Waziri Mkuu akumbana na mabango mkoani Njombe

Waziri Mkuu akumbana na mabango mkoani Njombe

Sumulenga

Member
Joined
Jul 2, 2016
Posts
60
Reaction score
36
Habari,

Wazir mkuu akiwa ziarani wilaya ya Wanging'ombe katika kijiji cha Ihanja kata ya Mdandu. Wananchi wakijipanga na mabango kuhusu kero zao ikiwemo ya umeme.

Wanakijiji hawa walijawa na gadhabu kwani tangu Tanesco iweke nguzo mwaka 2001 hadi Leo umeme haujawekwa kijijin hapo.

Ndipo wakahoji iweje wao tu ingali vijiji vya jiran umeme upo?
Hali ilikuwa kama hivi katika picha
FB_IMG_1485016356001.jpg
FB_IMG_1485016350542.jpg
FB_IMG_1485016344420.jpg
FB_IMG_1485016338859.jpg
FB_IMG_1485016332496.jpg
 
Ujumbe wa mabangoni hausomeki. Mabango yanasemaje? Yanawasilisha ujumbe hasi au chanya kwa Waziri Mkuu na serikali yake?

Ingekuwa vizuri kama ungetuwekea hapa picha zinazoonyesha ujumbe uliomo katika mabango hayo waziwazi au tuwekee texts. Asante!
 
Jambo zuri walilofanya wananchi hao kuelezea yanayojiri walipo, vizuri wengi wangefanya haya sababu wanayasoma.

Na sio kulalamika tu, haswa wanaojificha kwenye mitandao na kuponda kila kitu kama vile wanasomeka.
 
Kutoa kero kwanjia ya amani ni vizuri sana,
Pongezi kwa wananchi hao
Naimani ujumbe umefika
 
Yani serikali imekutana na mabango mengi kuliko hata wahudhuriaji.

Tena hao wanakijiji wategemee umeme utafika hapo kijijini mwaka 2029 kwasababu huo ni mradi wa MCC uliositishwa na wahisani baada ya serikali ya CCM kupora ushindi wa Maalim Seif huko Zenji.
 
Dah,hayo mabango noma.Naona wamechoka kudanganywa maskini.Meneja wa TANESCO Njombe atoe maelezo ya kuridhisha vingineyo atumbuliwe.Tatizo la TANESCO ni kwamba kuna vihiyo wengi sana,tatizo ambalo limesababishwa na mfumo mbovu wa ajira.
Habari
Wazir mkuu akiwa ziarani wilaya ya Wanging'ombe katika kijiji cha Ihanja kata ya Mdandu. Wananchi wakijipanga na mabango kuhusu kero zao ikiwemo ya umeme.
Wanakijiji hawa walijawa na gadhabu kwani tangu Tanesco iweke nguzo mwaka 2001 hadi Leo umeme haujawekwa kijijin hapo. Ndipo wakahoji iweje wao tu ingali vijiji vya jiran umeme upo?
Hali ilikuwa kama hivi katika pichaView attachment 462323View attachment 462324View attachment 462325View attachment 462326View attachment 462327
 
Dah,hayo mabango noma.Naona wamechoka kudanganywa maskini.Meneja wa TANESCO Njombe atoe maelezo ya kuridhisha vingineyo atumbuliwe.Tatizo la TANESCO ni kwamba kuna vihiyo wengi sana,tatizo ambalo limesababishwa na mfumo mbovu wa ajira.
Meneja wa njombe hana cha kujibu,
Haya maswali muulizeni waziri jembe la Magufuli Prof. Muhongo aliyesema Tanzania inaanza kuuza umeme kwa nchi jirani.
 
Hivi kutoa ujumbe kwa njia ya miadhara ya kisiasa niya vurugu?
Muulize tu Magu akisimama kusalimia barabarani na tukimpokea na mabango 40 tu kama hayo ya Njombe tutaambiwa ni vurugu au tutalindwa vizuri na OCD wa eneo husika?
 
Back
Top Bottom