Waziri Mkuu: Migogoro ya Ardhi kati ya Maeneo ya Hifadhi na Vijiji 920 yatatuliwa.

pefhana

Senior Member
Mar 26, 2017
158
105
Mh. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo hii ametoa taarifa ya kikao cha Baraza la Mawaziri kilichokaa mapema leo kupokea na kujadili ripoti ya Kamati ya Mawaziri wanane iliyoundwa kubaini idadi ya vijiji vyenye migogoro ya Ardhi na maeneo mbalimbali ya Hifadhi. Katika taarifa ya awali kabla ya kamati hiyo kuundwa ilisemekana kuna vijiji 366 ambavyo viliingia au vinafanya shughuli zao za kilimo, ufugaji na uvuvi katika maeneo hayo. Lakini taarifa ya kamati inaonesha jumla ya vijiji 975 ndivyo vimebainika kuwa katika migogoro hiyo

Taarifa ya Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichoendeshwa na Mhe. Rais kimeamua kuwa pasiwepo hata kijiji kimoja kitakachohamishwa kutoka katika maeneo hayo na kwamba kwa baadhi ya Hifadhi maeneo yanayokaliwa na vijiji viachiwe vijiji na kwamba serikali itaweka mipaka mipya bila kuviumiza vijiji.

Kwa hatua ya kwanza maeneo ya jumla ya vijiji 920 yameidhinishwa na imeagizwa vijiji hivi vipatiwe hati za vijiji. Kwa vijiji 55 vilivyosalia, upembuzi na uainishaji wa mipaka unaendelea na taarifa ya awamu ya pili pamoja na majina ya vijiji itatolewa mara baada ya mchakato kukamilika mapema iwezekenavyo.

 
Nilimsikiliza waziri mkuu akiwa live chanel ten, ila kiukweli nimesoneneka sana kusikia hifadhi za taifa zikimegwa na nyingine zikifutwa....kwa kweli jambo hili limenifanya nisadiki kuwa uongozi wa awamu ya tano sio rafiki wa mazingira na uhifadhi wa vinavyopatikana ndani yake
 
Hatujafika hata watu milioni 100 ila tushaanza kumega hifadhi za misitu na wanyawapori na sijui tukapofika idadi hiyo na zaidi hali itakuaje
 
Hujui mateso wanayopata wakulima na wafugaji kuhusu Ardhi. Wakati tunapata Uhuru idadi ya watu ilikuwa milioni 9. Maeneo ya vijiji yalitosha sasa tupo milioni 50 unaweza ukaona mahitaji ya ardhi ni makubwa kiasi gani. Lakini kwa upande mwingine hizo zinazoitwa hifadhi ama wanyama wamepungua sana kwa uwindaji haramu, mabadiliko ya hali ya hewa na magonjwa au hayana wanyama kabisa. Baadhi ya maeneo huwezi kumuona hata sungura. Binafsi nampongeza Rais na Baraza lake kwa kuwapigania wanavijiji wanyonge wapate ardhi kwa ajili ya uzalishaji mali
Nilimsikiliza waziri mkuu akiwa live chanel ten, ila kiukweli nimesoneneka sana kusikia hifadhi za taifa zikimegwa na nyingine zikifutwa....kwa kweli jambo hili limenifanya nisadiki kuwa uongozi wa awamu ya tano sio rafiki wa mazingira na uhifadhi wa vinavyopatikana ndani yake
 
Nilimsikiliza waziri mkuu akiwa live chanel ten, ila kiukweli nimesoneneka sana kusikia hifadhi za taifa zikimegwa na nyingine zikifutwa....kwa kweli jambo hili limenifanya nisadiki kuwa uongozi wa awamu ya tano sio rafiki wa mazingira na uhifadhi wa vinavyopatikana ndani yake
[/QUOThivi watu mnataka mtendewe nini ndo mguswe na ku appreciate kilichofanyika hata kama hamlazimishwi kufanya hivyo???hivi unadhani ktk idadi ya vijiji 900+ kuna watu wangapi wangetesekaje iwapo vijiji hivyo vingefutwa????hao watu wewe ulikuwa na pakuwapeleka bila kuathiri mila,tamaduni na shughuli zao za kila siku????
 
Nilimsikiliza waziri mkuu akiwa live chanel ten, ila kiukweli nimesoneneka sana kusikia hifadhi za taifa zikimegwa na nyingine zikifutwa....kwa kweli jambo hili limenifanya nisadiki kuwa uongozi wa awamu ya tano sio rafiki wa mazingira na uhifadhi wa vinavyopatikana ndani yake
[/QUOThivi watu mnataka mtendewe nini ndo mguswe na ku appreciate kilichofanyika hata kama hamlazimishwi kufanya hivyo???hivi unadhani ktk idadi ya vijiji 900+ kuna watu wangapi wangetesekaje iwapo vijiji hivyo vingefutwa????hao watu wewe ulikuwa na pakuwapeleka bila kuathiri mila,tamaduni na shughuli zao za kila siku????
 
