WAZAZI: Mwanangu anamchukia mdogo wake

WAZAZI: Mwanangu anamchukia mdogo wake

The only

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2011
Posts
11,131
Reaction score
14,636
Nina mtoto wa kike wa umri wa miaka 4 ambae tangu utoto wake amekuwa karibu na mimi sana ,nkitaka kwenda kazini inabidi nimvizie nitoroke na nikirudi nyumbani lazima nibuni mbinu za kutoroka kwenda baa akila kabla sijala anakula kidogo,nikirudi hata kama ni saa saba basi ataamka na kula na mimi ,na usiku hulala kanikumbatia ,hata nikiamka kwenda chooni ataamka na kunisindikiza akiamini natoroka . Aidha yuko na ukaribu wa wastani sana na mama yake kwa uchunguzi wangu mama yake anamkono wa kimachame kwao anapiga sana mtoto hata kwa kosa la kutema mate kwenye sofa mimi kanizoea hadi balaa.

Sasa mwezi uloisha nikajaaliwa mtoto wa pili kwa mwanamke huyu wa kiume ,siku mwanangu wa kike alipomuona hospitali naskia alipiga kelele '' Eeeeh wameninunulia mdogo wangu '' akawa mala amlete hiki mara kile na hata mdoli wake pendwa uitwao emii (lilikuwa jina la rafiki yake jirani alieondoka) alimuachia mtoto hospitali .

Sasa mziki ukaanza alipoanza kushuhudia attention yetu ilivyohamia kwa mtoto mpya siku moja aligoma kulala akiwa sebuleni baada ya kumbembeleza akiwa amejikunyata alilia sana na kusema '' dadiii naomba mumrudishe huyu mtoto kwao mlikomnunua mimi simpendi'' looh nafsi iliumia sana ,niligundua niliacha mbachao ,baya zaidi hata wanafamilia wengine wanaonekana wamehusika katika kumtenga .

Basi nikaja na mbinu matata ya kujifanya sitambui uwepo wa mwanangu mpya kikweli anafurahia sana nakatoa out,kuogelea ,nakapeleka mwenyewe shule na kitandani mama busy na kichanga mimi na ka daughter kangu .tatizo ni akilia tu mtoto anasema ''kelele rudi kwenu..'' ukiimpa zawadi anaficha eti mtoto ataiba ,hivi zipo mbinu zozote za kisaikolojia au nisubiri tu akue mambo yatajiset ,Maana tulipofikia hairuhusiwi kumiacha mtoto na dada yake .
 
Huyo yupo kwenye phallic stage of growth hutokea mtoto akiwa na miaka 4 hadi 6,katika umri Huo mtoto huanza kutambua utafauti uliopo kati ya Me na ke,mtoto wakike humpendelea baba na mtoto wa kiume huvutiwa na mama yake,

N.b itafika mda ataacha ila hata wewe upunguze taratibu kumcare
 
Hata mm niko na mtoto mdogo na mkubwa umri km wa kwako, mwanzoni wkt nimejifungua hali ilikuwa hivyo japo sio sana kama kwako lkn badae alianza kumzoea taratibu na sasa hata anaweza kulala nae, anambeba. Yaan kiufupi yy ndio kawa na mapenzi zaidi na mdogo wake kuliko wanafamilia wengine. Ht akitoka shule ndio anakuwa mlinzi wa mdogo wake.
 
Huyo yupo kwenye phallic stage of growth hutokea mtoto akiwa na miaka 4 hadi 6,katika umri Huo mtoto huanza kutambua utafauti uliopo kati ya Me na ke,mtoto wakike humpendelea baba na mtoto wa kiume huvutiwa na mama yake,

N.b itafika mda ataacha ila hata wewe upunguze taratibu kumcare
Mkuu nadhani ntazingatia japo kumcare ni kupunguza gape la uchungu wa kusahauliwa
 
Hata mm niko na mtoto mdogo na mkubwa umri km wa kwako, mwanzoni wkt nimejifungua hali ilikuwa hivyo japo sio sana kama kwako lkn badae alianza kumzoea taratibu na sasa hata anaweza kulala nae, anambeba. Yaan kiufupi yy ndio kawa na mapenzi zaidi na mdogo wake kuliko wanafamilia wengine. Ht akitoka shule ndio anakuwa mlinzi wa mdogo wake.
Hongera sana ni furaha iliyoje kwenye moyo wa mzazi watoto kupendana
 
