BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,020
Date::10/28/2008
Waziri Mkuu Pinda akerwa na watu wanaoikosoa serikali
Na Ally Sonda, Bomang'ombe
Mwananchi
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, ameonekana kukerwa na kelele zinazopigwa na baadhi ya wananchi kwamba utendaji kazi wa Serikali ya awamu ya nne, hauridhishi na kufafanua kuwa madai hayo, hayana msingi wowote kwa kuwa zinatolewa na watu wasiojua nchi ya Tanzania.
Pinda alitoa kauli hiyo mwishoni mwa ziara yake mkoani Kilimanjaro wakati akihutubia mkutano wa hadhara kwenye Kijiji cha Lemira baada ya kuzindua Sekondari ya Wananchi wa kata ya Lemira.
Pinda aliwataka Watanzania wafanye kazi za uzalishaji mali kwa bidii kwa kushirikiana na viongozi wa Serikali ili waweze kuboresha zaidi huduma za jamii badala ya kuendekeza kelele zinazotolewa na wababaishaji wachache.
"Wananchi acheni kusikiliza kejeli za baadhi ya watu wa mjini, unajua ukiwa mjini maelezo unayoyapata kuhusu hali ya nchi, yanaweza kukuogopesha, kumbe sivyo, serikali yenu inajitahidi kuwafikishia maendeleo makubwa huku vijijini,"alisema Pinda.
Pinda alichukua muda mwingi katika hotuba yake kumpongeza Mbunge wa Hai, Fuya Kimbita kwa jitihada nyingi anazofanya kusaidia kuboresha huduma za kijamii katika jimbo hilo.
"Ndugu zangu wananchi Mbunge wenu Fuya Kimbita alinisumbua sana tangu nikiwa Waziri wa Tamisemi, alitaka nije jimboni kumsaidia kuhimiza maendeleo yenu, sasa Mungu amejalia nimekuja nikiwa Waziri Mkuu, nitamsaidia sana kuwaleteeni maendeleo,"alisema Pinda.
Waziri Mkuu aliwaomba wananchi wampe ushirikiano mbunge huyo kwa kumuelekeza badala ya kumteta ili aweze kutekeleza ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2005 kwenye jimbo lake.
Waziri Mkuu Pinda akerwa na watu wanaoikosoa serikali
Na Ally Sonda, Bomang'ombe
Mwananchi
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, ameonekana kukerwa na kelele zinazopigwa na baadhi ya wananchi kwamba utendaji kazi wa Serikali ya awamu ya nne, hauridhishi na kufafanua kuwa madai hayo, hayana msingi wowote kwa kuwa zinatolewa na watu wasiojua nchi ya Tanzania.
Pinda alitoa kauli hiyo mwishoni mwa ziara yake mkoani Kilimanjaro wakati akihutubia mkutano wa hadhara kwenye Kijiji cha Lemira baada ya kuzindua Sekondari ya Wananchi wa kata ya Lemira.
Pinda aliwataka Watanzania wafanye kazi za uzalishaji mali kwa bidii kwa kushirikiana na viongozi wa Serikali ili waweze kuboresha zaidi huduma za jamii badala ya kuendekeza kelele zinazotolewa na wababaishaji wachache.
"Wananchi acheni kusikiliza kejeli za baadhi ya watu wa mjini, unajua ukiwa mjini maelezo unayoyapata kuhusu hali ya nchi, yanaweza kukuogopesha, kumbe sivyo, serikali yenu inajitahidi kuwafikishia maendeleo makubwa huku vijijini,"alisema Pinda.
Pinda alichukua muda mwingi katika hotuba yake kumpongeza Mbunge wa Hai, Fuya Kimbita kwa jitihada nyingi anazofanya kusaidia kuboresha huduma za kijamii katika jimbo hilo.
"Ndugu zangu wananchi Mbunge wenu Fuya Kimbita alinisumbua sana tangu nikiwa Waziri wa Tamisemi, alitaka nije jimboni kumsaidia kuhimiza maendeleo yenu, sasa Mungu amejalia nimekuja nikiwa Waziri Mkuu, nitamsaidia sana kuwaleteeni maendeleo,"alisema Pinda.
Waziri Mkuu aliwaomba wananchi wampe ushirikiano mbunge huyo kwa kumuelekeza badala ya kumteta ili aweze kutekeleza ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2005 kwenye jimbo lake.