Wazee wa kujilipua kimaisha (risk takers) kwa style tofauti tukutane hapa!

Wiki majuzi nakatiza zangu mitaa ya Salt River Cape Town Nakutana na madogo wawili wa kibongo wanataka kunitapeli na biashara yao ya Almasi feki...Nikatabasamu kimoyomoyo nikawaambia kuna ndugu yangu mmbongo anaishi mitaa ya Roodebloem Road karibu na WALMER ESTATE (Ninapojisitiri na Familia Yangu)... twendeni mnaweza kufanya nae biashara bcoz mimi bado foreigner hapa Cape Town(NIKAWADANGANYA) .....Wakaunga tela nikampigia simu wife apike ugali mkubwa sana na Tuna Fish (Jodari)..Tukafika chakula kikaiva tukala wakashiba nikawachana hiyo biashara wanayotaka kunitapeli Mimi Baba wawili nilishaifanyaga hapa hapa miaka 16 iliyopita...jasho likaanza kuwatoka,.
Nikawapa option mbili za mimi kuwasaidia mmoja naona anaonyesha ushirikiano mwenzake ametokomea nahisi atakua karudi Juhannesburg...To make the long story short kwa sasa ni Risk sana kuja kutapeli almasi feki Cape Town ila madogo wa kibongo wamethubutu (RISK TAKERS)
 
This is my story

Niko kidato cha tatu macho yananisumbua yakisababisha kichwa kuuma sana! Mara nashindwa kuwa attention katika vipindi darasan nikirudi nyumbani kujisomea tatizo kichwa kinauma mbaya kabixa perfomance inashuka xana,dharau kwa wanafunzi wenzangu mpaka dingi nyumbani naiona mama tu ndio kimbilio langu, form three inakwisha nakwenda hospital napata miwani ya macho mwaka wa mwisho form four nasoma xana kama sina akili vizuri mtaani sionekani full kujifungia ndani miezi mitatu siendi shule napiga masomo ya three pamoja na four kwa kuwa niliamin kama nisiposoma vizuri masomo ya three basi mimi ni failure mtarajiwa,narudi shule mwezi wa nne tukiwa kwenye mid-term test naongoza somo la physics watu wakidhani nimebahatisha ikawa hivyo mpaka mwisho namaliza,sikuwa mmoja kati ya wale waliopata division one lakin kwa sayansi nilifaulu sawa na wale wa division one roho iliniuma kwa nini sikupata one? Lakini nikapiga moyo konde,chaguzi zinakuja nimechaguliwa CBG na mimi dream nisome PCB na si kwamba labda PCB nilifeli rahasha nilikuwa na point sawa na CBG yaan point 8 CCB in phys,chem and bio moto ukawaka kichwani nikamfuata afisa elimu nikafanikiwa kupata shule moja ilikuwa inaanza tu lakin ina PCB na ni day kwa kuwa ishu ilikuwa ni kupita dream zangu kiroho nikasema nitakomaa kimbembe kinaanza niko advance nakomaa na PCB mara hee! Macho yanarudixha hali ka iliyonikumba kidato cha tatu nabadili miwani bila msaada, baba anatuma Tsh 50000/=kila mwezi mmoja ya matumizi ya chakula na mimi binafsi life limetight kombi yenyewe ishu plus kichwa kinauma ilifika wakati nikawaza nisurende tu nirudi home nitakapojiona nikofiti bhax nitardi tena school lakin nikikumbuka dhihak za baba home plux za watu nikaona nitaririka sana licha ya afya yangu mbovu nikajitahidi ivo ivo ilimradi tyu nionekane nimemaliza six, kulala njaa ilikuwa kawaida sana kwangu siku hata tano ivu,uneza kula ugari chumvi unavamia bustani ya mtu usiku wa saa tano sita unanyukua mboga life goes on Necta ya six inakuja unaangukia division three ilokosa principle pass za kukuwezesha soma degree yeyote direct mzee kapata motivation kwa majirani kakubali nitafte chuo cha diploma natumia cheti cha four napata diploma ya clinical medicine swala la afya ukimwambia haelewi daah! Nikajipa matumain nikifika chuo nikapata kadi ya bima bax atakuwa mkombozi wangu kuliko kusema nisiende chuo nikakomaa hapa mtaani kwa afya yangu sitoweza na ntakuwa nimelost vyote. Natimba chuo mara paap napata kadi ya bima naenda hospital doctor ana nambia kuna damu imeviria ndani hivyo inazuia miali ya mwanga kupenyeza kwenye jicho na kuifikia retina hii nikutokana na kumpa story kwamba wakati wa utoto nishawahi umia, ananiambia hapa hatutoweza kufanya operation ya namna hiyo hivyo utahitajika kwenda KCMC ama muhimbili wao ndio wenye huduma hiyo,nasubiri kidogo semester inakwisha ikumbukwe kuwa kwa kipindi cha semester ilikuwa kusoma kwangu magumash yaan nasoma kiasi cha kwamba nisipate less than 50 lakin hata kwa hiyo baadhi ya module unapata less, baada ya semister kuisha nakwenda KCMC nakutana na muhindi ana nambia nilipoumia nerve impulses ziliharibika hivyo hakuna uwezekano wa kulitibu jicho langu nimtafute tu mtu wa neurons anisaidie kutatua tatizo la kichwa nampata mtu wa neurons mizumgusho mingi kila siku ananipiga tarehe plus dawa ambazo sizion kunipa matumain ya kupona niko kwa kaka arusha kaoa msukuma roho mbaya usipime! Ikafikia hatua akaaniita mbwa bro nikimpima kakamatwa ile kisawasawa yaan ka kapewa dawa vile maana anamheshim hatari hataki kusikiliza chochote tusemacho sisi ndugu zake, mama dada na kaka wengine anatuona ka si ndugu zake ila huyo mwanamke na ndugu wa upande wa mwanamke. Uvimilivu unanishinda kuendelea kaa pale hata kama kweli niko kimatibabu lakin kitendo cha kuitwa mbwa roho haipendi nikakwea bus mpaka nyumbani baada ya hapo naenda hospital ya wilaya nampata jaamaa kanambia kichwa chako kinakuuma kwa kuwa macho yako yanashindwa pambana na mwanga mkali hivyo wahitaji miwani special kwa ajili ya kupambana na mwanga daa napimwa macho napewa miwani naanza kuona kichwa kina settle,mambo mengi yaliyobadilika yanaanza kurudi kwenye mstali yaani hapa uhusiano na jamiii ukaanza imarika hata katika maongezi nikaanza kujiona nakuwa vyema si kama pale nilipokuwa nikiumwa ambapo nilipenda sana kujitenga na jamii. Mara mda wa kurudi chuo unawadia nakwenda chuo, kutokana na kuto kuwa na mawasiliano na watu wa chuo kipindi nahangaika hasa baada ya kupoteza simu nardi chuo nakuta nina supplementary tatu out of eight modules ratiba kwenye ubao ya kufanya supplementary imekarbia na mm sijajiandaa kabxaa, axee nikajitahidi xana nikasoma kwa bidii zote but mtihani unakuja nimesapua mbili moja still nimekamatwa hivyo nahitajika kurudia semester nzima kwa somo moja tu la ANATOMY( Study of body structure) we nikasema usinitanie we elimu nikaacha pesa ya ada nikanunua kompyuta,printer,amplifier na spikers nikapanga chumba baada ya kamda semester imekata nardi home wao wanajua niko chuo! Mzee mwaka mwingine ananipa pesa mi naanzisha stationery na movies and music liblary hapo najua kutumia kompyuta vyema pamoja na tuhuduma twake kidogo ka kupandisha windows naandika bango kubwa PABRO ESCOBAR LIBRALY AND STATIONERY naanza ingiza pesa maisha yanasonga napata pesa kichele kwa mzee ya chakula kwa mwezi ya biashara natupia benk baada ya kumaliza chuo sirudi home kwa kisingizio cha nayaanza maisha kumbe nishaanza kitambo wanashitukia tu namiliki bussness kubwa kiwanja na matofali tayar kwa kupandisha njenge kali. Nitaoa nakuacha mtoto then nitarudi chuo nisome diploma ya electronics niachane kabixa na mambo ya kumtibu bin adam
 
