Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,903
- 945
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo kuhusu kuendeleza ushirikiano wa kibiashara baina ya Tanzania na Indonesia na Balozi wa Indonesia nchini Mhe. Tri Yogo Jatmiko Septemba 9, 2023 katika Ofisi ndogo za Wizara, jijini Dar es Salaam..
Waziri Kijaji amemhakikishia Balozi huyo kuwa Tanzania iko tayali kuendeleza ushirikiani baina ya nchi hizo na iko tayari kuwezesha miradi ya uwekezaji hususani katika sekta ya kilimo hasa katika uongezaji wa mnyororo wa thamani katika mazao ambayo nchi hiyo imepanga kuyaendeleza kama vile karafuu ili kuongeza ajira na kipato kwa wanzania.
Aidha, Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb.) amekutana na kuzungumza kuhusu kuendeleza ushirikiano wa kibiashara baina ya Tanzania na Uturuki na Balozi wa Uturuki nchini Mhe. Dkt. Mehmet Güllüoğlu 11/09/ 2023 katika Ofisi ndogo za Wizara, jijini Dar es Salaam
Vilevile, Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb.) amekutana na kuzungumza kuhusu kuendeleza uhusiano wa kibiashara na China hususan uchakataji wa mazao ya kilimo na Balozi wa China nchini, Mhe. Chen Mingjian katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam 11/09/2023.
Waziri Kijaji amemhakikishia Balozi huyo kuwa Tanzania iko tayali kuendeleza ushirikiani baina ya nchi hizo na iko tayari kuwezesha miradi ya uwekezaji hususani katika sekta ya kilimo hasa katika uongezaji wa mnyororo wa thamani katika mazao ambayo nchi hiyo imepanga kuyaendeleza kama vile karafuu ili kuongeza ajira na kipato kwa wanzania.
Aidha, Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb.) amekutana na kuzungumza kuhusu kuendeleza ushirikiano wa kibiashara baina ya Tanzania na Uturuki na Balozi wa Uturuki nchini Mhe. Dkt. Mehmet Güllüoğlu 11/09/ 2023 katika Ofisi ndogo za Wizara, jijini Dar es Salaam
Vilevile, Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb.) amekutana na kuzungumza kuhusu kuendeleza uhusiano wa kibiashara na China hususan uchakataji wa mazao ya kilimo na Balozi wa China nchini, Mhe. Chen Mingjian katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam 11/09/2023.