Waziri Lukuvi nisaidie, ni mwezi wa pili sasa nasubiri saini ya kamishna wa ardhi ili niweze kupata hati

manyusi

JF-Expert Member
Mar 3, 2009
292
170
Muheshimiwa William Lukuvi kwanza nikupongeze kwa jitihada zako katika wizara ya Ardhi, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni umejitahidi kwa kadiri unavyoweza na angalau sasa kuna afadhali upande huu wa ardhi maana ilikuwa majanga, nina malalamiko yangu najua huku hata kama si wewe binafsi unapita basi vijana wako watapita na kukupatia ujumbe.

Nimehangaika kupima viwanja vyangu kwa miaka miwili na nusu sasa nilianza kabla ya huu utaratibu wa kutumia kampuni binafsi haujashika kasi, kwa miaka miwili nimekuwa mtu wa kuzunguka kuanzia ofisi za manispaa ya kinondoni mpaka finally mwezi January hati zikawa tayari zimeandaliwa imebaki kusainiwa tu,

Tatizo limekuja hapo kwenye kusainiwa ni mwezi wa pili sasa nasubiri saini ya kamishna wa ardhi ili niweze kupata hati zangu maana ni zaidi ya moja,kiukweli naona hili zoezi lina kila dalili ya kuchukua si chini ya miezi sita kitu ambacho ni ajabu sana maana najiuliza hivi kweli hata kama kamishna yuko busy vipi kusaini na ana kazi nyingi kiasi gani hivi kweli inaweza chukua zaidi ya miezi miwili kusaini hati?

Wewe mwenyewe waziri umekuwa ukionekana kwenye vyombo mbalimbali vya habari ukieleza kwamba utaratibu wa sasa hati ikishakuwa tayari haichukui zaidi ya mwezi kuipata napenda kukuambia hili jambo si kweli na kama ndio dhamira yako basi wasaidizi wako wanakuangusha hati zangu ni za manispaa ya Kinondoni.

Mara ya mwisho nimekwenda pale nimepangiwa kwenda baada ya wiki mbili yaani mwisho wa mwezi huu wa tatu ambapo nitakuwa na miezi miwili na nusu nasubiri hati isainiwe,hii inakatisha tamaa sana muheshimiwa kama nimehangaika miaka miwili na nusu nashuhulikia hati,hati imekamilika nayo ichukue miezi sita kusainiwa kweli mnapaswa kujipanga kwa upya si kwa utaratibu huu,na mimi nakushauri ili kupima utendaji kazi wa mtu kila mtu apimwe kwa utoaji mafaili mezani kwake akiwa chini ya kiwango basi nafasi hiyo apewe mtu mwingine.

Ni hayo tu muheshimiwa waziri ila naomba kitengo hiki cha hati kiangaliwe kwa jicho la tofauti watu wanajenga mazingira ya rushwa kwa makusudi japo hawasemi lakini mtu anakuambia njoo uangalie baada ya wiki mbili ukija hakupi sababu wala taarifa faili limefikia wapi anakuambi njoo baada ya wiki mbili tena namna hii ukiwa mwepesi au hutaki usumbufu huu ni rahisi sana kushawishika kutoa rushwa ili mambo yako yashuhulikiwe haraka. Natumaini hili litashuhulikiwa kwa namna ifaayo.

Sina mawasiliano ya senior personel yoyote pale wizarani ambaye ningeweza kufikisha ujumbe huu ndo maana nimeandika huku kwa wenye mawasiliano yako watakufikishia ujumbe, pale wizarani napendekeza badala ya maboksi ya maoni wekeni namba ya mtu anayeweza kupokea malalamiko ya wananchi tena iwe waziwazi kila mtu aione ili tuwe tunatoa mrejesho wa huduma inayotolewa pale kama ni mbaya au nzuri.
 
Muheshimiwa William Lukuvi kwanza nikupongeze kwa jitihada zako katika wizara ya Ardhi, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni umejitahidi kwa kadiri unavyoweza na angalau sasa kuna afadhali upande huu wa ardhi maana ilikuwa majanga, nina malalamiko yangu najua huku hata kama si wewe binafsi unapita basi vijana wako watapita na kukupatia ujumbe.

