Waziri Mbarawa tumbua hawa walionunua rada sanamu ya hali ya hewa

Status
Not open for further replies.

Ngalikivembu

JF-Expert Member
Oct 6, 2010
1,959
872
Nampongeza Rais Magufuli kwa kutekeleza ahadi zake alizozitoa wakati wa kampeni. Tarehe 20. November 2015 alipolihutubia bunge aliahidi kutumbua majipu. Alisema amejipa kazi ya kutumbua majipu. Tumeona anatekeleza ahadi hii.
Kwenye utumishi kulioza sana. Nampongeza kwa tumbua tumbua hii. Waziri wake wa ujenzi na mawasiliano anafanya kazi nzuri. Na hakika tunajua sisi watumishi wa umma tulilala lakini pia tulikuwa tuna hujumu nchi kwa ufisadi.

Tangu aletwe wizara hii Mbarawa ameshatumbua majipu kadhaa kama kumtoa mkurugenzi mkuu wa tcaa na waandamizi wake.
Lakini leo ninachomwomba ni kutupia jicho wale waliohusika kununua rada ya hali ya hewa ambayo imefungwa huko mwanza yapata miaka miwili imepita sasa.

Cha kusikitisha ni kuwa rada hii haifanyi kazi na majibu ya wahusika wanasema hatuna umeme wa kutosha kuendesha mitambo hii. La ziada hatuna wataalamu kuendesha rada hii. Sasa maswali ni haya kabla ya kununua hawakuliona hili? Hawakujua kama hawana wataalamu? Billion 7 zimetumika kununua rada hii. Waziri Mbarawa ameenda mara mbili huko mwanza tulitegemea angeelezwa hili tatizo. Hebu jaribu kurudi huko kupata majibu ya maswali haya. Tumbua jipu hili.


===============
UPDATE Kutoka TMA
===============




JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA UJENZI,UCHUKUZI NA MAWASILIANO

MAMLAKA YA HALI YA HEWA


TAARIFA KWA UMMA


YAH: UFANISI WA RADA YA HALI YA HEWA MWANZA


Tafadhali husika na somo tajwa hapo juu na taarifa inasambaa kwenye mitandao ya kijamii


Mamlaka inapenda kukanusha taarifa zinazosambaa kuhusu kutokufanya kazi kwa Rada ya Hali ya Hewa iliyopo Mwanza. Taarifa sahihi ni kwamba Rada hiyo inafanyakazi kama ilivyopaswa vilevile tunapenda kuutarifu umma wa watanzania kuwa Mamlaka ya Hali ya Hewa ina wataalamu wa kutosha wa kuendesha Mitambo ya RADA za hali ya hewa tulizanazo. Aidha gharama halisi za ununuzi wa Rada hiyo si kama bilioni 7 kama ilivyosambazwa.


Kwa taarifa hiyo fupi, tunapenda kuisihi jamii kuacha kuichafua Mamlaka na Serikali kwa ujumla kwa taarifa zisizo rasmi zenye upeo hasi na pindi wanapohitaji kupata taarifa sahihi wasisite kuwasiliana na Ofisi zetu.


Tunawatakia kazi njema katika ujenzi wa Taifa.


IMETOLEWA NA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA.
 

Attachments

  • kanusho radar.pdf
    53.2 KB · Views: 54
Hoja nzuri sana hii, sijui wahusika wataiona..????
Nchi nyingi za kiafrica zinakuwa masikini kwasababu watu wake ni wajinga na waliokosa uzalendo kwa Nchi zao. Fikiria bil 7 zimetumika lakini kifaa kinaoza tu bila kutumika.kuna watu wanastahili kuuawa ndio pengine walio baki watashika adabu.hakuna umeme wa kutosha? wamekosa kisingizio.
 
