Waziri Maghembe: "TANESCO, ukiritimba too much"

Waziri Maghembe: "TANESCO, ukiritimba too much"

EMT

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
14,477
Reaction score
15,347
Waziri wa maji, Prof Jumanne Maghembe ameelezea kukerwa kwake na shirika la umeme nchini (TANESCO) kwa madai limeshindwa kufikisha umeme vijijini na hivyo miradi ya maji kusuasua.

Kadhalika waziri huyo ametamani kuwapo kwa shirika mbadala ambalo litatoa ushindani kwa TANESCO ili iweze kutekeleza shughuli zake na hivyo miradi ya maji kukamilika kwa watati.

"Tungekuwa na mashirika mengine ya umeme tungeweza kufungiwa umeme haraka, lakini kwa vile ni TANESCO peke yake, sasa wananchi hawana maji…. TANESCO, ukiritimba too much," alisema.

Profesa Maghembe alisema hayo wakati anazindua mradi wa usambazaji majisafi katika kata ya Kiboroloni na viunga vyake. Aidha waziri huyo alisema kati ya vijiji hivyo 74, ni vijiji 28 ambavyo miradi yake imekamilika na wananchi wanapata huduma hiyo huku Vijiji 17 miradi yake ipo katika hatua za mwisho lakini tatizo lililopo ni kukosekana kwa umeme.

"Lakini kwa kweli tatizo tulilonalo sasa ni Tanesco…. Kwa muundo walionao ni lazima TANESCO wapandishe soksi zao juu," alisema.

Source: Waziri Maghembe azindua mradi wa maji Kiboriloni, asema "TANESCO ukiritimba too much"inakwamisha mipango; Atamani ipate mshindani - wavuti.com
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Viongozi wa serikali ya Ccm wamelogwa, hawajui watendalo, kama waziri anaongea huu ugoro sisi hohehahe tusemeje??? Majanga natupu hiki chama
 
Tanesco ni hovyo kabisa,
Janga la nchi hii
 
Huyu Waziri ni majanga, huko vijijini anaitwisha mzigo TANESCO! Looh, wakati huku mjini Dawasco/dawasa walikatiwa umeme wakiwa wanadaiwa bil.6, huku taasisi za serikali ikiwemo na wizara yake na wakubwa wenzake wanaadaiwa zaidi ya bil.40 za maji
 
Huyu wazuri ameshindwa kuyasema hayo kwenye baraza la mawaziri, analalamika kwa wananchi kama vile uongozi wa Tanesco hupigiwa kura na wananchi,

Waziri anatakiwa kutambua kuwa moja ya tatizo kubwa linalouwa Tanesco ni serikali yenyewe
 
Huyu waziri ameshindwa kuyasema hayo kwenye baraza la mawaziri, analalamika kwa wananchi kama vile uongozi wa Tanesco hupigiwa kura na wananchi,

Waziri anatakiwa kutambua kuwa moja ya tatizo kubwa linalouwa Tanesco ni serikali yenyewe kwa kuwa na madeni makubwa kwa shirika hilo.
 
Huyu Waziri ni majanga, huko vijijini anaitwisha mzigo TANESCO! Looh, wakati huku mjini Dawasco/dawasa walikatiwa umeme wakiwa wanadaiwa bil.6, huku taasisi za serikali ikiwemo na wizara yake na wakubwa wenzake wanaadaiwa zaidi ya bil.40 za maji
Kwani maghembe siyo mzigo? Kama hayo uliyoyasema ni kweli basi yeye ni mzigo mzito.
 
Huyu waziri naye hajitazami, ameshindwa kusambaza maji vijijini analalamikia umeme, unadhani wananchi wa vijijini wanashida ya umeme! watu wanataka maji ili waache kuamka usiku wa manane kwenda kuchota maji, watoto hawaendi shule badala yake wanaenda kutafuta maji. Uishasikia mtu akatoka kwake kwenda kuufuata umeme? Anatkiwa aone aibu.

Waziri wa maji, Prof Jumanne Maghembe ameelezea kukerwa kwake na shirika la umeme nchini (TANESCO) kwa madai limeshindwa kufikisha umeme vijijini na hivyo miradi ya maji kusuasua.

Kadhalika waziri huyo ametamani kuwapo kwa shirika mbadala ambalo litatoa ushindani kwa TANESCO ili iweze kutekeleza shughuli zake na hivyo miradi ya maji kukamilika kwa watati.

"Tungekuwa na mashirika mengine ya umeme tungeweza kufungiwa umeme haraka, lakini kwa vile ni TANESCO peke yake, sasa wananchi hawana maji…. TANESCO, ukiritimba too much," alisema.

