Waziri kapuya ndani ya pekecha pekecha kujiandaa na mgomo wa tucta

sijafulia

Member
Mar 26, 2010
86
2

Katika hali isiyo ya kawaida kwa viongozi wa juu nchini kuonekana katika kumbi za starehe tena katika sare sambamba na waimbaji wa bendi, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya aliingia ukumbini na kuyarudi mapigo ya pekecha pekecha ya wana wa Akudo.Huku akiwa amevalia sare sawa na waimbaji wa bendi ya Akudo, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya alijitosa ukumbini na kuanza kuyarudi mapigo ya pekecha pekecha ya bendi ya Akudo Impact iliyokuwa ikitoa burudani kwenye ukumbi wa Msasani Beach.

Kapuya ambaye ndiye mmliki wa bendi hiyo alijimwaga stejini na kusakata muziki kwa nguvu zote huku jasho likimtoka akiwa pamoja na mpambe wake ambaye jina lake halikufahamika.

Kapuya anakuwa kiongozi wa pili wa juu serikalini kumiliki bendi wa kwanza alikuwa Waziri Mdhihiri Mdhihiri ambaye aliwahi kumiliki bendi ya Mchinga Sound ambayo baadaye ilivunjika.

Kutokana na jinsi anavyoithamini bendi yake, waziri Kapuya amefanikiwa kuifanya bendi ya Akudo iwe miongoni mwa bendi zinazopendwa sana nchini kiasi cha kuleta ushindani mkubwa katika medani ya muziki wa dansi hapa nchini.

WAZIRI KAPUYA AKIJIANDA NA MAZOEZI YA MGOMO WA TUCTA HAPA AKIWA KWENYE ""PEKECHA PEKECHA"""AKUDO ...KAMA UNA MUDA KARIBU UMWONE WAZIRI WETU AKIFURAHIA MAISHA.NI MMOJA WA MAWAZIRI ANAEMILIKI BENDI ..MWINGINE ALIKUWA MH MUDHIHIRI MUDHIRI!!!

SRCE NIFAHAMISHE DOTI COMU
 

Attachments

  • KP 1.jpg
    KP 1.jpg
    13.7 KB · Views: 105
Katika hali isiyo ya kawaida kwa viongozi wa juu nchini kuonekana katika kumbi za starehe tena katika sare sambamba na waimbaji wa bendi, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya aliingia ukumbini na kuyarudi mapigo ya pekecha pekecha ya wana wa Akudo.Huku akiwa amevalia sare sawa na waimbaji wa bendi ya Akudo, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya alijitosa ukumbini na kuanza kuyarudi mapigo ya pekecha pekecha ya bendi ya Akudo Impact iliyokuwa ikitoa burudani kwenye ukumbi wa Msasani Beach.

Kapuya ambaye ndiye mmliki wa bendi hiyo alijimwaga stejini na kusakata muziki kwa nguvu zote huku jasho likimtoka akiwa pamoja na mpambe wake ambaye jina lake halikufahamika.

Kapuya anakuwa kiongozi wa pili wa juu serikalini kumiliki bendi wa kwanza alikuwa Waziri Mdhihiri Mdhihiri ambaye aliwahi kumiliki bendi ya Mchinga Sound ambayo baadaye ilivunjika.

Kutokana na jinsi anavyoithamini bendi yake, waziri Kapuya amefanikiwa kuifanya bendi ya Akudo iwe miongoni mwa bendi zinazopendwa sana nchini kiasi cha kuleta ushindani mkubwa katika medani ya muziki wa dansi hapa nchini.

WAZIRI KAPUYA AKIJIANDA NA MAZOEZI YA MGOMO WA TUCTA HAPA AKIWA KWENYE ""PEKECHA PEKECHA"""AKUDO ...KAMA UNA MUDA KARIBU UMWONE WAZIRI WETU AKIFURAHIA MAISHA.NI MMOJA WA MAWAZIRI ANAEMILIKI BENDI ..MWINGINE ALIKUWA MH MUDHIHIRI MUDHIRI!!!

SRCE NIFAHAMISHE DOTI COMU
mkuu hii kitu ipo hapa jamvini tayari mkuu,mods unganisheni hizi mada
 
Hili ni dogo.
Ukitaka kumfahamu Kapuya, Uliza waliokuwa naye pale UDSM. Utasikia uchafu wa mkuu huyu kiasi cha kutia wasiwasi ya uzima wa akili yake.

BTW, jamaa huyu nilisikia siyo m-TZ. ana asili ya nchi ya Burundi na hakuwahi kuingia uraia rasmi. Ndivyo nilivyowahi sikia.
 
Back
Top Bottom