Waziri Lugola: Aliyekuwa Mkurugenzi NIDA, Dickson Maimu na Jack Gotham wasipoitikia wito ‘watapata tabu sana’

Swali hapa ..... ni kwa nini atutangazie kwenye vyombo vya habari kuwa fulani na fulani ni lazima wafike ofisini kwake siku fulani. La sivyo watapata tabu sana.

Wewe huoni kuwa anawadhalilisha hao watu ....!!
Ah! Mkuu sazingine vitisho vinajenga nidhamu buana!
Ungekuwepo miaka ya 80' enzi za Lyatonga Mrema akiwa na wadhifa huohuo alionao Lugola leo, unakumbuka alivyonasa madhahabu pale air port, unakumbuka alivyokuwa akiwaita na kuwapangia matajiri na wahujumu uchumi kwenda kuripoti kwake kwa muda alioutaka yeye na walitii?
Nyani ukiwachekea utaambulia mabua.
Hii nchi ilikuwa imefikia pabaya
Acha kuwatisha tu, awasweke ndani na kuwafungulia mashitaka wakajibu tuhuma zao mahakamani huko wasipotekeleza maagizo yake.
 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ameipa wiki mbili kampuni ya Kimataifa ya Iris Corporation Berhard impe majibu ya kuwa italeta mtambo wa kutengeneza kadi ghafi au Dola za Marekani Milioni 14 sawa na zaidi ya shilingi bilioni 32 za Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano wa Wizara, Dodoma leo,baada ya kikao na Menejimenti ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)na viongozi wa Kampuni hiyo, Waziri Lugola alisema kampuni hiyo haiwezi ikacheza na fedha za Watanzania na walipa kodi.

Lugola aliongeza kuwa lazima fedha hizo au mtambo huo upatikane kwa kuwa Serikali ya Awamu ya Tano haitakubaliana na mchezo mchafu wa aina yoyote, na pia yeye kama Waziri wa Wizara hiyo anaendelea kutekeleza maagizo ya Rais Dkt John Magufuli. “Tumezungumza nao na tumekubaliana

Aidha, Waziri Lugola amewataka wamiliki wa kampuni zilizolipwa kifisadi fedha za Mradi wa mtambo wa NIDA kujisalimisha jijini Dodoma Agosti 3 mwaka huu wakiwa na mtambo huo vinginevyo warejeshe fedha zilizotumika.

Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amesisitiza kuwa kutokana na wito alioutoa kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa NIDA, Dickson Maimu pamoja na Jack Gotham kufika ofisini kwake, wasifanye jaribio la kutokuitikia wito huo, kwani wakifanya hivyo watapata tabu sana.

hivi hawa kwa nini wanaogopa kumjibu Lugola ki-Trump-Trump??

"WE WE WE!! USITHUBUTU KURUDIA KUTUTISHA. UKIRUDIA TU, YATAKAYOKUSIBU NI WACHACHE SANA DUNIA HII YAMEWAHI KUWAPATA. SISI SI WATU WA MCHEZO MCHEZO BANA - HATUOGOPI VITISHO VYAKO WALA UBABE WAKO WALA KIFO. JIHADHARI SANA KIJANA!"
 
Acha hai wakina Gotham waitwe tu...mbona kipindi cha nyuma humu Jf kulikuwa na nyuzi nyingi zikiwashuku kwa kufanya madudu

Ova
 
Ah! Mkuu sazingine vitisho vinajenga nidhamu buana!
Ungekuwepo miaka ya 80' enzi za Lyatonga Mrema akiwa na wadhifa huohuo alionao Lugola leo, unakumbuka alivyonasa madhahabu pale air port, unakumbuka alivyokuwa akiwaita na kuwapangia matajiri na wahujumu uchumi kwenda kuripoti kwake kwa muda alioutaka yeye na walitii?
Nyani ukiwachekea utaambulia mabua.
Hii nchi ilikuwa imefikia pabaya
Acha kuwatisha tu, awasweke ndani na kuwafungulia mashitaka wakajibu tuhuma zao mahakamani huko wasipotekeleza maagizo yake.
Inaelekea huamini katika utawala wa sheria.
 
Kangi lugola ,ataweza huu mfupa ?

Huyu Jack Gotham , mfadhili na mmoja wa wana mikakati wa Bernard membe , aliyepewa tenda hiyo ili wapige pesa za kampeni 2015, huku huyu Dickson Maimu akiwekwa pale kukamilisha dili, bila kujua mlokole wa kitengo alikuwa pale ,akiwasoma na kuwa study vilivyo ,alivyomaliza kazi yake kwa ustadi , akapewa U DG , hakika kikwete na udhaifu wake kuna mambo alistahili pongezi kwa kiasi maana alikuwa na uzalendo nusu ubandidu nusu


Je kangi ataweza huu mfupa wenye chain ndefu ?