Nimehangaika kupima viwanja vyangu kwa miaka miwili na nusu sasa nilianza kabla ya huu utaratibu wa kutumia kampuni binafsi haujashika kasi, kwa miaka miwili nimekuwa mtu wa kuzunguka kuanzia ofisi za manispaa ya kinondoni mpaka finally mwezi January hati zikawa tayari zimeandaliwa imebaki kusainiwa tu,

Tatizo limekuja hapo kwenye kusainiwa ni mwezi wa pili sasa nasubiri saini ya kamishna wa ardhi ili niweze kupata hati zangu maana ni zaidi ya moja,kiukweli naona hili zoezi lina kila dalili ya kuchukua si chini ya miezi sita kitu ambacho ni ajabu sana maana najiuliza hivi kweli hata kama kamishna yuko busy vipi kusaini na ana kazi nyingi kiasi gani hivi kweli inaweza chukua zaidi ya miezi miwili kusaini hati?

Wewe mwenyewe waziri umekuwa ukionekana kwenye vyombo mbalimbali vya habari ukieleza kwamba utaratibu wa sasa hati ikishakuwa tayari haichukui zaidi ya mwezi kuipata napenda kukuambia hili jambo si kweli na kama ndio dhamira yako basi wasaidizi wako wanakuangusha hati zangu ni za manispaa ya Kinondoni.

Mara ya mwisho nimekwenda pale nimepangiwa kwenda baada ya wiki mbili yaani mwisho wa mwezi huu wa tatu ambapo nitakuwa na miezi miwili na nusu nasubiri hati isainiwe,hii inakatisha tamaa sana muheshimiwa kama nimehangaika miaka miwili na nusu nashuhulikia hati,hati imekamilika nayo ichukue miezi sita kusainiwa kweli mnapaswa kujipanga kwa upya si kwa utaratibu huu,na mimi nakushauri ili kupima utendaji kazi wa mtu kila mtu apimwe kwa utoaji mafaili mezani kwake akiwa chini ya kiwango basi nafasi hiyo apewe mtu mwingine.

Ni hayo tu muheshimiwa waziri ila naomba kitengo hiki cha hati kiangaliwe kwa jicho la tofauti watu wanajenga mazingira ya rushwa kwa makusudi japo hawasemi lakini mtu anakuambia njoo uangalie baada ya wiki mbili ukija hakupi sababu wala taarifa faili limefikia wapi anakuambi njoo baada ya wiki mbili tena namna hii ukiwa mwepesi au hutaki usumbufu huu ni rahisi sana kushawishika kutoa rushwa ili mambo yako yashuhulikiwe haraka. Natumaini hili litashuhulikiwa kwa namna ifaayo.

Sina mawasiliano ya senior personel yoyote pale wizarani ambaye ningeweza kufikisha ujumbe huu ndo maana nimeandika huku kwa wenye mawasiliano yako watakufikishia ujumbe, pale wizarani napendekeza badala ya maboksi ya maoni wekeni namba ya mtu anayeweza kupokea malalamiko ya wananchi tena iwe waziwazi kila mtu aione ili tuwe tunatoa mrejesho wa huduma inayotolewa pale kama ni mbaya au nzuri.
Pole kaka
Rushwa imepanda bei
Hawataki kukuambia ukweli.

Ila huyo Uliyemtafuta akiupata ujumbe atakuokoa
Kwakweli wizara ya ardhi wafanyakazi wake wengi ni mawakala wa rushwa tena mawakala wa kuzimu...

Hii wizara...Ina malakika 1 kwa sasa Mh.Lukuvi
Huyu Baba
Kweli ni mtimishi wa Mungu kwenye nafasi hiyo.
Yani hata akiongea unamuona kamaanisha.

Mh.Lukuvi....Msaidie ndugu yetu huyo
 
Pole kaka
Rushwa imepanda bei
Hawataki kukuambia ukweli.

Ila huyo Uliyemtafuta akiupata ujumbe atakuokoa
Kwakweli wizara ya ardhi wafanyakazi wake wengi ni mawakala wa rushwa tena mawakala wa kuzimu...

Hii wizara...Ina malakika 1 kwa sasa Mh.Lukuvi
Huyu Baba
Kweli ni mtimishi wa Mungu kwenye nafasi hiyo.
Yani hata akiongea unamuona kamaanisha.

