Waziri Mahiga: Mkataba kusaka walioficha mabilioni Uswisi wasainiwa Tanzania

Nina amini Tanzania tunaweza kulinda na kutetea maslahi yetu huko nje. Je unafikiri hatuna makachero mahili wa kuweza kufanya kazi ya kusaka pesa zetu huko uswisi?. Hivi hakuna watanzania wowote wanaofanya kazi katika mashirika makubwa ya kikachero huko ulaya na marekani?. Hivi ni mara ya kwanza tanzania kufuatilia pesa huko ng'ambo? hujawahi kusikia kwamba account flani flani miaka ya 90 huko huko uswisi ziliwahi kufungwa kwa maslahi ya Taifa ni nani aliyefanikisha?

Tutunze maneno haya tutakuja kumbushana. Nasisitiza si kila kitu unaweza kubeza kwa sababu tu uko UKAWA.CCM, CUF Chadema nk. Tuwape muda serikali hii ni makini na inajua nini inafanya. Mimi ninafikiri tunajishaua tu hatukuambiwa kwamba kuna mkataba wanaingia na nchi ya uswisi ila sisi kwa mtazamo wetu mbaya tunajitoa ufahamu kwamba hichi ni kiini macho kivipi? Tushikamane na muda utafika nchi hii itakuwa na neema na uchumi mzuri zaidi Afrika na dunia nzima.
hili ni zao la elimu yetu mbovu
 
NASISITIZA, TAMBUA ZILIZOFICHWA HAPO STANBIC BANK KUTOKA ESCROW KWANZA. HUWEZI KUSHINDWA KUJUA ZA NYUMBANI UKAJUA ZILIZO NJE YA NCHI, VIPIIIII? AU MAIGIZO?
Nadhani za stanbic Bank zipo ktk track ktk ufuatiliaji,Za Escrow nakumbuka Bunge lilitoa maazimio.Na za Uswisi taratibu kwa mashirikiano ya Serikali zote mbili tutafika pazuri tu
 
tulia wewe umeshalishwa sumu kaa chini ikumalize
hapana bwana ila kama ni jina la Rais anaitwa Dr John Joseph Pombe Magufuli na kama ni chama chake ni Chama Cha Mapinduzi,nchi huru na una uhuru wa kutoa maoni yako katika kujenga nchi,kumbuka bado tuna safari ndefu sana katika kufikia maendeleo ya kweli.
 
Chief, salama lakini?
Salama chifu.

Mimi pia nimeona hiyo taarifa lakini kwa uelewa wangu ni kwamba kutakuwa na ushirikiano kwenye "administrative na key organizational changes" ili kuwezesha ufanisi kwenye ushirikiano.

Sasa hii administrative na key organizational changes inamaanisha kwamba kutakuwa na vitengo maalum upande wa Tanzania na Switzerland ambavyo vitashirikiana kwenye utekelezaji au administrative issues kama hiyo ya suala la fedha ambazo kama zipo ndani ya benki za huko wao Switzerland watawajibika kusaidia kufahamu ziliingiaje.

Hili haliondoi kile nilichokisema kwenye huu uzi Ukweli kuhusu Uswisi na siri za kibenki: Siasa za Uswisi ndiyo mwamuzi

Lakini linapokuja suala la kuonyesha taarifa za wateja, hapo ndipo haiwezekani, labda kuwe na strong case kweli kweli. Unaposema kuwasaidia kufahamu ziliingiaje, tayari hapo breach of secrecy inatokea; na sheria ya Uswisi itamlinda huyo mtu.

Kwa hiyo ushirikiano ni kwenye sheria, forensic accounting na auditing na pale wanapohitaji msaada kama kutoa notice basi wanazungumza na wizara ya fedha.

Sijaona kwenye taarifa ya Ubalozi na hata ya Federal Council, Bern zikitoa details hizo juu ya ushirikiano. Hivyo hizo ni assumptions zako tu, ambazo haziko proven. By the way, ukiongelea ushirikiano kwenye sheria, ninarudi kule kule juu ya siasa za Uswisi zilivyo sasa. Mabadiliko ya sheria zinazoruhusu banking secrecy siyo rahisi kufanyika kwa sasa.

Hivyo haijalishi ni lini fedha zisizo halali ziliingia kwenye mabenki nchini humo lakini makubaliano ya leo hayakuja tu.

