Waziri Ndalichako avisotesha vyuo vikuu

Waziri Ndalichako avisotesha vyuo vikuu

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,252
Reaction score
16,171
Asilimia 90% ya uendeshaji wa vyuo vikuu nchini unategemea ada za mwanafunzi. Asilimia 98 ya wanafunzi wa walioko vyuo vikuu nchini wanategemea mikopo kutoka board ya mikopo lakini mpaka sasa Board ya mikopo haijatoa ada hizo za wanafunzi kwa vyuo tangu November vyuo vilipofunguliwa kwa kisingizio cha kutafuta wafanyakazi na wanafunzi hewa.

Hali hii imesabababisha vyuo vinavyotengemea ada hizo kuzorota katika kutoa mafunzo.

Mishahara ya wakufunzi na huduma muhimu kwa wanafunzi vinashindikana kutolewa kutokana na vyuo kushindwa kujiendesha.

Kijana wangu amezuiwa kufanya mitihani kama mkakati wa vyuo hivyo kusaka hela za kuendeshea chuo kutoka kwa wazazi wao.

Jamani Ndali utatufanya tukuchukie wewe na wenzio kwa kadhia hii. Wakati unaendelea kuwatafuta wahalifu ukumbuke na wale wena nao huwa wana haki zao.

Do not strengthen the weakest by weakening the strongest.
 
Kweli watanzania mlizoea bure ndio maana elimu inakuwa chini kazi yenu kupinga kila jambo jema. Ila ujinga linashabikiwa na kila MTU mwisho tunapata wasomi vilaza
 
Nachelea kuiunga serikali mkono kwa hili la kuwanyima mkopo wanafunzi ambao tayari walikuwa wanahudumiwa na board.

Kama kulikuwa na tatizo la wizi ni bora wakashughulika nao lakini watoto wapewe mikopo yao.

Najua wengi mateso wanayoyapata wanachuo pale wanapozuiliwa fedha za kujikimu na hasa watoto wa kike.

Hebu huyo waziri aache unazi wake wa ualimu awe mama kwanza kisha aukumbuke kuwa aliwahi kuwa msichana.
 
Wanatoa boam kwa wanafunzi ili wasigome lakini inaacha kuwalipia ada ambayo ndo msingi wa vyuo kumudu kutoa huduma kwa wanafunzi. Hii sio sawa nadhani
 
Asilimia 90% ya uendeshaji wa vyuo vikuu nchini unategemea ada za mwanafunzi. Asilimia 98 ya wanafunzi wa walioko vyuo vikuu nchini wanategemea mikopo kutoka board ya mikopo lakini mpaka sasa Board ya mikopo haijatoa ada hizo za wanafunzi kwa vyuo tangu November vyuo vilipofunguliwa kwa kisingizio cha kutafuta wafanyakazi na wanafunzi hewa.

Hali hii imesabababisha vyuo vinavyotengemea ada hizo kuzorota katika kutoa mafunzo.

Mishahara ya wakufunzi na huduma muhimu kwa wanafunzi vinashindikana kutolewa kutokana na vyuo kushindwa kujiendesha.

Kijana wangu amezuiwa kufanya mitihani kama mkakati wa vyuo hivyo kusaka hela za kuendeshea chuo kutoka kwa wazazi wao.

Jamani Ndali utatufanya tukuchukie wewe na wenzio kwa kadhia hii. Wakati unaendelea kuwatafuta wahalifu ukumbuke na wale wena nao huwa wana haki zao.

Do not strengthen the weakest by weakening the strongest.
Alipe ada mbona huko private mnakopeleka kuanzia chekechea mnalipa hela nyingi tu.
 
Nachelea kuiunga serikali mkono kwa hili la kuwanyima mkopo wanafunzi ambao tayari walikuwa wanahudumiwa na board.

Kama kulikuwa na tatizo la wizi ni bora wakashughulika nao lakini watoto wapewe mikopo yao.

Najua wengi mateso wanayoyapata wanachuo pale wanapozuiliwa fedha za kujikimu na hasa watoto wa kike.

