Wazazi wa kisasa msijisahau kwenye Malezi, hawa kina junior wamekuwa mizigo hawawezi hata kujioshea vyombo ni mizigo, ni kero kubwa wakiwa ugenini

Wazazi wa kisasa msijisahau kwenye Malezi, hawa kina junior wamekuwa mizigo hawawezi hata kujioshea vyombo ni mizigo, ni kero kubwa wakiwa ugenini

Haujui hata unachoongea😀

Hauwezi kudelegate kazi ambayo hata ww mwenyewe kuifanya ni ngumu kwako.

Na nikuambie tu huwa hawaji kuwa waratibu, na huwa wanakuja kuishi kwa survival na dependence ya hali ya juu kutoka kwa wazazi wao.

Ni watoto ambao hawana self discipline, self reliance.

Ni watoto ambao kuhandle hata ndoa au mahusiano kwao ni ngumu.

Ni watoto ambao hata kupanga life budget yao tu huwa hawawezi.

Ni watoto ambao wako FRAGILE in every aspect of life.
Haya ni mambo ambayo tunaamini tu mkuu kwasababu hatuuelewi ulimwengu wao.

Kwanza ni wachache sana, dollar millionaires ambao wapo 2,000-3,000 tu hapa nchini. Wamejitenga na wanaishi maisha tofauti sana.

Matarajio ya kuajiriwa, kupangisha nyumba kujichanga changa kama sisi hawana mkuu. Na wengi hawaishi Tanzania pekee, wana residencies za nchi nyingi.

Hawa ndo watu ninaozungumzia. Top 0.005% ya nchi.

Wanaoa, wanapata watoto na wanafanya biashara vizuri tu.

Nimeona maisha ya baadhi na wako poa tu.
 
Haya ni mambo ambayo tunaamini tu mkuu kwasababu hatuuelewi ulimwengu wao.

Kwanza ni wachache sana, dollar millionaires ambao wapo 2,000-3,000 tu hapa nchini. Wamejitenga na wanaishi maisha tofauti sana.

Matarajio ya kuajiriwa, kupangisha nyumba kujichanga changa kama sisi hawana mkuu. Na wengi hawaishi Tanzania pekee, wana residencies za nchi nyingi.

Hawa ndo watu ninaozungumzia. Top 0.005% ya nchi.

Wanaoa, wanapata watoto na wanafanya biashara vizuri tu.

Nimeona maisha ya baadhi na wako poa tu.
Nakuelewa sana mkuu,sisi wengi wetu tunalea watoto kwa kujihami kulingana na vipato vyetu,uwezekano wa maisha kubuma ni mkubwa Sasa tukilea watoto wetu kibabe hata vikibuma watajua namna ya kujipambania tofauti na ma billionea wao hatari ya kubuma ni ndogo mtoto wake asipojua hizi kazi ndogo ndogo sio inshu alishatengenezewa njia imara!
 
Kwa kuliona hilo serikali imeanzisha somo la historia ya Tanzania na maadili. Kidogo kina junior wataokota vitu vya maadili. Nimepitia kitabu kina mada za maadili, kazi za nyumbani, Kuheshimu wakubwa na jamii
 
Sijui ni nani aliwadanganya baadhi ya wazazi, hasa wale waliotoka kwenye familia duni, kwamba mara tu wakipata vijisenti basi watoto wao hawapaswi tena kufanya majukumu ya kujitegemea wala ya nyumbani.

  • Watoto wakila waache vyombo kwenye sinki house girl ataosha
  • watoto wakitoka shule watupe nguo kwenye tenga hg atafuta
  • watoto wakiamka wajianda tu kwenda shuleni hg atafagia uwanja
  • watoto wakichezea vitu wasivirudishe walipovikuta
  • mazingira ya nyumbani yakiwa machafu hayawahusu wanasubiri mkata majani
  • watoto wakunjiwe nguo
  • n.k.

Kuna baadhi ya ndugu zetu wnalea watoto hivi, watoto wakija kututembelea weekend majumbani hadi tunahisi wana matatizo ya kiafya kumbe ni malezi. Na sisi ni waelewa itakuwaje sasa wakiwa huko ugenini ?
Mimi sitaki matoto yenu manroilers kwangu
 
Kwanza saizi kama namshauri kijana wangu kuoa nitamwambia atafute wale Wanaoitwa Beki tatu will make good wife kuliko hao pimbi wengine waliofugwa kwenye mageti makubwa.
 
Back
Top Bottom