Fact-Check: Kauli ya Muenezi wa Matamko (Paul Makonda) Kuhusu Migogoro ya Ardhi

Abdul Nondo

JF-Expert Member
Oct 28, 2016
515
2,875
Fact-Check ,Fact-Check Kuhusu Migogoro Ardhi.

Kwenda kwa Muenezi wa Matamko Bwana Ndug.Paul Makonda.

Bwana Muenezi Mtoa Matamko umetoa tamko Kwaniaba ya chama kumpa Waziri Mkuu miezi 6 kushughulikia suala la migogoro ya ardhi nchini. Miaka 60 ya uhuru ,CCM mmetawala mmeshindwa kutatua changamoto ya migogoro ya ardhi nchini mtawezaje leo kwa kutoa "matamko " na kutoa miezi 6 huku miaka 60 mmeshindwa bwana Muenezi Mtoa Matamko?.

Migogoro mingi ya ardhi chanzo chake ni kushindwa kwa utekelezaji wa sera na mipango na ubunifu ,CCM mmeshindwa kutatua changamoto ya Ardhi nchini , mmeshindwa hata kutekeleza ilani yenu,sasa mmeamua kujificha kwenye mgongo wa matamko ya Bwana Muenezi.

Bwana Muenezi Mtoa Matamko, punguza kutoa matamko,matamko hayatasaidia kitu.Soma katiba yenu ya CCM ibara ya 107(2) a -e , inaelezea majukumu yako kama Muenezi . Jukumu lako la kwanza ni kushughulikia masuala ya itikadi na sera za CCM . Sera ni pamoja na "Ilani". kama unataka kuleta uwajibikaji basi vyema iwe kupitia ilani yenu sababu Wananchi watawapima kupitia ilani yenu,tujue kwanini mliyoahidi kuhusu Ardhi hamjatekeleza hadi sasa?. Na huu unapaswa kuwa uthibitisho wa kwamba CCM na serikali yake wameshindwa kutatua changamoto ya Ardhi nchini.

Mfano, ilani yenu CCM ya 2020,kurasa ya 116 kuanzia kifungu cha 72 mliahidi "Upangaji,Upimaji na umilikishaji wa Ardhi " hii ina maana mliahidi Ardhi zote nchini kupimwa . Bwana Muenezi Mtoa Matamko nikupe taarifa kutoka kwa Mtoa taarifa ya kwamba hadi sasa naongea na wewe Upangaji ,Upimaji na urasimishaji wa Ardhi nchini umefikia asilimia 25% ya vijiji vyote,Tume ya Mipango bora ya Ardhi mnaipa bajeti ndogo kwasababu sio kipaumbele chenu kutatua migogoro ya ardhi nchini kupitia kupima Ardhi yote.

Kwa tafsiri hiyo CCM mmeshindwa tangu awali kusimamia serikali yenu kuhakikisha mipango ya serikali ya muda mfupi, muda wa kati na mrefu inashabihiana na ahadi zenu na sera zenu mlizoahidi kwenye ilani ya 2020 . Ni wazi kwa tafsiri hii CCM na serikali yake mmeshindwa kazi ya kutatua changamoto za wananchi.Mwaka mmoja na nusu sasa kuelekea 2025 mmeshindwa kutekeleza ahadi yenu katika ilani yenu ya Upangaji, Upimaji na urasimishaji wa ardhi nchini (Ilani ya CCM kurasa 116. ).

ACT wazalendo katika ilani yetu 2020 kurasa wa 37, tulisema tutafuta gharama za Upimaji wa viwanja na Ardhi nchi nzima sababu tunaamini kupanga miji ni wajibu wa serikali sio Wananchi. CCM mmeshindwa kuipima nchi hii sababu sio kipaumbele kwenu ,mnawezaje kujipa kazi ya kukata matawi sasa badala ya shina ?.