Hebu huyo waziri aache unazi wake wa ualimu awe mama kwanza kisha aukumbuke kuwa aliwahi kuwa msichana.
selekali yako haina uwezo wa ku handle mambo mengi kwa wakati mmoja!
 
ni afadhali tuwe na vyuo vichache lakini vinatoa wahitimu bora na siyo kua na utitiri wa vyuo lakini product yake ni zero
Vyuo vya umma sawa na shule za umma kitaaluma, sijui hivyo vyuo vichache unavyotaka vibaki ambavyo havitategemea ada za wanafunzi vitakuwa ni vipi?
 
Vyuo vya umma sawa na shule za umma kitaaluma, sijui hivyo vyuo vichache unavyotaka vibaki ambavyo havitategemea ada za wanafunzi vitakuwa ni vipi?
kuna vitu viwili quantity and quality katika elimu tunahitaji quality awamu iliyopita iliweka mkazo kwenye quantity matokeo yake ndio wanafunzi vilaza
 
Luna vitu viwili quantity and quality katoka elimu tunahitaji quality awamu iliyopita iliweka mkazo kwenye quantity matokeo yakr ndio wanafunzi ******
Kila kitu kinawezekana kama huo utawekwa kuwa huo ndio muelekeo wa taifa katika elimu badala ya kuwa muelekeo wa mtu fulani au waziri fulani kwenye awamu fulani ya chama tawala fulani. Taifa litayumba kama litatawaliwa kutokana na muono wa mtu mmoja ambaye tuna uhakisha kuwa hatabakia hapo alipo milele. Kila jambo zuri kwa taifa lazima liwe sustainable, na namna ya kuwa sustainable ni lazima lishirikishe wadau watakaoathiriwa na utekelezwaji wa jambo hilo. Vinginevyo taifa lita oscillate na ku spin badala ya ku-move forward. Kuna maana gani ya kupoteza nguvu nyingi kujenga nyumba imara na ya gharama kandoni mwa barabara ambayo una uhakika kuwa itabomolewa na mpimaji wa mpya wa maeneo ya barabara?. Mfumo wa GPA na Division ni mfano hai wa hili, waliobadilisha Division kwenda GPA ni watanzania wapo na wanaweza kurejea tena madarakani muda wowote na kuuponda tena mfumo huu wa kindalichako (Division) na kurejesha mfumo wa GPA au mwingine ule kama atakavyoona inamfaa yeye.
 
Asilimia 98 ya wanafunzi wanategemea mkopo""""" hapo umedanganya sana labda asilimia 48
 
Kwa wadogo zangu mliomaliza kidato cha sita na wa kidato cha nne mnaohitaji info kuhusu vyuo vya china(kozi,ada na admission process) kwa mwaka 2016 ninaweza kuwasaidia na i can help with admission process too.tuwasiliane kupitia +8613065131363 whatsapp only.na kwa wale form 6 science waliokosa sifa za kujiunga shahada foundation courses zipo za mwaka 1.KWA WANAFUNZI WANOJILIPIA WENYEWE TU.Karibuni huduma inatolewa bure
 
kitaa hawalijui hilo ndomana bado wanaichekea serikali yetu mbovu
ila tunaojua na tunaokuja huko chuo siku chache zijazo tunawasiwasi mkubwa
TUNAVUMILIA KUZALIWA TANZANIA
wasomi tupo tite kuliko hata asiyedeal na kusoma
now swala la elim limekua chungu mpaka mwenye one form 4 hataki kwenda five..... watu wanaona bora employment kuliko kusoma coz elim now imekua michosho na wajuaji wamekua wengi
Im done
 
kitaa hawalijui hilo ndomana bado wanaichekea serikali yetu mbovu
ila tunaojua na tunaokuja huko chuo siku chache zijazo tunawasiwasi mkubwa
TUNAVUMILIA KUZALIWA TANZANIA
wasomi tupo tite kuliko hata asiyedeal na kusoma
now swala la elim limekua chungu mpaka mwenye one form 4 hataki kwenda five..... watu wanaona bora employment kuliko kusoma coz elim now imekua michosho na wajuaji wamekua wengi
Im done
mm mwenyew najutia apa bora ningeachana na elim tangu la saba.
Ningejiemploy tu kulko sasa iv ninavyoisoma namba.
 
Back
Top Bottom