Waziri Makamba zidisha jitihada za kuifanya nchi ihamie kwenye gesi kikamilifu

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,619
46,259
Nchi hii inakabiliwa na hali mbaya sana ya uharibifu mkubwa mno wa mazingira unaotokana na kukata miti kwa ajili ya biashara mbaya ya mkaa na kuni. Kulima kwenye vyanzo vya maji nitazungumzia wakati mwingine.

Waziri, maeneo ya kanda ya ziwa uliyotembelea ndio kitovu cha biashara ya mkaa. Tabora, Shinyanga na Simiyu miti inakatwa haswa na mkaa unazalishwa na kuuuzwa bei rahisi sana, Unaweza kupata gunia la mkaa kwa Sh.15,000/=! kwenye hii mikoa. Kila kukicha hii mikoa inazidi kugeuka jangwa. Hii iwe alama nyekundu ya hatari.

Nilikusikia unamuambia mama mmoja uliyekuwa unampa jiko la gesi kwamba aachane na kuni kwa sababu zinazalisha sumu. Nataka niamini ukweli halisi wa moyoni mwako ni kwamba unauona mkaa ni uharibifu wa mazingira na ulifanya hivyo tu kwa yule mama ili kupunguza maneno kutoka kwa wakosoaji wa chama chako ambao kama ungesema mkaa na kuni ni janga kwa mazingira wangesema chama chako mmekuwa madarakani muda wote tangu kupata uhuru lakini mmeshindwa kuumaliza umaskini wa hao watu wanaotegemea mkaa.

Jambo la kushangaza, ni kwamba hata hata watu wa daraja la kati kiuchumi na matajiri wanaoishi mijini bado wanatumia sana mkaa na kuni. Watakuwa na jiko lao la gesi kwa ajili ya kupikia mama mwenye nyumba akiwepo na pia sio kwa vyakula vyote. Dada wa kazi inabidi apikie mkaa/kuni. Maharage, nyama, makande, wali, ugali mara nyingi vinapikiwa kwenye mkaa au kuni. Hawa hata umeme wa JHNPP ukianza kupatikana wataendelea tu na matumizi yao ya mkaa kama wasipodhibitiwa.

Mh Waziri, shirikiana na mawziri wengine kupandisha sana gharama za mkaa kwa kodi urasimu na vibali vya biashara mpaka watu wa mjini wauone mkaa kama anasa na waukimbie, halafu fanyeni bei na upatikanaji wa gesi uwe rahisi kwa njia hizo hizo.
 
i, Kwani sera ya gas Tanzania inasemaje?
ii, Kwani gas iliyomo kwenye mitungi inachimbwa hapa hapa Tanzania au inaagizwa nje?
iii, Vipi kuhusu makaa ya mawe hayatakuwa mbadala unaofaa wa mkaa kwa wale wasioweza kujikimu kwa kutumia gas?
iv, Hiyo mitungi anayogawa makamba anawapa na hela ya kujazia kila mwezi?
V, Pia hiyo mitungi anagawa kwa kila mkoa hapa nchi? Na anagawa kwa watu wenye hali ipi ya kiuchumi?
 
Kama ana nia ya dhati watu tuhamie kwenye matumizi ya gas kwanza adhibiti bei ya gas, kujaza gas ni gharama kuliko kununua gunia la mkaa na gunia la mkaa linatumika kwa muda mrefu kuliko gas, siku gas ikishuka bei na kuwa sawa au chini ya mkaa watu wataachana na mkaa
 
Haya maswali yako ni muhimu sana ila mengi yake sina majibu yake. Ninachofahamu gesi inapatikana Tanzania na ni mbadala mzuri na wa haraka kwa mkaa na kuni ili kusalimisha misitu ya nchi hii kama serikali ikiamua kutenda kwa nguvu na weledi wote.
i, Kwani sera ya gas Tanzania inasemaje?
ii, Kwani gas iliyomo kwenye mitungi inachimbwa hapa hapa Tanzania au inaagizwa nje?
iii, Vipi kuhusu makaa ya mawe hayatakuwa mbadala unaofaa wa mkaa kwa wale wasioweza kujikimu kwa kutumia gas?
iv, Hiyo mitungi anayogawa makamba anawapa na hela ya kujazia kila mwezi?
V, Pia hiyo mitungi anagawa kwa kila mkoa hapa nchi? Na anagawa kwa watu wenye hali ipi ya kiuchumi?
 
Makamba ana project yake binafsi ya Kujitangaza, akiwa ame lenga wananchi wamfahamu aki pitishwa CCM 2025. Hana ajenda ya Taifa huyo dogo.
 