Bwana Muenezi wa matamko,sasa mmemgeuza Waziri wa Ardhi kuwa mtatua migogoro ya ardhi hadi ngazi ya vijijini. Mmeshindwa kutekeleza Mikakati imara na ya muda mrefu kama tulivyoahidi ACT Wazalendo kwenye ilani yetu kurasa wa 37,kujengea uwezo stahiki Halmshauri za vijiji ,Kamati za Ardhi za vijiji,mabaraza ya ardhi ya vijiji katika usuluhishi (Mediation) na utatuzi wa migogoro ya ardhi huko huko chini, na pia kuwezesha rasilimali fedha mabaraza ya Wilaya na Mahakama ya ardhi katika kushughulikia migogoro ya ardhi. Badala yake mmegeuza wizara kuwa wasuluhishi wa Migogoro ya ardhi nchini badala ya kuweka mifumo imara nchini.

Bwana muenezi wa matamko,umempa miezi 6 Waziri Mkuu Majaliwa aratibu wizara 3, Wizara ya Tamisemi,Wizara ya Ardhi na Wizara ya Maliasili kushughulikia migogoro ya ardhi nchini. Bwana Muenezi wa matamko nikupe taarifa kutoka kwa Mtoa taarifa ya kwamba Serikali ya CCM 2019 iliagiza mawaziri 5 kwenda Kigoma -Kasulu kushughulikia mgogoro wa Ardhi Msitu wa Makere Kusini(Kagerankanda) walikwenda na hakuna mgogoro uliotatuliwa hadi sasa mgogoro bado upo.

Pia tar 16,Feb 2019 serikali ya CCM iligiza mawaziri 8 kwenda Mbarali-Mbeya kutatua mgogoro wa Ardhi wa GN.28 ya 2008 ila walienda zidisha mgogoro , hadi sasa mgogoro upo na umezidi mara dufu. Bwana Muenezi mlishindwa kutatua migogoro hii miwili ya ardhi Kigoma (Makere) na Mbarali (GN 28) ,mtaweza kutatua migogoro ya ardhi nchi nzima kwa miezi 6 uliyotoa Bwana Muenezi Mtoa Matamko ?.


Ahsante.

Abdul Nondo.

Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ACT Wazalendo Taifa.
1076601307.jpg
 
Mdogo wangu Abdul Nondo wewe ni Kiongozi wa Ngome ya Vijana ACT ( mchekupo wa CCM)

Naomba nikushauri jambo uache kutumikia huku wenzako wakineemeka hapo Chama chenu jiulize swali kwanini mpaka Leo unatembelea Boda boda?

juzi mvua imenyesha kubwa sana nakuona unajibanza kwenye daladala makumbusho huku umevaa barakoa kwa aibu?

Mwambie Zitto akununulie walau passo au jimmy kwa maana utaishia kutumiwa ukitane na vibaka wakutie panga

Wasalam
MIMI KAKA YAKO

GILBERT MASSAWE ( GM)
 
Mdogo wangu Abdul Nondo wewe ni Kiongozi wa Ngome ya Vijana ACT ( mchekupo wa CCM)

Naomba nikushauri jambo uache kutumikia huku wenzako wakineemeka hapo Chama chenu jiulize swali kwanini mpaka Leo unatembelea Boda boda?

juzi mvua imenyesha kubwa sana nakuona unajibanza kwenye daladala makumbusho huku umevaa barakoa kwa aibu?

Mwambie Zitto akununulie walau passo au jimmy kwa maana utaishia kutumiwa ukitane na vibaka wakutie panga

Wasalam
MIMI KAKA YAKO

GILBERT MASSAWE ( GM)
jiwe la utosi
 
Mdogo wangu Abdul Nondo wewe ni Kiongozi wa Ngome ya Vijana ACT ( mchekupo wa CCM)

Naomba nikushauri jambo uache kutumikia huku wenzako wakineemeka hapo Chama chenu jiulize swali kwanini mpaka Leo unatembelea Boda boda?

juzi mvua imenyesha kubwa sana nakuona unajibanza kwenye daladala makumbusho huku umevaa barakoa kwa aibu?

Mwambie Zitto akununulie walau passo au jimmy kwa maana utaishia kutumiwa ukitane na vibaka wakutie panga

Wasalam
MIMI KAKA YAKO

GILBERT MASSAWE ( GM)
Eeka mbacho
 
Kwa akili hizi naweza amini kuwa ulijiteka
Why una muattack mtu? Kwa mbwembwe na taarab
Inalisaidia nini taifa hili?
Why unasumbuliwa na katiba ya CCM?
Waache wafu wazikane
Jirekebishe hujachelewa bado !!
 