Nampongeza Rais Magufuli kwa kutekeleza ahadi zake alizozitoa wakati wa kampeni. Tarehe 20. November 2015 alipolihutubia bunge aliahidi kutumbua majipu. Alisema amejipa kazi ya kutumbua majipu. Tumeona anatekeleza ahadi hii.
Kwenye utumishi kulioza sana. Nampongeza kwa tumbua tumbua hii. Waziri wake wa ujenzi na mawasiliano anafanya kazi nzuri. Na hakika tunajua sisi watumishi wa umma tulilala lakini pia tulikuwa tuna hujumu nchi kwa ufisadi.

Tangu aletwe wizara hii Mbarawa ameshatumbua majipu kadhaa kama kumtoa mkurugenzi mkuu wa tcaa na waandamizi wake.
Lakini leo ninachomwomba ni kutupia jicho wale waliohusika kununua rada ya hali ya hewa ambayo imefungwa huko mwanza yapata miaka miwili imepita sasa.

Cha kusikitisha ni kuwa rada hii haifanyi kazi na majibu ya wahusika wanasema hatuna umeme wa kutosha kuendesha mitambo hii. La ziada hatuna wataalamu kuendesha rada hii. Sasa maswali ni haya kabla ya kununua hawakuliona hili? Hawakujua kama hawana wataalamu? Billion 7 zimetumika kununua rada hii. Waziri Mbarawa ameenda mara mbili huko mwanza tulitegemea angeelezwa hili tatizo. Hebu jaribu kurudi huko kupata majibu ya maswali haya. Tumbua jipu hili.
akimaliza huko aje ujenzi kwenye mv dar 7.8 biliion na kivuko akifanyi kazi
 
Kumbe mambo ya RADA bado ni vimeo?!, tangu ile rada ya BAE, ilikuwa ni rada ya ulinzi kwa kutumia obsolate tech ndio tunayoiweza, migao ilikwenda hadi kwa mkuu wa kaya!, yule Msukuma Chenge ndie mkweli pekee aliyekiri kupokea mgao, watu wakadhani ni pesa nyingi, ndipo akauweka ukweli kuwa tule ni tujisenti tuu, wangeijua migao ya wengine, ndipo wangeelewa!.

Sasa imenunuliwa rada ya the modern tech, hatuna watu wa kuiendesha!. Wenzetu huanza na capacity building ndipo waje kununua, ila naamini by now vijana watakuwa tayari wako class!.

Pasco
 
Nampongeza Rais Magufuli kwa kutekeleza ahadi zake alizozitoa wakati wa kampeni. Tarehe 20. November 2015 alipolihutubia bunge aliahidi kutumbua majipu. Alisema amejipa kazi ya kutumbua majipu. Tumeona anatekeleza ahadi hii.
Kwenye utumishi kulioza sana. Nampongeza kwa tumbua tumbua hii. Waziri wake wa ujenzi na mawasiliano anafanya kazi nzuri. Na hakika tunajua sisi watumishi wa umma tulilala lakini pia tulikuwa tuna hujumu nchi kwa ufisadi.

Tangu aletwe wizara hii Mbarawa ameshatumbua majipu kadhaa kama kumtoa mkurugenzi mkuu wa tcaa na waandamizi wake.
Lakini leo ninachomwomba ni kutupia jicho wale waliohusika kununua rada ya hali ya hewa ambayo imefungwa huko mwanza yapata miaka miwili imepita sasa.

Cha kusikitisha ni kuwa rada hii haifanyi kazi na majibu ya wahusika wanasema hatuna umeme wa kutosha kuendesha mitambo hii. La ziada hatuna wataalamu kuendesha rada hii. Sasa maswali ni haya kabla ya kununua hawakuliona hili? Hawakujua kama hawana wataalamu? Billion 7 zimetumika kununua rada hii. Waziri Mbarawa ameenda mara mbili huko mwanza tulitegemea angeelezwa hili tatizo. Hebu jaribu kurudi huko kupata majibu ya maswali haya. Tumbua jipu hili.
Mimi naombeni msaada wa kujua kama haya majipu yanayotumbuliwa kama yalizaliwa na majipu hayo ama vimelea vya majipu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom