Mkuu LG,
Huitaji utabiri wa wazee wa CCM kujua CCM inaelekea wapi akili za kawaida kabisa zinatosha kubaiani chama kikongwe bara Afrika kina karibia kujizika chenyewe kama kambare anapobaiani msimu wa kiangazi umekaribia.
Ukitazama kampeni za CCM kuanzia Igunga na Arumeru unabaini jambo moja muhimu sana CCM imeacha misingi mikuu ya kuanzishwa kwake [Chama cha wakulima na wafanyakazi] CCM imegeuka kimekuwa chama cha matajiri na wezi wa rasilimali za taifa.CCM imeacha msingi wake mkuu wa kuwatetea wanyonge,imeacha kulinda rasilimali za taifa,inakumbatia wezi,sera zake hazitekelezwi,rushwa inapingwa majukwaani lakini nyuma ya pazia inapaliliwa,inawekewa mbolea na kuvunwa kwa ustadi mkubwa.
Kwakuwa CCM haina sera na hili limejitokeza katika chaguzi za Igunga Hijjab ikachukua nafasi kubwa badala ya kuufahamisha umma wa Igunga nchi inakwenda wapi,mafanikio yaliyofikiwa na changamoto zake,Arumeru CCM imekujua na sera za washili hawamtaki mgombea wa chama cha upinzani hawana kitu cha kuwaambia wapiga kura wa Arumeru wanaokabiliwa na uhaba mkubwa wa ardhi kwakuwa wanajua wanahusika kwa asilimia zote kuiuza ardhi kwa wawekezaji uchwara na kuwaacha wananchi bila ardhi.
Hii si ile CCM ya Nyerere iliyokuwa ikiwasemea wanyonge,wakulima na wafanyakazi hii ni CCM ya Kikwete,Mkapa na Mwinyi inawasemea wawekezaji wanaopora madini yetu,wanaopora ardhi yetu,wanaopora ajira zetu.CCM ya leo inazalisha ajira kwa kuongeza idadi ya mikoa na wilaya haina habari na viwanda !.Hii ni CCM ya washili na Hijabu,hii ni CCM ya Wasira na genge la wahuni hawana uchungu na umasikini wa watanzania,hawawezi kutueleza baada ya miaka 50 ya uhuru wamefanikiwa kupunguza umasikini vijijini kwa asilimia ngapi !.Rwanda ya Kagame baada ya mapigano ya muda mrefu inapiga hatua kubwa utashangaa haina rasilimali nyingi ukilingalisha na Tanzania.