Waziri anapolima na suti

Waziri anapolima na suti

Pinda ana unafki kutoka moyoni, namshangaa kila anapo jiliza bungeni kumbe hakuna kitu!
 
hapo analima nini sasa........nadhani alikuwa anamalizia kale kakipande kake ka muvi ya mtoto wa mkulima tu
halafu ajabu yenyewe, eti anafundisha jinsi ya kupalilia katika shamba ambalo linaonekana limeshapaliliwa tayari.
 
Jambo lingine tena limekaa ovyo! WAZIRI MKUU yuko mbele ya mwanamama amebeba mtoto mgongoni na yuko peku, eti waziri Mkuu anamwelekeza namna ya kupalilia? Hii imekaa ovyo!
 
alienda kulima au kutembea?

Sijamsikia mda mrefu kumbe yupo nyumbani ndio maana

Huyu mheshimiwa anajulikana kwa jina la "mtoto wa mkulima".
Hata MMJ anaelewa hilo.

Pinda anaweza kulima akiwa kavaa suti, au hata akiwa amevalia fulana na kofia za CCM. Kulima iko ndani ya damu yake..."mtoto wa mkulima"

Kuna member amemsifia Pinda,mtoto wa mkulima kuwa ni zaidi ya Cleopa Msuya. link https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/369511-pinda-ni-zaidi-ya-cleopa-david-msuya.html
 
Pinda ni muongo muongo sana...yaaani amfundishe nani kupalilia mahindi kama sio sanaaa hizi
 
Hawajamaa ni wasanii sanaa,sasa pinda ile dhana ya mtoto wa mkulima imekuwa mtoto wa msanii,analima na suti, anapalilia mahindi yanyewf hayana hatamagugu yaani full sanaa, ukilinganisha na mwl Nyerere akhwa shamba!
 
securedownload.jpeg
securedownload-2.jpeg
securedownload-1.jpeg

Sijui nianze kulia au nisubiri kidogo..... !!!!!!!!!!!!!!
 
He! Anapalilia nini pale mbona pameshapaliliwa? "Demo" inatolewa live. Angefanya "demo" mahali ambapo pana majani lukuki!! Kwa mavazi sina comment maana kaamua mwenyewe kwenda shambani na suti. Mi naona huo ni uamuzi wake.
[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD="align: center"] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption, align: center"]Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh, Mizengo Pinda akiwaelekeza Wakulima wa Mahindi namna ya Kupalilia zao hilo. Mheshimiwa alikuwa shambani hapo akiwa amevalia vazi la Suti Wakati alipotembelea shamba la Mkuu wa Mkoa wa Katavi Desemba 18, 2012 eneo la Tenki fupi kata ya Nsimbo, wilayani Mlele, Katavi. Bi. Kipande ni mfanyakazi katika shamba hilo. (Picha na Irene Bwire wa OWM).

source maasinda
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Jamani mwacheni mtoto wa mkulima, aonyeshe mavituz yake kwa wakulima wa Mahindi, Daily anasema yeye ni mtoto wa mkulima, hivi ndio vitendo sasa, tuone.
 
Off point!

Wewe ndio katika wale wanaosoma vichwa vya habari vya kuchakachuwa (kiwanda cha uongo) vya JF na kuwacha kusoma utumbo wa habari na kuuelewa ukweli, soma hii:

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh, Mizengo Pinda akiwaelekeza Wakulima wa Mahindi namna ya Kupalilia zao hilo. Mheshimiwa alikuwa shambani hapo akiwa amevalia vazi la Suti Wakati alipotembelea shamba la Mkuu wa Mkoa wa Katavi Desemba 18, 2012 eneo la Tenki fupi kata ya Nsimbo, wilayani Mlele, Katavi. Bi. Kipande ni mfanyakazi katika shamba hilo. (Picha na Irene Bwire wa OWM).

Hapo mizengo pinda anaonesha kuwa kilimo cha mahindi anakijuwa na wala suti za ofisini si kikwazo cha kuweza kumuelekeza mtu kivitendo. Kuweni makini.
 
hivi pinda ni waziri mkuu wa tanzania au wa rukwa na katavi tu? mwezi mmoja hauwezi pita bila yeye kutembelea mikoa hiyo. binafsi sijawahi kusikia ametembelea lindi au mtwara

Mimi nimeshamsikia akitembelea Lindi na Mtwara...
 
Back
Top Bottom