Mdogo wangu Abdul Nondo wewe ni Kiongozi wa Ngome ya Vijana ACT ( mchekupo wa CCM)

Naomba nikushauri jambo uache kutumikia huku wenzako wakineemeka hapo Chama chenu jiulize swali kwanini mpaka Leo unatembelea Boda boda?

juzi mvua imenyesha kubwa sana nakuona unajibanza kwenye daladala makumbusho huku umevaa barakoa kwa aibu?

Mwambie Zitto akununulie walau passo au jimmy kwa maana utaishia kutumiwa ukitane na vibaka wakutie panga

Wasalam
MIMI KAKA YAKO

GILBERT MASSAWE ( GM)
Kuniona tuu hujawahi niona ! Siku utaniona
 
Mdogo wangu Abdul Nondo wewe ni Kiongozi wa Ngome ya Vijana ACT ( mchekupo wa CCM)

Naomba nikushauri jambo uache kutumikia huku wenzako wakineemeka hapo Chama chenu jiulize swali kwanini mpaka Leo unatembelea Boda boda?

juzi mvua imenyesha kubwa sana nakuona unajibanza kwenye daladala makumbusho huku umevaa barakoa kwa aibu?

Mwambie Zitto akununulie walau passo au jimmy kwa maana utaishia kutumiwa ukitane na vibaka wakutie panga

Wasalam
MIMI KAKA YAKO

GILBERT MASSAWE ( GM)
Duh! Ina maana mwenyekiti wa ngome ya vijana ACT hana gari? Itabidi niongee na mwenyekiti wa UVCCM amsaidie mwenzake wa ACT kagari hata Vitz.
 
Fact-Check ,Fact-Check Kuhusu Migogoro Ardhi.

Kwenda kwa Muenezi wa Matamko Bwana Ndug.Paul Makonda.

Bwana Muenezi Mtoa Matamko umetoa tamko Kwaniaba ya chama kumpa Waziri Mkuu miezi 6 kushughulikia suala la migogoro ya ardhi nchini. Miaka 60 ya uhuru ,CCM mmetawala mmeshindwa kutatua changamoto ya migogoro ya ardhi nchini mtawezaje leo kwa kutoa "matamko " na kutoa miezi 6 huku miaka 60 mmeshindwa bwana Muenezi Mtoa Matamko?.

Migogoro mingi ya ardhi chanzo chake ni kushindwa kwa utekelezaji wa sera na mipango na ubunifu ,CCM mmeshindwa kutatua changamoto ya Ardhi nchini , mmeshindwa hata kutekeleza ilani yenu,sasa mmeamua kujificha kwenye mgongo wa matamko ya Bwana Muenezi.

Bwana Muenezi Mtoa Matamko, punguza kutoa matamko,matamko hayatasaidia kitu.Soma katiba yenu ya CCM ibara ya 107(2) a -e , inaelezea majukumu yako kama Muenezi . Jukumu lako la kwanza ni kushughulikia masuala ya itikadi na sera za CCM . Sera ni pamoja na "Ilani". kama unataka kuleta uwajibikaji basi vyema iwe kupitia ilani yenu sababu Wananchi watawapima kupitia ilani yenu,tujue kwanini mliyoahidi kuhusu Ardhi hamjatekeleza hadi sasa?. Na huu unapaswa kuwa uthibitisho wa kwamba CCM na serikali yake wameshindwa kutatua changamoto ya Ardhi nchini.

Mfano, ilani yenu CCM ya 2020,kurasa ya 116 kuanzia kifungu cha 72 mliahidi "Upangaji,Upimaji na umilikishaji wa Ardhi " hii ina maana mliahidi Ardhi zote nchini kupimwa . Bwana Muenezi Mtoa Matamko nikupe taarifa kutoka kwa Mtoa taarifa ya kwamba hadi sasa naongea na wewe Upangaji ,Upimaji na urasimishaji wa Ardhi nchini umefikia asilimia 25% ya vijiji vyote,Tume ya Mipango bora ya Ardhi mnaipa bajeti ndogo kwasababu sio kipaumbele chenu kutatua migogoro ya ardhi nchini kupitia kupima Ardhi yote.

Kwa tafsiri hiyo CCM mmeshindwa tangu awali kusimamia serikali yenu kuhakikisha mipango ya serikali ya muda mfupi, muda wa kati na mrefu inashabihiana na ahadi zenu na sera zenu mlizoahidi kwenye ilani ya 2020 . Ni wazi kwa tafsiri hii CCM na serikali yake mmeshindwa kazi ya kutatua changamoto za wananchi.Mwaka mmoja na nusu sasa kuelekea 2025 mmeshindwa kutekeleza ahadi yenu katika ilani yenu ya Upangaji, Upimaji na urasimishaji wa ardhi nchini (Ilani ya CCM kurasa 116. ).

ACT wazalendo katika ilani yetu 2020 kurasa wa 37, tulisema tutafuta gharama za Upimaji wa viwanja na Ardhi nchi nzima sababu tunaamini kupanga miji ni wajibu wa serikali sio Wananchi. CCM mmeshindwa kuipima nchi hii sababu sio kipaumbele kwenu ,mnawezaje kujipa kazi ya kukata matawi sasa badala ya shina ?.

Bwana Muenezi wa matamko,sasa mmemgeuza Waziri wa Ardhi kuwa mtatua migogoro ya ardhi hadi ngazi ya vijijini. Mmeshindwa kutekeleza Mikakati imara na ya muda mrefu kama tulivyoahidi ACT Wazalendo kwenye ilani yetu kurasa wa 37,kujengea uwezo stahiki Halmshauri za vijiji ,Kamati za Ardhi za vijiji,mabaraza ya ardhi ya vijiji katika usuluhishi (Mediation) na utatuzi wa migogoro ya ardhi huko huko chini, na pia kuwezesha rasilimali fedha mabaraza ya Wilaya na Mahakama ya ardhi katika kushughulikia migogoro ya ardhi. Badala yake mmegeuza wizara kuwa wasuluhishi wa Migogoro ya ardhi nchini badala ya kuweka mifumo imara nchini.

Bwana muenezi wa matamko,umempa miezi 6 Waziri Mkuu Majaliwa aratibu wizara 3, Wizara ya Tamisemi,Wizara ya Ardhi na Wizara ya Maliasili kushughulikia migogoro ya ardhi nchini. Bwana Muenezi wa matamko nikupe taarifa kutoka kwa Mtoa taarifa ya kwamba Serikali ya CCM 2019 iliagiza mawaziri 5 kwenda Kigoma -Kasulu kushughulikia mgogoro wa Ardhi Msitu wa Makere Kusini(Kagerankanda) walikwenda na hakuna mgogoro uliotatuliwa hadi sasa mgogoro bado upo.

Pia tar 16,Feb 2019 serikali ya CCM iligiza mawaziri 8 kwenda Mbarali-Mbeya kutatua mgogoro wa Ardhi wa GN.28 ya 2008 ila walienda zidisha mgogoro , hadi sasa mgogoro upo na umezidi mara dufu. Bwana Muenezi mlishindwa kutatua migogoro hii miwili ya ardhi Kigoma (Makere) na Mbarali (GN 28) ,mtaweza kutatua migogoro ya ardhi nchi nzima kwa miezi 6 uliyotoa Bwana Muenezi Mtoa Matamko ?.


Ahsante.

Abdul Nondo.

Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ACT Wazalendo Taifa.View attachment 2800550
Chama pekee cha upinzani ni chadema. Hivi vingine ni CCM {B}, vyama vya mifukoni.
 
Mdogo wangu Abdul Nondo wewe ni Kiongozi wa Ngome ya Vijana ACT ( mchekupo wa CCM)

Naomba nikushauri jambo uache kutumikia huku wenzako wakineemeka hapo Chama chenu jiulize swali kwanini mpaka Leo unatembelea Boda boda?

juzi mvua imenyesha kubwa sana nakuona unajibanza kwenye daladala makumbusho huku umevaa barakoa kwa aibu?

Mwambie Zitto akununulie walau passo au jimmy kwa maana utaishia kutumiwa ukitane na vibaka wakutie panga

Wasalam
MIMI KAKA YAKO

GILBERT MASSAWE ( GM)
Ahahahahahahahhahahahahahhahahahahahahahha yaani Nimecheka sana!

Usuombe mvua ya Dar ikukute maeneo na huna pakukimbilia lkn ulikuwa unajishetua kumbe wahuni wanakuchora tu
 
Back
Top Bottom