Waziri mkuu akimbia maswali leo bungeni

Waziri mkuu akimbia maswali leo bungeni

m.o.d.y

Member
Joined
May 22, 2011
Posts
25
Reaction score
2
Katika hali isiyo ya kawaida leo spika ametangaza kuwa hakutakuwa na maswali ya papo kwa papo kwa kuwa waziri mkuu hayupo.ndugu wana jf je hii ni ishara ya kitu gani?
 
Katika hali isiyo ya kawaida leo spika ametangaza kuwa hakutakuwa na maswali ya papo kwa papo kwa kuwa waziri mkuu hayupo.ndugu wana jf je hii ni ishara ya kitu gani?

Ni ishara kwamba ana majukumu mengine nje ya ukumbi wa Bunge.
 
Kwa Hali ya hewa waliyoichafua CCM kuhusiana na vurugu maeneo mbalimbali nchini, ni wazi maswali yangekua mengi kuliko majibu,
PM kasoma alama za nyakati!!!!
 
Kwa Hali ya hewa waliyoichafua CCM kuhusiana na vurugu maeneo mbalimbali nchini, ni wazi maswali yangekua mengi kuliko majibu,
PM kasoma alama za nyakati!!!!

Duh wamepumua nini?
 
Kwa hiyo Waziri mkuu na CCM wenzake wana nafasi ya kusikiliza mipasho tu au?

Hiki kipindi cha maswali na majibu ni wakati wa SITTA chini ya huyu asiyeelewa nini maana ya utawala wa sheria hakuna maana.
 
maji yamefika shingoni..mtoto wa mkulima kala kona..ala..
 
Kwi Kwiii Mizengo Pinda kweli ame-pinda kama ameanza mizengwe ya kukacha kipindi cha maswali
ya papo kwa papo na hiyo yote ni kumkimbia Tundu Lissu baada ya Jana waziri wake Celina
Kombani kuonjeshwa joto ya jiwe STAR TV.

But on serious note, hivi u-PM ni mtu individual siyo Institution? Haya ndiyo majibu mepesi ya
viongozi (Spika) kwa maswali magumu. Mbona Sitta na Magufuri huwa wana kaimu hiyo
nafasi kwanini leo wasiwajibike kujibu maswali. Na Kama kiongozi wa Serikali leo hayupo Bungeni
then kwanini bunge liendelee na shughuli zake?

Huu ujanja ujanja wa kijinga kukwepa hoja badala ya kujibu hoja ndio uliotufikisha hapa.
 
Katika hali isiyo ya kawaida leo spika ametangaza kuwa hakutakuwa na maswali ya papo kwa papo kwa kuwa waziri mkuu hayupo.ndugu wana jf je hii ni ishara ya kitu gani?

Mtoto wa mkulima asiyekuwa mkulima.....
 
anajua maswali ya katiba yangekuwa mengi na maswali magumu na hakika hana majibu sahihi sana ya maswali hayo.
kwanini asiwepo wakatia anajua leo ni siku yake
 
Kwani ofisi yake si ndio kiongozi wa shughuli za serikali bungeni? Sasa wanaomwakilisha leo kwanini wasimsaidie kujibu?

Kuna jambo lakimbiwa hapo.
Who is next on the run?
 
Back
Top Bottom