Na Mwandishi wetu - Zanzibar
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe Dkt Faustine Ndugulile aipongeza Shirika la Mawasiliano Tanzania kwa kuboresha muonekano wa Vituo vya Huduma kwa Wateja nchi nzima ili kuongeza mvuto kwa wateja wa huduma za mawasiliano.
Amesema hayo katika hafla ya uzinduzi wa Kituo cha Huduma kwa Wateja uliofanyika katika ofisi za Shirika hilo zilizoko Kijangwani katika Mkoa wa Mjini Magharib- Unguja Zanzibar.
“Nawapongeza TTCL Corporation kwa ukarabati mkubwa mliofanya katika kuleta muonekano mpya wa ofisi yenu hii, mmeboresha mazingira ya utoaji huduma na ninaamini Kituo hiki kitaleta mvuto kwa wateja wetu kuja kupata huduma” amesema Dkt. Faustine Ndugulile (Mb).
Waziri aliongeza kuwa pamoja na muonekano mpya huo ambao utasaidia kuleta mvuto wa kibiashara kwa wateja wa bidhaa na huduma za shirika hilo amewapa rai watumishi na watoa huduma wa TTCL kuendelea kuboresha huduma na utoaji wa huduma hizo ili kuifanya Kauli Mbiu ya Shirika hilo ya Rudi Nyumbani Kumenoga kuwa na uhalisia.
Aliongeza kuwa Wafanyakazi wa Shirika la Mawasiliano Tanzania wanapaswa kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wateja wao huku wakizingatia uzalendo, weledi, kasi na kutafuta masoko badala ya kusuburia wateja ofisini.
Naye, Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe, Rahma Kassimu alisema Wizara yake itaendelea kufanya kazi kwa ukaribu na TTCL ili kuhakikisha huduma bora za mawasiliano kwa wateja zinatolewa kwa wananchi wa Zanzibar.
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe Dkt Faustine Ndugulile aipongeza Shirika la Mawasiliano Tanzania kwa kuboresha muonekano wa Vituo vya Huduma kwa Wateja nchi nzima ili kuongeza mvuto kwa wateja wa huduma za mawasiliano.
Amesema hayo katika hafla ya uzinduzi wa Kituo cha Huduma kwa Wateja uliofanyika katika ofisi za Shirika hilo zilizoko Kijangwani katika Mkoa wa Mjini Magharib- Unguja Zanzibar.
“Nawapongeza TTCL Corporation kwa ukarabati mkubwa mliofanya katika kuleta muonekano mpya wa ofisi yenu hii, mmeboresha mazingira ya utoaji huduma na ninaamini Kituo hiki kitaleta mvuto kwa wateja wetu kuja kupata huduma” amesema Dkt. Faustine Ndugulile (Mb).
Waziri aliongeza kuwa pamoja na muonekano mpya huo ambao utasaidia kuleta mvuto wa kibiashara kwa wateja wa bidhaa na huduma za shirika hilo amewapa rai watumishi na watoa huduma wa TTCL kuendelea kuboresha huduma na utoaji wa huduma hizo ili kuifanya Kauli Mbiu ya Shirika hilo ya Rudi Nyumbani Kumenoga kuwa na uhalisia.
Aliongeza kuwa Wafanyakazi wa Shirika la Mawasiliano Tanzania wanapaswa kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wateja wao huku wakizingatia uzalendo, weledi, kasi na kutafuta masoko badala ya kusuburia wateja ofisini.
Naye, Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe, Rahma Kassimu alisema Wizara yake itaendelea kufanya kazi kwa ukaribu na TTCL ili kuhakikisha huduma bora za mawasiliano kwa wateja zinatolewa kwa wananchi wa Zanzibar.