Mi watoto wa ndugu yangu wanapishana mwaka mmoja wote watatu.. Mkubwa wa kike ana miaka mitano sasa kwakweli anawapenda sana wadogo zake... Akikuona tu umemshika umchape anageuka shield anakinga na onyo muacheee anapanic vibaya
Nimeshangaa hao wako mkuu
 
Hongera sana ni furaha iliyoje kwenye moyo wa mzazi watoto kupendana
Kwakweli inanipa faraja sana, ila mwanzoni nilikuwa naogopa hata kumuacha mtoto peke yake.
Mwenyewe akitoka shule anaanza kumsimulia vya shule basi mdogo wake akicheka yy anajua kameleewa basi nae anafurahi kumbe mwenzake anajichekea zake tu malaika wake
 
Mi watoto wa ndugu yangu wanapishana mwaka mmoja wote watatu.. Mkubwa wa kike ana miaka mitano sasa kwakweli anawapenda sana wadogo zake... Akikuona tu umemshika umchape anageuka shield anakinga na onyo muacheee anapanic vibaya
Nimeshangaa hao wako mkuu
Umeona eeeh, mi mwenyewe wa kwangu sasa hv kawa mlinzi wa mdogo wake. Hata akisikia hodi, yy ni mbio chumbani kukaa na mtoto hadi mgeni aondoke. Anakwambia wageni wataiba mtoto ndio maana anamchunga
 
Uyo atakuja kuwa karibu sana na bro wake, wewe tulia tu labda nikushauri usiache mpa misingi ya dini tangu sasa hivi utakuja gundua faida yake.

Pia hongera mkuu. Familia ni kitu kizuri sana.
Asante bro Najitahidi sana ,mfano nimeondoa stock yote ya pombe nyumbani ,sivuti sigara mbele yake na sirudi kabla sijala big g,Mamake humpeleka kanisa kila jumapili na nilimpeleka kujiunga sunday school wamesema awe anaenda kushinda tu ila at 5 ndo ataanza rasmi
 
Umeona eeeh, mi mwenyewe wa kwangu sasa hv kawa mlinzi wa mdogo wake. Hata akisikia hodi, yy ni mbio chumbani kukaa na mtoto hadi mgeni aondoke. Anakwambia wageni wataiba mtoto ndio maana anamchunga
waaaooo so sweety
 
Au katoto hako si kako kweli.. Jaribu kuwa makini labda umeuziwa mbuzi kwenye gunia..
Anyway uzi wako huu unatamanisha sana mzazi kuwa na ukaribu na watoto wake hata watoa mimba wanaumia sana waonapo mapenz ya dhati
 
Au katoto hako si kako kweli.. Jaribu kuwa makini labda umeuziwa mbuzi kwenye gunia..
Anyway uzi wako huu unatamanisha sana mzazi kuwa na ukaribu na watoto wake hata watoa mimba wanaumia sana waonapo mapenz ya dhati
[emoji3][emoji3][emoji3] JF majibu yote unapata. Uliyoyataraji na usiyoyataraji. So fun
 
Mume wa ndoa - JamiiForums
Hata mm niko na mtoto mdogo na mkubwa umri km wa kwako, mwanzoni wkt nimejifungua hali ilikuwa hivyo japo sio sana kama kwako lkn badae alianza kumzoea taratibu na sasa hata anaweza kulala nae, anambeba. Yaan kiufupi yy ndio kawa na mapenzi zaidi na mdogo wake kuliko wanafamilia wengine. Ht akitoka shule ndio anakuwa mlinzi wa mdogo wake.
Bila shaka baba wa mtoto ulimpata JF
 
Kila unakifanya maishani kina matokeo hasi au chanya maishani ,jitaidi unakuwa na mtoto usizidishe mapenzi mpaka mwingine akajua kuwa mm sipendwi.kuna mzee mmoja alikuwa kama ww yy alizidisha mahaba kwa mmoja pia alikuwa mkali sana kwa wengine sasa wale ambao hakuwa penda waliajiliwa America na huyu aliempenda alikuwa kawaida tu kimaisha.sasa hawa wa America kidogo tu mama kaitwa America kwa wanawe mpaka ikafikia hatua America ikawa kama home 🏠.baba wivu ukaanza mbona mm siitwi mara vile kisa alilofanya ni kubagua watoto nao wanambagua,majuto ni mjukuu.
 
Back
Top Bottom