Mh.Lukuvi....Msaidie ndugu yetu huyo
sidhani hata kama habari hii itamfikia; mimi lakwangu lina miaka mitatu hapo manipaa ya Bagamoyo nazungushwa na kakijana kanaita Kelvin ambako ndio kalinifanyia upimaji wa viwanja vyangu Kaole halafu kakarudi mgongoni mwangu na kuanza kupimia majirani kuingia ndani ya eneo langu ili hatimaye wizarani wakipitia wapate ukakasi na hati zisitoke; hazijatoka mpaka leo hii na hakuna maelezo mazuri zaidi ya njoo kesho njoo baada ya wiki mbili njoo baada ya mwezi
 
Hati huwa zinaingizwa kwenye mfumo,ili kubaini ucheleweshwaji:
Waombaji hati wangekuwa wanaandika majina kuona lini WAMEFUATILIA NA NAMBA YA KIWANJA,UTAJUA TU NI NANI ANACHELEWESHA.!!!
ANASAINI HATI AU ANAYEPEWA KUZIGAWA HIZO HIZO HATI KWA WATEJA.
SABABU ZINGINE ZA KUCHELEWESHA,NI PAMOJA NA WATUMISHI KUTOWAJULISHA WATEJA WAO KUWA HATI ZAO ZIPO TAYARI(Kwani wateja huwa wameandika namba za simu katika nyaraka,lakini hawapigiwi)!!
Katika mtiririko hapo juu,utagundua viongozi husika wameshindwa kuwadhibiti watumishi wa ardhi.
 
Na ikumbukwe kuwa hati zipo za watu wengi sio kwamba ni wewe peke yako mleta Mada ndo unakiwanja hadi upewe hati mapema wapo wengi walotangulia kabla yako. Kuwa mvumilivu watakupatia
 
Adumu W. Lukuvi pale Wizara ya Ardhi !
Mungu twakuomba uzidi kumlinda Lukuvi siku zote!
Ila ajitahidi kuepuka kufanya maamuzi Kwa ushawishi wa kisiasa ndivyo atakavyozidi kupata kibali machoni pa Mungu na Wanadamu!
Mungu akuongoze uamue kwa haki bila kujali itikadi n.k
 
Halafu gharama za kulipia hati Mbona ni kubwa sana jamani?!
Ada Kwa mwaka nayo bado ni kubwa sana!
 
Mimi wakati nanunua kiwanja wizara ya ardhi kulikuwa na muhuri mmoja ulikuwa haujapigwa.tangu mwezi Wa 10 mwaka jana naambiwa wakili yuko busy.muhuri uligongwa mwezi Wa 3 mwaka huu. Wapo so slow
 
Wizara ya ardhi longolongo zimepungua kwa kiasi kikubwa sana kwa sisi wa viwanja vidogodogo. Ukiambiwa urudi baada ya wiki mbili ukarudi na ukaambiwa tu urudi tena baada ya wiki mbili usinyanyuke tu na kuondoka bila kuambiwa sababu. Ni vizuri ukarekodi tarehe na jina la afisa anayekuhudumia pia maana wakati mwingine anakwambia urudi baada ya muda Fulani halafu hafuatilii. Sasa hivi ndani ya siku 60 unapata hati yako labda kutokee matatizo kuhusu hati husika. Nimehudumiwa pale mara tatu tofauti na nimeona tofauti kubwa sana. Zamani ulikuwa ukiambiwa urudi baada ya siku 90 unaamua kujikalia siku 300 na bado hupati kitu kama hujui kuongea vizuri lakini sasa hivi mambo ni mazuri kwa kweli. Kuna mabosi pale hawakai tu maofisini. Wakikuta wateja ni wengi wanajaribu kutafuta jinsi ya kuharakisha. Kuna wakati nilifikiri kwamba naota siko Tanzania.

Kimbembe kimebaki kwenye halmashauri. Unatumwa ukanunue faili la 500!, kila ukienda mara faili sijui limepanda wapi likashuka wapi, halionekani tufungue jipya..... Ili faili lisogee unatakiwa uwepo ufatane mguu kwa mguu na mhudumu na uwe na afisa masijala mmoja anayeshughulikia faili lako. Ukisema ufanye shughuli zako kwa imani kuwa nao watafanya za kwao utashangaa. Tunapoteza muda mwingi sana kufatilia maswala ya ardhi huko halmashauri. Ni imani yangu serikali itasambaza teknolojia na mikakati ya kuboresha huduma kwenye halmashauri zake. Ukifatilia hati halmashauri kwa miaka mitatu ni lazima uone siku 60 wizarani ni nyingi lakini si nyingi. Kuwa na subira na ondoa wazo la kutakiwa rushwa.
 
Halmashauri ni shida sana!
Hivi faili linawezaje kupotea Ofisini ?!
Yani bado sana huduma Kwa wananchi siyo ya kuridhisha hata kidogo!
 
Back
Top Bottom