Yetu Macho na masikio

Sasa kama kila kundi la Chama huweka mikakati ya namna hii ili kujinyakulia madaraka nchi itaendeleaje?
 
Mdogo mdogo tu ipo siku na aliyeuza nyumba za umma atatakiwa kuripoti makao makuu ya sungusungu.
"atapata tabu sana"!
Acha ushabiki wa kijinga Wewe..serikali IPO madarakani kusimamia Mali na fedha kwa niaba ya wananchi Mimi sina mlengo wa kichama ila kwa hili ninampongeza kangi
 
K
Lugola naye kazidi kwa matamko yake sasa. Kila siku anakuja na mpya. Ya awali ameshayatekeleza?

Hana tofauti na Aggrey Mwanri RC wa Tabora ambaye akifika site hufoka mno lakini utekelezaji zero.

Lugola mpaka sasa amerukia rukia mambo mengi lakini sioni anachofanikiwa zaidi ya kutoa masaa kadhaa lakini baada ya hapo hurukia mengine.
Kwa waziri anapoagiza hasa wa ulinzi lazima wayekeleze mfano..mbwa tiyari kashapatikana,arusha RPC ametekeleza maagizo yote ya waziri mpaka Jana, Etc. Tuache ushabiki
 
Kwakukusaidia ni kwamba mwenye dhamana ya usemaji wa mwisho kuhusu mambo yote yahusiyo wizara ni waziri husika hawa wengne kama watu wa PR. Ni watu ambao hutumika pale mwenye ofusu anapowapangia utaratibu na kuainisha mipaka yao.. inawezekana mwenye ofisi yake ameamua kuwa msemaji wa wizara yake which is fine.. And kumbuka maagizo yote ya kangi lugola ameyatatoa akiwa sight au ziarani sio akiwa na press conference..ni maagizo ya ghafla ambayi hayahusiani ni PR...QUOTE="Mkara-tu, post: 27720201, member: 482919"]Huyu mtu labda anatekeleza aliyotumwa na boss wake (which is fine), lakini hili la ku-summon suspects kila siku kupitia media linakera. Kama kuna ushahidi wa kutosha wa kosa la jinai mbona mahakama ya ufisadi ipo kwa ajili hiyo! By the way, hivi wizara ya mambo ya ndani haina public relations officer? Too much of media stunts, seriously.[/QUOTE]
Kwa
 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ameipa wiki mbili kampuni ya Kimataifa ya Iris Corporation Berhard impe majibu ya kuwa italeta mtambo wa kutengeneza kadi ghafi au Dola za Marekani Milioni 14 sawa na zaidi ya shilingi bilioni 32 za Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano wa Wizara, Dodoma leo,baada ya kikao na Menejimenti ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)na viongozi wa Kampuni hiyo, Waziri Lugola alisema kampuni hiyo haiwezi ikacheza na fedha za Watanzania na walipa kodi.

Lugola aliongeza kuwa lazima fedha hizo au mtambo huo upatikane kwa kuwa Serikali ya Awamu ya Tano haitakubaliana na mchezo mchafu wa aina yoyote, na pia yeye kama Waziri wa Wizara hiyo anaendelea kutekeleza maagizo ya Rais Dkt John Magufuli. “Tumezungumza nao na tumekubaliana

Aidha, Waziri Lugola amewataka wamiliki wa kampuni zilizolipwa kifisadi fedha za Mradi wa mtambo wa NIDA kujisalimisha jijini Dodoma Agosti 3 mwaka huu wakiwa na mtambo huo vinginevyo warejeshe fedha zilizotumika.

Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amesisitiza kuwa kutokana na wito alioutoa kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa NIDA, Dickson Maimu pamoja na Jack Gotham kufika ofisini kwake, wasifanye jaribio la kutokuitikia wito huo, kwani wakifanya hivyo watapata tabu sana.

Sawa tunasubili utekelezaji waziri
 
Anaingilia kazi za wengine kwa hawa wapelekwe kwenye vyombo vinavyo husika watoe maelezo na sio kumwona yeye huyu Alikuwa alikuwa na kesi ya rushwa
 
Waziri akiwa kizimbani
 

Attachments

  • IMG-20180726-WA0009.jpg
    IMG-20180726-WA0009.jpg
    74.6 KB · Views: 38
Back
Top Bottom