Uzi umenigusa sana huu! Nilikuwa mzuri class ila nilipofika chuo mambo yakawa magumu nikafeli, sikukata tamaa washkaji kwa mbaali mawasiliano yakapungua nikawaachia wasomi wenyewe wasome mi nikaingia kitaa kubangaiza nilikuwa nilifanya kazi ngumu balaa nalipwa buku 3 nauli, msosi imeisha mara nikahama nikaajiriwa sehemu mshahara kidunyuu, sikukata tamaa sasa hivi sio yule tena wasomi wangu wale kama nawaona vileee! Nimegundua kubadili Elimu kuwa pesa hapa Bongo lazima U-risk.
 
Uzi umenigusa sana huu! Nilikuwa mzuri class ila nilipofika chuo mambo yakawa magumu nikafeli, sikukata tamaa washkaji kwa mbaali mawasiliano yakapungua nikawaachia wasomi wenyewe wasome mi nikaingia kitaa kubangaiza nilikuwa nilifanya kazi ngumu balaa nalipwa buku 3 nauli, msosi imeisha mara nikahama nikaajiriwa sehemu mshahara kidunyuu, sikukata tamaa sasa hivi sio yule tena wasomi wangu wale kama nawaona vileee! Nimegundua kubadili Elimu kuwa pesa hapa Bongo lazima U-risk.
Tatizo la wasomi wa kibongo wamejaa pride, kujishusha kwao mwiko.
 
Yap uzi murua kabisa huu, unatakiwa uishi siku zote mpaka kiama ,maana wengi wetu tuliotoka kwenye familia za kubangaiza tumepitia mengi magumu,na hatukuwahi kulaumu,kumlaumu mtu tulipambana na hali zetu kibabe
 
Uzi umenigusa sana huu! Nilikuwa mzuri class ila nilipofika chuo mambo yakawa magumu nikafeli, sikukata tamaa washkaji kwa mbaali mawasiliano yakapungua nikawaachia wasomi wenyewe wasome mi nikaingia kitaa kubangaiza nilikuwa nilifanya kazi ngumu balaa nalipwa buku 3 nauli, msosi imeisha mara nikahama nikaajiriwa sehemu mshahara kidunyuu, sikukata tamaa sasa hivi sio yule tena wasomi wangu wale kama nawaona vileee! Nimegundua kubadili Elimu kuwa pesa hapa Bongo lazima U-risk.
ulikuwa unapiga michongo gani kitaa
 
Niliacha kazi serikalini mwaka 2016 baada ya kudumu kwa miaka 4,,wengi walinishangaa hadi baadhi ya ndugu wakajua nimelogwa ila niliamua mwenyewe,,nikajikita kwenye biashara hapa ninapoandika wale walionioinga wengi wao ndo wananiomba misaada,,nilokuwa nafanya nao kazi wengi wananiomba njia za kupita nao waache....

NAJIVUNIA NILIPO
ulipiga michongo kitaa
 
Uzi umenigusa sana huu! Nilikuwa mzuri class ila nilipofika chuo mambo yakawa magumu nikafeli, sikukata tamaa washkaji kwa mbaali mawasiliano yakapungua nikawaachia wasomi wenyewe wasome mi nikaingia kitaa kubangaiza nilikuwa nilifanya kazi ngumu balaa nalipwa buku 3 nauli, msosi imeisha mara nikahama nikaajiriwa sehemu mshahara kidunyuu, sikukata tamaa sasa hivi sio yule tena wasomi wangu wale kama nawaona vileee! Nimegundua kubadili Elimu kuwa pesa hapa Bongo lazima U-risk.
Hujasimulia uliweza vipi kubadili elimu kuwa pesa
 
Back
Top Bottom