Makubaliano ya leo yalianza na mazungumzo mwezi March mwaka jana na unaweza kusoma hapo chini sehemu yake:

"Approved by the Federal Council on 13 March 2015, the memorandum of understanding is intended in particular to support the Tanzanian government in its efforts to combat corruption. These efforts are also in the interests of a clean Swiss financial centre. The memorandum does not create any new rights or obligations with regard to international mutual assistance in criminal matters, but it does introduce some key administrative and organisational changes to ensure efficient cooperation. In particular, in the future the central authorities of both states (in Switzerland's case the Federal Office of Justice) will be able to deal with each other directly and support each other in the drafting of requests for legal assistance. The appendix to the memorandum also includes model requests which satisfy the formal requirements of both states."

Sijui ni kwanini hamtaki kuona na kuelewa hayo maandishi niliyoya-bold!! Kama makubaliano hayatengenezi commitments mpya juu ya Uswisi kutoa msaada katika masuala ya jinai, sasa nini itakuwa faida ya makubaliano hayo?

Hivyo inaonekana hili suala lilizimwa ghafla mwaka jana na baada ya Swistzerland kuona juhudi za serikali ya awamu ya tano katika kupambana na rushwa na mambo mengine ya kudhibiti fedha, ndiyo wakaamua kujikumbusha hii kitu ya mwaka jana.

You must be joking, right? Yaani unataka kusema Uswisi imeona juhudi za serikali ya awamu ya tano katika kupambana na rushwa? Unawafahamu waswisi kweli chifu? They standards and views of issues are the highest in the world! Ndiyo maana watu wengine wa Ulaya uwa wanawatania waswisi kuwa ni perfectionists. Sasa sijui juhudi gani hizo unazoziongelea ambazo zimeweza kuwafanya waswisi wavutiwe na serikali ya Magufuli!! Unajua nini chifu, hata mswisi aliye na siasa na misimamo ya mrengo wa kushoto akija Tanzania, hakuna jambo lolote ambalo linaweza kumvutia katika kupambana na rushwa na matumizi mabaya ya fedha za umma. Kwanza, atashangaa kuona Rais na viongozi wa serikali wakiendeshwa kwenye magari ya bei mbaya huku hospitali na huduma nyingine za msingi za kijamii ni mbovu. Pili, atashangaa kusikia Rais halipi kodi! Tena hili litam-put off kabisa. Kwa sababu pamoja na kuwa na sheria ambazo hazioni tax evasion kama kosa (haswa kwenye banking industry), waswisi ni walipa kodi wazuri na waaminifu sana. Kama ilivyo baadhi ya nchi zilizoendelea (nafahamu Marekani), mswisi kila mwisho wa mwaka ujaza tax returm forms kwa ajili ya kuonyesha mapato yake (mshahara na vyanzo vingine vyote vya mapato) yote kwa mwaka, mali zake, dini yake (huku kulipa kodi ya kanisa ndiyo kunam-identify mtu na dini yake - ingawa kodi inalipwa kwa serikali, kisha serikali inapeleka kwenye kanisa husika, ukiacha kulipa kodi inamaanisha umejivua uanakanisa), hali yake ya ndoa n.k. ili alipe kodi katika ngazi tatu: kodi kwa Confederation (nchi), kwa Canton (nafikiri ni kama mkoa au jimbo) na kwa Commune (ndiyo ngazi ya mwisho ya kiserikali, hivyo ni kama kijiji kwa Tanzania) anapoishi. Sasa kwa mswisi anayelipa kodi kwa namna hii, sidhani kama ataona kuna juhudi zozote za maana za Magufuli, kwa sababu waswisi wanathamini sana honesty.

Sasa Magufuli isn't honest katika juhudi zake hizo; he has yet to walk the talk. Hapambani na rushwa na matumizi mabaya ya fedha za umma ni an honest manner. Hadi sasa sijamsikia akizungumzia ufisadi wa IPTL, Lugumi, Richmond/Downs/Symbion, Escrow, EPA na mikataba ya kinyonyaji ya madini. Utasemaje waswisi wameona juhudi za mtu ambaye amesema mara kadhaa 'hafukui makaburi'? Sasa kwa taifa kama Tanzania, ambalo misingi ya rushwa kubwa imejengwa na serikali za awamu zilizopita (haswa kuanzia kwa Mkapa), utapambana vipi na rushwa bila 'kufukua makaburi'? Au Magufuli anaogopa kivuli chake cha uuzaji wa nyumba za serikali na ununuzi wa ferry used kwa bei ya ferry mpya?