Profesa Maghembe alisema hayo wakati anazindua mradi wa usambazaji majisafi katika kata ya Kiboroloni na viunga vyake. Aidha waziri huyo alisema kati ya vijiji hivyo 74, ni vijiji 28 ambavyo miradi yake imekamilika na wananchi wanapata huduma hiyo huku Vijiji 17 miradi yake ipo katika hatua za mwisho lakini tatizo lililopo ni kukosekana kwa umeme.

"Lakini kwa kweli tatizo tulilonalo sasa ni Tanesco…. Kwa muundo walionao ni lazima TANESCO wapandishe soksi zao juu," alisema.

Source: Waziri Maghembe azindua mradi wa maji Kiboriloni, asema "TANESCO ukiritimba too much"inakwamisha mipango; Atamani ipate mshindani - wavuti.com
 
Hawa watu wamechoka kabisa kwa kweli!!!!!
Hivi ule mnara kabla ya kushindwa kuelewana sababu ilikuwa nini vile???!!!!
 
Maghembe alishashindw kazi siku nyingi. Mawaziri wengine sijui walingiaje serikalini.Hivi huyu si yupo kwenye list ya mzigo!
 
tanesco ni hovyo kabisa,
janga la nchi hii

nyie mnawalea hawa tanesco, hili ni shirika la matajiri nasi masikini tuchukue hatua jamani dhidi yao.

Jamani kuna solar siku izi mchina ametufaa, zinawaka km kawaida jamani, tuwahache matajiri waliĹee shirika lao.

Ajabu ati elf20 nimenunua leo unit8 tu, naliona ili li tanesco likifa km ilivo makabulini ttcl ilotzarau enzi izo ikiwa na ukilitimba peke yake
 
Hata hivyo hii ni changamoto kubwa ya uendeshaji wa miradi ya maji vijijini, kwani ukiangalia mamlaka kubwa tu zinashindwa kulipia gharama za umeme ili wapate maji, sasa kwa mwananchi wa kawaida wa kijijini hata umeme ukifika. gharama za kila mwezi za umeme zitamshinda tu, ukizingatia na umeme ulivyopanda ni balaa. Watanzania/wataalam bado mna kazi ya kutafuta njia mbadala ya kutoa huduma ya maji uko vijijini ya gharama nafuu
 
Viongozi wa serikali ya Ccm wamelogwa, hawajui watendalo, kama waziri anaongea huu ugoro sisi hohehahe tusemeje??? Majanga natupu hiki chama

Chuki mbaya sana ukishapandikizw hujitambui kabisa. Kuwa mpinzani haina uwe mpingaji wa kila kitu mkuu.
 
nyie mnawalea hawa tanesco, hili ni shirika la matajiri nasi masikini tuchukue hatua jamani dhidi yao.

Jamani kuna solar siku izi mchina ametufaa, zinawaka km kawaida jamani, tuwahache matajiri waliĹee shirika lao.

Ajabu ati elf20 nimenunua leo unit8 tu, naliona ili li tanesco likifa km ilivo makabulini ttcl ilotzarau enzi izo ikiwa na ukilitimba peke yake

Kuna haja ya kuwa na mashirika mengi ya umeme kama yalivo makampuni ya simu ili watu tuchague. Tanesco ovyo kbx
 
Kweli Tanesco wanazingua sana sio miradi ya maji tu kutofika bali Tanesco ndio wanadidimiza hata uchumi wetu. Ifike wakati tuwe na mashirika mengi na si kutegemea hili shirika la vigogo
 
Nakumbuka huyu naye ni mmoja wa wale mizigo. Hivi maneno haya ni ya kuongea waziri kwa wananchi? Wananchi wanachotaka ni maji. Hizi porojo kaongee na waziri mwenzako wa nishati ambaye nilisikia nae anakudai ma bilioni ya pesa za bili ya umeme. Lipa pesa uungiwe umeme maeneo unayotaka. Coconut kabisa...!
 
Nahis wengine mmetushika na hii mbinu yenu hakika sio uongo
Gharama za umeme zipo juu zimepanda sawa, hatukatai
Lkn ni mitambo gani isiyolekebishwa karibu mwezi mzima watu tunalala giza
ili hali umeme upo eti Network inasumbua (kuna tatzo la kiufundi)
-Kweli kama ndo mbinu ya kuzima mitambo ili swala la mgao litimie, kwa hili tumepatikana wengine

Wadau nauliza kulikuwa na haja gani ya Tz kukimbilia Digital na wakati uwezo wetu ni mdogo na hili zigo digitali ni kubwa????
 
Back
Top Bottom