasi mpaka nikajiuliza kuwa Mh waziri amekosa Cha maana katika ukuaji wa mpira wetu huu?! Mpaka anaanza kuingilia Kati ushabiki wa Simba sc na Yanga Sc?!
Katika ligi yetu hii Kuna wachezaji wazuri wengi mno ambao mataifa Yao hayawatambui (hayawaiti katika kikosi Cha taifa) wachezaji kutoka Kongo, wachezaji kutoka Ivory coast tunawachezaji kutoka mataifa mbali mbali ambao hata ukipiga hesabu katika kikosi Chao Cha taifa ni ngumu kuitwa.
Kwa nini waziri Ndubalo usichangamke kuokoteza wachezaji wazuri (wenye TALANTA) na unafanya mpango wapate uraia watusaidie AFCON 2027?
Kama alipewa Kibu denisi Kuna wachezaji wazuri Kama Max Nzengeli n.k Hawa ukiwapa uraia hawatokuangusha katika kulipambania taifa letu maan nchi Kama ya Kongo Ina wachezaji wengi sana kuitwa Katika kikosi ni ndoto.
Ushauri wangu kwa Waziri wa michezo : Mashabiki wa Simba sc na Yanga Sc ni watani wa Jadi kuwapangia wafanye nini katika utani wao ni kuwaingilia uhuru wa furaha Yao unapaswa kufanya Jambo litakalo acha legacy katika uongozi wako lakini siyo kuingilia uhuru wa mashabiki wa kariakoo.
NALIA NGWENA niliposikia kauli yako nilipatwa na ukakasi mpaka nikajiuliza kuwa Mh waziri amekosa Cha maana katika ukuaji wa mpira wetu huu?! Mpaka anaanza kuingilia Kati ushabiki wa Simba sc na Yanga Sc?!
Katika ligi yetu hii Kuna wachezaji wazuri wengi mno ambao mataifa Yao hayawatambui (hayawaiti katika kikosi Cha taifa) wachezaji kutoka Kongo, wachezaji kutoka Ivory coast tunawachezaji kutoka mataifa mbali mbali ambao hata ukipiga hesabu katika kikosi Chao Cha taifa ni ngumu kuitwa.
Kwa nini waziri Ndubalo usichangamke kuokoteza wachezaji wazuri (wenye TALANTA) na unafanya mpango wapate uraia watusaidie AFCON 2027?
Kama alipewa Kibu denisi Kuna wachezaji wazuri Kama Max Nzengeli n.k Hawa ukiwapa uraia hawatokuangusha katika kulipambania taifa letu maan nchi Kama ya Kongo Ina wachezaji wengi sana kuitwa Katika kikosi ni ndoto.
Ushauri wangu kwa Waziri wa michezo : Mashabiki wa Simba sc na Yanga Sc ni watani wa Jadi kuwapangia wafanye nini katika utani wao ni kuwaingilia uhuru wa furaha Yao unapaswa kufanya Jambo litakalo acha legacy katika uongozi wako lakini siyo kuingilia uhuru wa mashabiki wa kariakoo.