Hata hivyo Switzerland wamekuwa wakitoa ushirikiano na nchi kadhaa katika kufahamu kama wananchi wanalipa kodi kabla ya kuweka fedha huko.

Mwaka jana mwezi wa 11, raia wa Ugiriki walichunguzwa katika taarifa hiyo hapo chini:

Nchi zingine kama Uingereza nao wamekubaliana tangu mwaka 2013 na Switzerland kushirikiana kwenye masuala ya kodi kufahamu wale raia ambao wanakwepa kodi nchini Uingereza na kuweka fedha zao huko Uswiss.

Mwaka huohuo Marekani nayo ilikubaliana na Uswiss kuwezesha kufuatiliwa wale awote ambao wameficha fedha huko katika habari hii:

Switzerland And United States Reach Agreement On Swiss Bank
Last Updated: October 18 2013


Mwaka 2010 Ujerumani nao walitaka orodha ya wakwepa kodi ambao wameficha fedha zao Geneva:

Swiss Bank Data Offered to Germany

Pressure Rises About Secret Accounts

Sijui kama ulisoma ule uzi ninaoelezea kwa mapana siasa za Uswisi. Naona hapa umetaja nchi za Ulaya na Marekani. Sasa sijui unataka kusema kwamba katika mizani ya siasa za kimataifa, waswisi wanaiweka Tanzania sawa na Ulaya na Marekani? Chifu, seriously? Nchi inayoongozwa na siasa za nationalism, isolationism, pro-Europeanism, national conservatism n.k. iitazame Tanzania kwa jicho sawa na lile linalozitazama nchi nyingine za Ulaya na Marekani?!??

By the way, umeweka taarifa (zilizo za zamani) zinazoonyesha nchi hizo kutaka orodha na kukubaliana tu. Lakini hujasema kama zilifanikiwa kupata orodha; jambo ambalo naamini huwezi kuleta taarifa zake. Kwani kama msingi ni tax evasion, hapo hakuna kitu. Hivi unajua kuna baadhi ya Cantons za Uswisi zinatumia tax heavens (tax evasion) kama incentive ya kuvutia wawekezaji? Huku kila Canton inajitungua sheria zake za kodi kutokana na matakwa na mazingira yao. Hivyo, siyo ajabu Cantons kutofautiana kwenye sheria za kodi. Yaani kama Tanzania inaenda na gia ya 'wakwepa kodi', itakuwa vigumu sana kufanikiwa; kwani lazima 'ukwepaji kodi' huo uwe defined na sheria za Uswisi, jambo ambalo litapelekea kushindwa. Kwani kinachoku-defined ukwepaji kodi Tanzania, kwa Uswisi siyo ukwepaji kodi. Sasa sijui utajenga kesi gani hapo.


Kesi hizi na zingine nyingi tu zipo arounbd tokea mwaka huohuo wa 2005 ambao umekuwepo huko Uswiss na ungeweza kufahamu kinachoendelea khasa masuala haya ya fedha za kutumwa kutoka nje.

Chifu, labda uni-enlighten, maana kama msingi wa repatriation ni tax evasion, hapo hakuna kesi kwa Uswisi, haswa kwa kuangalia fedha zilizomo kwenye mabenki.

Na katikati ya mwaka huu Jumuiya ya Ulaya walizungumza na Panama ili kutaka kushirikiana kwenye masuala khasa ya data sharing kuona ni watu wangapi khasa na thamani ya fedha walizo nazo huko Uswiss baada ya ile orodha ndeefu kutoka na TAKUKURU wanayo nakala..

Hapa sijaelewa. Sasa TAKUKURU kuwa na hiyo nakala kunasaidia nini? Pia umetaja Jumuiya ya Ulaya, unataka kusema nini? Sijui kama unafahamu kwamba Uswisi siyo mwanachama wa Jumuiya ya Ulaya. Uswisi ni mwanachama wa European Free Trade Association tu (yaani mahusiano na ushirikiano kati ya Uswisi na Jumuiya ya Ulaya yanafanyika kupitia bilateral sectoral agreemens tu), uanachama unawafanya waswisi watumie za single market katika kutembea na kufanya kazi kwenye nchi zilizo wanachama wa Jumuiya hiyo. Sasa hayo makubaliano ya Jumuiya ya Ulaya na Panama hayawezi kuathiri sheria na misimamo ya Uswisi katika banking secrecy.