Haya maswali yako ni muhimu sana ila mengi yake sina majibu yake. Ninachofahamu gesi inapatikana Tanzania na ni mbadala mzuri na wa haraka kwa mkaa na kuni ili kusalimisha misitu ya nchi hii kama serikali ikiamua kutenda kwa nguvu na weledi wote.
Gesi ya kupikia inapatikana Tanzania? Hadi hapa hupaswi tena kuendelea na huu uzi
 
i, Kwani sera ya gas Tanzania inasemaje?
ii, Kwani gas iliyomo kwenye mitungi inachimbwa hapa hapa Tanzania au inaagizwa nje?
iii, Vipi kuhusu makaa ya mawe hayatakuwa mbadala unaofaa wa mkaa kwa wale wasioweza kujikimu kwa kutumia gas?
iv, Hiyo mitungi anayogawa makamba anawapa na hela ya kujazia kila mwezi?
V, Pia hiyo mitungi anagawa kwa kila mkoa hapa nchi? Na anagawa kwa watu wenye hali ipi ya kiuchumi?
Nimegundua mleta Uzi ana uelewa mdogo kwenye gas alafu anataka hapohapo kutoa ushauri.
Anasema Anachofahamu Gas inapatikana Tanzania. Aiseeee
Tanzania hii hii tuwe na uwezo wa kuzaisha gesi ya kupikia? Hii hii Tanzania?? Kabisa tuzalishe LPG?? Tatizo kubwa humu watu ni kujifanya wanajua alafu ni weupe kichwani, hebu ona post ndefu Kama hii alafu aliyeleta hajui chochote kuhusu LPG na jinsi inavyozalishwa na inapotoka
 
Gesi ni ajenda ya Taifa,
Kupunguza matumizi ya mkaa na kuni vinapaswa kuwa ajenda ya Taifa.
Makamba ana project yake binafsi ya Kujitangaza, akiwa ame lenga wananchi wamfahamu aki pitishwa CCM 2025. Hana ajenda ya Taifa huyo dogo.
 
Angekuwa serious angejikita na hii gesi ya bomba la TPDC majumbani walau budget yao iwe 500 Billion badala ya 10 Billion ya sasa kwa mwaka.

Huo mkaa wa kanda ya ziwa hautumiki huko pekee hivyo wateja wao wakiugiwa bomba automatically itakuwa biashara isiyolipa.


Halafu huo utoaji mitungi uambatane na utoaji wa elimu ya safety and precautions,siyo kofia za kampeni hizo, ajali za moto wa gesi zimekuwa nyingi mno.
 
Angekuwa serious angejikita na hii gesi ya bomba la TPDC majumbani walau budget yao iwe 500 Billion badala ya 10 Billion ya sasa kwa mwaka.

Huo mkaa wa kanda ya ziwa hautumiki huko pekee hivyo wateja wao wakiugiwa bomba automatically itakuwa biashara isiyolipa.


Halafu huo utoaji mitungi uambatane na utoaji wa elimu ya safety and precautions,siyo njugu hizo, ajali za moto wa gesi zimekuwa nyingi mno.
Tatizo gas bei ipo juuu sn
 
Hakika, ila itachukua muda, na siyo kwa style ya kupeana majiko ya gesi...

Inapaswa mifumo ya mabomba ya gesi kusambazwa majumbani...
 
Angekuwa serious angejikita na hii gesi ya bomba la TPDC majumbani walau budget yao iwe 500 Billion badala ya 10 Billion ya sasa kwa mwaka.

Huo mkaa wa kanda ya ziwa hautumiki huko pekee hivyo wateja wao wakiugiwa bomba automatically itakuwa biashara isiyolipa.


Halafu huo utoaji mitungi uambatane na utoaji wa elimu ya safety and precautions,siyo njugu hizo, ajali za moto wa gesi zimekuwa nyingi mno.
Hivi hiyo gesi ya TPDC ya majumbani ikoje,wanaisambaza kama wanavyosambaza maji dawasco majumbani au na kwa maeneo yote

Ova
 
i, Kwani sera ya gas Tanzania inasemaje?
ii, Kwani gas iliyomo kwenye mitungi inachimbwa hapa hapa Tanzania au inaagizwa nje?
iii, Vipi kuhusu makaa ya mawe hayatakuwa mbadala unaofaa wa mkaa kwa wale wasioweza kujikimu kwa kutumia gas?
iv, Hiyo mitungi anayogawa makamba anawapa na hela ya kujazia kila mwezi?
V, Pia hiyo mitungi anagawa kwa kila mkoa hapa nchi? Na anagawa kwa watu wenye hali ipi ya kiuchumi?
Hiyo mitungi ya gas imetolewa nyuma ya mgongo wa Rostam Azizi,
 

Attachments

  • Pg-1-copy-696x464.jpg
    Pg-1-copy-696x464.jpg
    40.3 KB · Views: 2
  • makamba-pic2-data.jpg
    makamba-pic2-data.jpg
    105.2 KB · Views: 3
  • images-10.jpeg
    images-10.jpeg
    18.6 KB · Views: 3

Similar Discussions

Back
Top Bottom