Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,894
- 155,914
Chama Cha MajiziWaziri wa Tamisemi Mh Mchengerwa amesema alishangazwa baada ya kuletewa bajeti ya manunuzi ya dola laki 5 kwa basi moja la mwendokasi !
Mchengerwa aliifutilia mbali hiyo bajeti baada ya kubaini ni sawa na kununua behewa la treni.
My take
Hawa wapigaji mbona hawachukuliwi hatua?
Rais Samia pia alishawahi kulalamika na kutukana stupid baada ya kugundua bei ya ndege imeongezwa mara 3 zaidi!
Pia uwanja wa mpira utakaojengwa Arusha ambao utakuwa mdogo kabisa wenye uwezo wa kuingiza watu elfu 30 tu kama ule wa New Amaan Zanzibar, bajeti yake imetengwa billion 286 !, hela ambayo ni nyingi mara nne kuliko uwanja wa Mkapa ambao unauwezo wa kuingiza watu zaidi ya elfu 60!
Je tabia hii ya kuongeza bei ya miradi tungeweza kweli kuhamishia serikali na kujenga ikulu Dodoma, kujenga bwawa ?