Pia katikati ya mwaka tulisikia jinsi wachunguzi kutoka Marekani walivyoivamia FIFA mjini Geneva na kuwakamata baadhi ya maofisa wake baada ya kuchunguza accounts zao ambazo zikituna kwa muda mrefu sana.

Kwanza, FIFA HQ hayapo Geneva, yapo Zurich; yamekuwa Zurich mwaka mmoja baada ya mimi kufika Uswisi. Pili, hao majamaa tayari walikuwa wana criminal charges kule Marekani, na sikumbuki charges zao kuhusishwa na tax evasion. Nafikiri charges zilikuwa ni upokeaji wa rushwa; na tayari majamaa yalikuwa yamefunguliwa kesi Marekani. Hivyo Marekani wakaiomba Uswisi iwasaidie kuwakamata na kuwa extradited.

Tumeshuhudia Sepp Blatter na Platini waliachia ngazi kutoka kwenye taasisi hiyo kubwa duniani yote hiyo ni baada ya makubaliano hayahaya ya hiki tunachokiona kikifanywa na nguli wa diplomasia Dr Mahiga na waswiss.

What are talking bruh? Yaani kukamatwa kwa Blatter ni baada ya makubaliano gani? Hivi unafahamu kama Blatter ni mswisi? By the way, Blatter anatoka kwenye Canton inayoitwa Valais, ambayo stereotype yake (miongoni mwa waswisi) ni kwamba watu wa Valais na Valais yenyewe ni corrupt. Blatter aliachia ngazi kutokana na tuhuma za rushwa. Sasa sijui kuna makubaliano gani hapo ambayo unayaongelea!!

I thought you were serious and know what you are talking about bruh! But, after hili la Blatter na kufikiri Uswisi ni mwanachama wa EU, nimeona unaleta siasa tu. Nime-confirm hii suspicion kwa ulichokiandika juu ya Mahiga. Licha ya kukubali kwamba he is a seasoned diplomat. Lakini so far, he hasn't done anything special to live to his standard. And I can assure you, Mahiga knows hili suala la banking secrecy siyo rahisi kama mnavyolichukulia.

Ukiangalia msururu huo wa kesi hizo utaona kwamba zote zinalingana kwenye administyrative issues na hiyo ndiyo key.

Hivyo kwa Tanzania ni hatua kubwa sana na serikali ya awamu ya tano inasogea kidogokidogo kuelekea kuwatambua wale ambao waliiba fedha au kufanya ufisadi na wameficha hizo fedha huko Uswiss.

Kwanza, sijaona kesi yoyote hapo juu! Hiyo ya Blatter na wenziwe haihusiani na banking secrecy as such. Pili, mpaka Tanzania iwafungulie criminal charges hao watu 'walioficha' pesa Uswisi ndiyo inaweza kuwa na chance ya ku-make a case for repatriation. Tatizo linakuja: Tanzania itawafungulia hao watu criminal charges kwa misingi ipi? Kama wakifungua kwa misingi ya tax evasion, watagonga mwamba.
 
Kwa mwendo huu msonganzila ifunguliwe haraka wazee wa mjini wote watalazwa huko
 
View attachment 430265

Serikali ya Tanzania na Uswisi zimesaini Mkataba utakaowawezesha Makachero wa Tanzania kwenda nchini Uswisi na kufanya uchunguzi katika mabenki ya huko ili kupata taarifa sahihi za walioficha mabilioni toka Tanzania.

Mkataba huo umesainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dr Augustine Mahiga na Balozi wa Uswisi nchini Florence Mattli.

Hata hii ni moja ya hatua muhimu ya Serikali awamu ya tano katika kudhibiti matumizi mabaya ya madaraka na fedha za umma.
========================

HUKU kukiwepo na dhana ya kuwa kuna Watanzania wanaotorosha fedha na kuzificha katika mataifa mbalimbali ikiwemo Uswisi, hatua moja muhimu imefanyika katika kukabili suala hilo, baada ya serikali ya nchi hizo mbili, kusaini mkataba muhimu.

HabariLeo Jumapili imebaini kufikiwa kwa makubaliano ya ushirikiano muhimu wa kisheria kwenye masuala ya jinai, unaolenga kuwajengea uwezo makachero wa Tanzania, kuchunguza masuala mbalimbali ya kiuhalifu nchini Uswisi.