Hujui mateso wanayopata wakulima na wafugaji kuhusu Ardhi. Wakati tunapata Uhuru idadi ya watu ilikuwa milioni 9. Maeneo ya vijiji yalitosha sasa tupo milioni 50 unaweza ukaona mahitaji ya ardhi ni makubwa kiasi gani. Lakini kwa upande mwingine hizo zinazoitwa hifadhi ama wanyama wamepungua sana kwa uwindaji haramu, mabadiliko ya hali ya hewa na magonjwa au hayana wanyama kabisa. Baadhi ya maeneo huwezi kumuona hata sungura. Binafsi nampongeza Rais na Baraza lake kwa kuwapigania wanavijiji wanyonge wapate ardhi kwa ajili ya uzalishaji mali
Watanzania tuache kujidanganya kuwa miaka ya leo tumekuwa wengi sana hadi kufuta na kumega hifadhi za misitu na mapori ya akiba

Huko nyuma hakujawahi fanyika maamuzi ya ajabu kama haya - kufuta na kumega hifadhi nyingi kiasi hiki, zaidi walikua wakikazana kuhifadhi na kuongeza idadi ya hifadhi

Kama leo tuwengi je 2050 tutakapokuwa zaidi ya milioni 100 mtasemaje?
 
Nilimsikiliza waziri mkuu akiwa live chanel ten, ila kiukweli nimesoneneka sana kusikia hifadhi za taifa zikimegwa na nyingine zikifutwa....kwa kweli jambo hili limenifanya nisadiki kuwa uongozi wa awamu ya tano sio rafiki wa mazingira na uhifadhi wa vinavyopatikana ndani yake

Wanyama na Binadamu nani muhimu? Acha kuwa blind minded
 
Wanyama na Binadamu nani muhimu? Acha kuwa blind minded

Binadamu halinganishwi na chochote jomba....na still nakazia uongozi wa awamu ya tano umekurupuka kumega na kufuta hifadhi za misitu na mapori ya wanyama

Hivi nchi ikifikia watu zaidi ya milioni 100 kama Nigeria, Bangladesh, Egypt, Ethiopia, Ufilipino suluhisho litaendelea kuwa ni kumega na kufuta hifadhi?
 
Nilimsikiliza waziri mkuu akiwa live chanel ten, ila kiukweli nimesoneneka sana kusikia hifadhi za taifa zikimegwa na nyingine zikifutwa....kwa kweli jambo hili limenifanya nisadiki kuwa uongozi wa awamu ya tano sio rafiki wa mazingira na uhifadhi wa vinavyopatikana ndani yake
Hili jambo kumega maeneo ya wazi kuwa hifadhi ndo matokeo yake haya tunayaona leo wafugaji kutapatapa ..maswa gem ilikua eneo la wazi na lile la meatu enelo linamilikiwa na kampuni ya uwindishaji iitwayo MWIBA ilikua eneo la wazi, walioyafanya kuwa wa wazi walifaham baada ya mika ijayao mifigo na watu wataongezeka lakini bila kujali serikali za awamu hiyo zikabadili matumizi ndo yaha tunayoyana kuhamahama kwa wafuga.
Pia haya maeneo mapya kama yalikua maeneo ya wazi wakati ule na kuyabadili kuwa ya hifadhi na kisha sasa wameamua kuyarudisha sio ubaya kwa kuwa haya yalikuepo na yalibadilishwa kuwa hifadhi kwa faida ya wachache..
 
Hili jambo kumega maeneo ya wazi kuwa hifadhi ndo matokeo yake haya tunayaona leo wafugaji kutapatapa ..maswa gem ilikua eneo la wazi na lile la meatu enelo linamilikiwa na kampuni ya uwindishaji iitwayo MWIBA ilikua eneo la wazi, walioyafanya kuwa wa wazi walifaham baada ya mika ijayao mifigo na watu wataongezeka lakini bila kujali serikali za awamu hiyo zikabadili matumizi ndo yaha tunayoyana kuhamahama kwa wafuga.
Pia haya maeneo mapya kama yalikua maeneo ya wazi wakati ule na kuyabadili kuwa ya hifadhi na kisha sasa wameamua kuyarudisha sio ubaya kwa kuwa haya yalikuepo na yalibadilishwa kuwa hifadhi kwa faida ya wachache..

Wewe ndio umetoa point katika hitimisho lako
 
Hili swala naona halijawagusa jamij ya wamasai waishio ndani ya mamlaka ya hifadhi ya ngorongoro....natamani sana rais ajue kinachoendelea kule idadi ya wamasai waishio Kule asilimia 97% wanaishi katika umaskini uliokithiri na nafikiri ndio wamasai maskini kuliko wamasai wenzao Wa east Africa na tatizo ni kuishi ndan ya hifadhi bila kuruhusiwa kulima au kujenga!!! Hali n tete lakini nitaitafutia uzi wake soon
 
Walininyang'anya mashamba yangu TANAPA Nafurahi kusikia yamerudi Mungu mbariki RAIS wangu Magufuli
 
Back
Top Bottom