Wazazi jifunzeni hili

Wazazi jifunzeni hili

Kaguo Willy

Senior Member
Joined
Nov 3, 2016
Posts
194
Reaction score
172
Habari za muda huu wanaJF.
Kama mada inavyojieleza nimekuwa nikijiuliza kuhusu wazazi wengi at least 90% huwa wanakula nyama nzuri zaid kuliko watoto wao na hii hujitokeza pale ambapo panapopikwa nyama let say nyama ya kuku au ya bata unaweza kukutana wazazi hasa wamama kupeleka nyama nzuri yaani mapaja na sehemu zenye minofu high table lakn watoto watakula nyama isiyo na kiwango na wakat mwingne watoto kuishia kupewa michuzi tu pasipo nyama.
Hivyo basi wazazi ni vyema tulifahamu hili kuwa kula nyama nzuri zaid kuliko watoto ni kuwadhulumu hak yao kwani watoto bado wanakua na wanahitaj protein kwa wingi kuliko wazazi ambao tayar wameshakua kimwili na kiakili tofaut na watoto ambao wanauhitaj zaid wa proteins na virutubisho mbalimbali kwa ajili ya kujenga miili yao na kuwasaidia kukua kimwili na kiakili kuliko hao wazee ambao hata cells zao zmezeeka
 
Mtoa thread kwani wewe ni mtoto au mtu mzima? Tuanzie hapo kwanza.
 
Sasa kuna kizazi utakinyima haki ya kula vinono hapo, maana hao wazazi wa leo nao walinyimwa vinono walipokuwa wadogo teh teh teh........

Nafikiri kwa kipindi hiki (zama hizi) wazazi au watoto nani anakula vizuri linategemea zaidi uwezo wa familia kuliko hizo taratibu za vizazi vya nyuma.
 
Mkuu, unazungumzia maisha ya kizamani sana.
Mimi kila siku baada ya kutoka kibaruani, lazima nirudi home nimebeba kitu chochote kwaajili ya wanangu. Na inapo fika wakati wa chakula cha usiku, nilazima nikae na nikule na wanangu kwa meza moja.
Hayo unayo yazungumzia nadhani ni aina ya maisha ya kizamani sana aiseeee
 
Oooh "Junia" you make yua dady to cry,stop that "junia".

Broken english 'juniya",teh
 
Ila mkuu hapo huoni ni cycle nzuri tu?

Wakubwa wanakula vinono kwakuwa wakiwa wadogo hawakuvila. Vivyo hivyo watoto ambao hawali vinono kwa sasa wakikua ndio utakuwa wakati wao wa kula vinono.

Mzunguko huo na uzingatiwe
 
Sasa kuna kizazi utakinyima haki ya kula vinono hapo, maana hao wazazi wa leo nao walinyimwa vinono walipokuwa wadogo teh teh teh........

Nafikiri kwa kipindi hiki (zama hizi) wazazi au watoto nani anakula vizuri linategemea zaidi uwezo wa familia kuliko hizo taratibu za vizazi vya nyuma.
, nimecheka haswaaa
 
Habari za muda huu wanaJF.
Kama mada inavyojieleza nimekuwa nikijiuliza kuhusu wazazi wengi at least 90% huwa wanakula nyama nzuri zaid kuliko watoto wao na hii hujitokeza pale ambapo panapopikwa nyama let say nyama ya kuku au ya bata unaweza kukutana wazazi hasa wamama kupeleka nyama nzuri yaani mapaja na sehemu zenye minofu high table lakn watoto watakula nyama isiyo na kiwango na wakat mwingne watoto kuishia kupewa michuzi tu pasipo nyama.
Hivyo basi wazazi ni vyema tulifahamu hili kuwa kula nyama nzuri zaid kuliko watoto ni kuwadhulumu hak yao kwani watoto bado wanakua na wanahitaj protein kwa wingi kuliko wazazi ambao tayar wameshakua kimwili na kiakili tofaut na watoto ambao wanauhitaj zaid wa proteins na virutubisho mbalimbali kwa ajili ya kujenga miili yao na kuwasaidia kukua kimwili na kiakili kuliko hao wazee ambao hata cells zao zmezeeka
Mila zetu za kiafrika, nakumbuka kwetu kijijini! Samaki wanawake hawali vichwa kwasababu mkipakuliwa wanaume kichwa ujue mboga imeisha kwahiyo mkatafute nyingine. Suala la mapaja na firigisi ni huwa ni nyama ya heshima kwa mgeni. Kwani wewe kuku kula nyumbani hafi waje wageni?
 
Hii tabia niliichukia Sana! Mamdogo anawapa wageni minyama yote na mikuku yote mpaka miguu! Sisi tunawahi utumbo pale kuku akitengenezwa tunachoma tunakula...wageni walkuwa wanafaidi Sana! Cfanyi ivo kwa watoto wangu hata aje mheshimiwa nani! Natoa mapaja kwa wanangu kwanza vitavyobaki tutagawana!
 
Back
Top Bottom