Mkataba huo umeenda mbali zaidi, kwa kuweka wazi kuwa kuanzia sasa makachero hao, wanaweza kuchunguza fedha za Watanzania zilizohifadhiwa nchini Uswisi, tofauti na awali ambapo sheria za nchi hiyo zilikuwa zinazuia.

Mkataba huo umesainiwa hivi karibuni wakati wa Maadhimisho ya miaka 50 ya ushirikiano kati ya Tanzania na Uswisi. Uswisi ni nchi inayosifiwa kuwa na huduma bora za kibenki huku ikiwa na sheria kali zinazowalinda wateja wake.

Mkataba wa makubaliano hayo, ambao umeleta mwanga katika kukabiliana na usiri wa fedha hizo, ulisainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Augustine Mahiga na Balozi wa Uswisi nchini, Florence Mattli.

Akizungumza na gazeti katika mahojiano maalumu kuhusu mkataba huo, Balozi Mahiga alisema kuwa katika kuendeleza ushirikiano mzuri baina ya nchi hizo, Tanzania itanufaika na ruhusa hiyo ya kufuatilia akaunti za fedha Uswisi.

Alisema kuwa kipengele hicho, kimekubaliwa kwenye makubaliano na kwa sasa hakuna tena kikwazo kitakachoizuia Tanzania kuchunguza akaunti hizo.

Alisema kuwa hatua hiyo inatokana na Serikali ya Uswisi pia kuridhishwa na namna ambavyo Tanzania imekuwa ikipambana na vitendo vya rushwa na ufisadi, kwa lengo la kuwaletea maendeleo wananchi wake chini ya uongozi wa Rais John Magufuli.

Alisema, Uswisi imekuwa ni rafiki mkubwa wa Tanzania tangu enzi na enzi huku ikiisaidia katika uboreshaji wa sekta mbalimbali.

“Kweli hiyo ni hatua nzuri kwa Tanzania hasa kwa kipindi hiki ambapo Serikali ya Awamu ya Tano imekuwa ikikabiliana na rushwa na kila aina ya ufisadi na kwa hiyo ruhusa hii itasaidia kulinda fedha zetu kutoroshwa,” alisema Balozi Mahiga.

Akijibu swali ni lini serikali itakuwa tayari kupeleka makachero nchini humo, kuchunguza madai ya kuwepo kwa Watanzania walioficha fedha kwenye benki za nchini humo, Balozi Mahiga alisema; “Siwezi kusema ni lini hatua hiyo inaweza kuanza kuchukuliwa kwa kuwa zipo mamlaka zinazohusika na utekelezaji wake, ila ninachoweza kusema ni kuwa hatua iliyofikiwa ni ya msingi kwetu kama nchi.”

Zitto apongeza Mkataba Akitoa maoni yake kuhusu makubaliano hayo, Mbunge wa Kigoma Mjini, Kabwe Zitto (ACT – Wazalendo ), mmoja wa wabunge ambaye amekuwa akilizungumzia suala la ufichwaji wa mabilioni ya fedha nje ya nchi, aliliambia gazeti hili kuwa kipengele hicho kwenye mkataba huo ni kizuri na kitasaidia kupatikana kwa fedha zilizofichwa katika benki za Uswisi.

Alitumia nafasi hiyo kuipongeza serikali kwa uamuzi huo uliofikiwa na kusema ni hatua ya kimafanikio, hasa ikizingatiwa kuwa fedha hizo zinatokana na nguvu za wanyonge, ambapo pia zilipatikana kinyume na sheria. Balozi Mattli, alisema kuwa ushirikiano kati ya Tanzania na Uswisi, umekuwa ukiimarika zaidi kila siku, na kuwa nchi hiyo itaendelea kuisaidia Tanzania kwa hali na mali.


Chanzo: Habari Leo
Kama Serikali ya tz inadhani au inafikiri kuna Nchi itakubali mabilioni yaondolewe kizembe kwenye mabenki yao basi watakua wanaota ndoto za mchana, actually watakua wanaota ndoto nyevu. Tanzania lazma waweke kitu kingine mezani ili situation iwe win win. Mahiga awe makini asije kua kama Membe ambaye alishindwa kuweka offer nzuri mezani kwenye suala la chenchi ya rada tukaishia kupewa vitabu.
 
