Waziri Muhongo Mfukoni Mwa Lowassa

Upuuzi mtupu. Kichwa cha habari na habari yenyewe haviendani. Lowasa kuwa na nyaraka za wizara kunaashiria vipi waziri kuwa mfukoni mwa Lowasa. Watanzania tuna matatizo makubwa sana, tunashindwa hata kutoa habari kwa namna inavyotakiwa.

Lowasa ni mbunge lakini pia ni mwenyekeiti wa kamati ya bunge ya mambo ya nchi za nje, kuwa na nyaraka za wizara mbalimbali siyo tatizo na wala siyo jambo la ajabu.

Mimi nimewahi kuwa na mkataba wa uchimbaji wa madini ya dhahabu kati ya serikali na kampuni, niliupata kwa kupitia mwekezaji mwenyewe. Je, kwa fikra zako ina maana waziri au kampuni ipo mfukoni mwangu?

Moderator ondoa hii thread, hakuna cha maana.

Siasa za nchi hii hazinogi bila kutajwa kwa jina la lowassa!
 
Lowassa yupo ndani ya damu za watanzania,maafisa wa serikali na hata wengi wa mawaziri wanaripoti kwake

Hayupo kwenye damu ya watanzania wala nini,ni trckstar tu ambaye anatumia vilivyo nguvu ya ukwasi alionao kupata anachotaka,that's influence of affluence.Chezea mkwanja wewe.
 

Mkuu Tunguli umeuona waraka mzito hivyo lazima aidha utakuwa mtu wa Lowasa ama uko wizarani na ni mwandamizi!
 
Last edited by a moderator:
Wananchi wenye kutaka maendeleo wanatamani na kutegemea EL awe rais, lkn wenye nia zao binafsi hawapendi kbs EL awe rais

Ila uzuri wapenda maendeleo ni wengi na wabinafsi ni wachache.

S6 ni mnafiki lkn kuna mambo ya msingi anaongeaga wakati mwingine moja ni lile CDM kuna Dr. slaa tu, lkn mie niongeze naona wameongezeka yupo Lissu,mnyika na lema. Sasa hawa hawajatosha kutuongoza ngoja waongezeke kwanza walio na mtizamu chanya CDM ndio 2020 tutawafikiria kuwa wanaweza kutuletea maendeleo."ngoja wakue-refer JKN"

Kuwapa 2015 bado wamezungukwa na njaa nyingi tutaangamiza taifa letu-Am sorry to say this lkn ndio ukweli
 
Lowasa anakazi kubwa sana. Ningemshauri afunge ndoa na wafuatao ili kushinda. Mwankyembe, mwandosya, sitta, magufuli na zitto kabwe.
 
Ujinga mtupu, nilipoona kichwa cha habari nilidhani Muhongo kajisalimisha kwa lowasa, kumbe wanaiba nyaraka? Kitu ambacho ni kawaida kabisa serikalini.

Angalau, hadi dakika hii hajawekewa price tag na Lowasa. Ningeshangaa
 
Ujinga mtupu, nilipoona kichwa cha habari nilidhani Muhongo kajisalimisha kwa lowasa, kumbe wanaiba nyaraka? Kitu ambacho ni kawaida kabisa serikalini.

Angalau, hadi dakika hii hajawekewa price tag na Lowasa. Ningeshangaa


wamesema Lowassa ndio anaamua mradi upi upite upi usipite
 
Swali la kwanza, Muhongo kaji-submit kwa Lowasa? Au Lowasa anatumia njia za kuhonga ili kufanikisha malengo yake(crime syndicate)?

Kama mradi anaoamua Lowasaa unapita kwa kutumia njia za kihalifu na si kwa kumnunua Muhongo, hiyo ni ishu nyingine.

Na ni mradi upi aliokataza au kupitisha Lowasa? Lowasa ni tabula rasa kwenye masuala ya mafuta na gesi, period.

wamesema Lowassa ndio anaamua mradi upi upite upi usipite
 
Hamkumbuki Sophia Simba aliwahi kusema kuwa hakuna mwanaume wa shoka hapa Tanzania kama Lowasa? Haishangazi hata wanaume wenzake kawaweka mfukoni kwake !
 
muulize mkuu Ben Saanane analo jibu sahihi
 
Last edited by a moderator:
Hamkumbuki Sophia Simba aliwahi kusema kuwa hakuna mwanaume wa shoka hapa Tanzania kama Lowasa? Haishangazi hata wanaume wenzake kawaweka mfukoni kwake !

Hata kumuongelea mtu ni hoja..itakua kuongea kashfa??nayo ni hoja tu.

Kwa kukusaidia jiulize kwanini wanaume unaowasema wanamuunga mkono ndio utapata jibu-na usikimbilie hela kama akili yako wangapi wanahela kama bakheresa wkenye issue zake na nimrodi mkono lkn mbona hawaungwii mkono.

Wanaume wanawaza maendeleo zaidi na sio umbea au makosa kila mtu anayo-EL anaweza shughulikia maendeleo

Wanawake wanaangalia maendeleo ya wanaume nakushangiria wao zaidi wanawaza watakacho kipata kwa muda ule ule-hivyo muda ukifika EL ataongea na wanawake muda ukifikaa wakati huo watakua wanataka nini

Jiulize upokundi gani kati ya hayo mawili hapo juu
 

Kama wenye dhamana hawawezi kutimiza wajibu wao basi waache wenye uwezo wazifanye kazi hizo; bottom line is lazima maisha yaendelee na nchi isonge mbele; serikali ya dhaifu kazi yake ni kusononeka; kulalamika na kulialia kila uchao!! kama imekubali kuwa remote controlled; wacha isaidiwe; hatima ya taifa itajulikana huko tuendako; we shall cross the bridge when we get there, not before.
 

Wee mwanamke una laana. Umemaliza chuo kikuu bado hujui kutofautisha kati ya R na L! Kuna vitu vingine mtu unaweza kukosea lakini sio jina la Mrema ambalo hata mtoto wa darasa la kwanza ataliandika kwa usahihi. Hii inaonyesha ulivyo mvivu na hutaki kujishughulisha! This is beyond believe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…