Kama Serikali ya tz inadhani au inafikiri kuna Nchi itakubali mabilioni yaondolewe kizembe kwenye mabenki yao basi watakua wanaota ndoto za mchana, actually watakua wanaota ndoto nyevu. Tanzania lazma waweke kitu kingine mezani ili situation iwe win win. Mahiga awe makini asije kua kama Membe ambaye alishindwa kuweka offer nzuri mezani kwenye suala la chenchi ya rada tukaishia kupewa vitabu.
Mazito hayo tena,nadhani Dr Mahiga ni Diplomat mzoefu sana ktk medani hizo za kijasusi he knows what is doing! Na hili suala ni multi sectoral,ondoa shaka, let's give them time na tusubiri matokeo.
 
Between the lines namaanisha huyu mwizi hawezi kukamata mwizi...hapambani na mafisadi papa huyu mtu,anaishia kwa vidagaa tu,lugumi na escrow hata kuvitaja anaogopa,nyinyi mnaamini blah blah zake!!zitto alishatoaga majina ya watu walioficha pesa nje,aanze na hayo!!!!
baba alishasema anaanzia alipopakuta hayo yaliyopita kufa nayo wewe. kama ni makaburi kachimbue wewe mikono c unayo
 
baba alishasema anaanzia alipopakuta hayo yaliyopita kufa nayo wewe. kama ni makaburi kachimbue wewe mikono c unayo
Mbona richmond wanalipwa hadi kesho,mbona escrow tunalipia na juzi tumeshindwa kesi na januari majizi tanesco yanapandisha bei ya umeme kulipa deni...unaongea ujinga gani wewe!!!!?
 
Mazito hayo tena,nadhani Dr Mahiga ni Diplomat mzoefu sana ktk medani hizo za kijasusi he knows what is doing! Na hili suala ni multi sectoral,ondoa shaka, let's give them time na tusubiri matokeo.
Yap, mimi nampa worning tu. Tujifunze kwa Iran. Mabilioni ya serikali ya Irani yalikuwa freezed marekani kutokana na vikwazo. Baada ya vikwazo Irani ikajua kabisa there is no way US akakubali pesa yoote iondoke hivi hivi so akaamua kununua ndege 400. So na sisi tuwe makini na mikakati yetu.
 
Yap, mimi nampa worning tu. Tujifunze kwa Iran. Mabilioni ya serikali ya Irani yalikuwa freezed marekani kutokana na vikwazo. Baada ya vikwazo Irani ikajua kabisa there is no way US akakubali pesa yoote iondoke hivi hivi so akaamua kununua ndege 400. So na sisi tuwe makini na mikakati yetu.
OK I know that about Iran,na kwa Dr Mahiga hopeful precaution zote zitakuwa zimeangaliwa kwa umakini sana leading to reach the desired target ktk makubaliano yaliyowekwa.
 
Naipongeza serikali kwa hatua hii nzuri ila itabidi pia madaktari wa magonjwa ya moyo waongezwe nchini kwani tusipoangalia mafisadi wangi watapoteza maisha kwa mshtuko wa moyo.
 
Mbona richmond wanalipwa hadi kesho,mbona escrow tunalipia na juzi tumeshindwa kesi na januari majizi tanesco yanapandisha bei ya umeme kulipa deni...unaongea ujinga gani wewe!!!!?
wewe acha ushamba hukumu za mahakama huwezi ingilia. hayo maden yalishatolewa hukumu na tanzania lazima kulipa. basi kama ndo hivyo na deni la taifa lisilipwe maana hajakopa makugufuli. mbona ulisemi na hilo.
 
wewe acha ushamba hukumu za mahakama huwezi ingilia. hayo maden yalishatolewa hukumu na tanzania lazima kulipa. basi kama ndo hivyo na deni la taifa lisilipwe maana hajakopa makugufuli. mbona ulisemi na hilo.
tunalipia pesa iliyoibiwa wazi na magu anajua hilo,swala sio mahakama swala tunalazimika kulipia hela zilizopigwa na maccm
 
wewe acha ushamba hukumu za mahakama huwezi ingilia. hayo maden yalishatolewa hukumu na tanzania lazima kulipa. basi kama ndo hivyo na deni la taifa lisilipwe maana hajakopa makugufuli. mbona ulisemi na hilo.
ata kama zimeibiwa maamuzi ya mahakama lazima yafatwe. magufuli kaingia hukumu tayari ishatolewa, sasa we unataka akatae maamuzi ya mahakama
 
This is shit tunawajua kabla hata hawajazipeleka huko ulaya richmond lugumi epa kwani hawafahiki hebu wasitutie gharama nyingine ya kujifanya wanaenda ulaya kuchunguza
 
Back
Top Bottom