Wazanzibari kuajiriwa Tanganyika (Bara) ni sawa?

Wazanzibari kuajiriwa Tanganyika (Bara) ni sawa?

Nimefuatilia tangazo la TAMISEMI kuhusu ajira za walimu mwaka 2015 nikabaini kuwa Wazanzibari ambao hawastahili kuajiriwa Tanzania bara katika idara au taasisi isiyohusu mambo ya muungano wamepangwa katika Halmashauri mbalimbali Tanzania Bara kwa ajira katika shule za sekondari. Je serikali imetumia kigezo gani kutoa ajira hizo?

source: http://www.pmoralg.go.tz/noticeboar...u_Sayansi_2015_OWM-TAMISEMI_30April2015_3.pdf

Watanzania wanaajiriwa marekani na Uingereza na wapo wageni kutoka nchi za nje kama US, Uk, India n.k wanaajiriwa Serikalini hapa Tanzania kama wataalamu waelekezi na wanalipwa dola za kufa mtu n.k Sembuse Mpemba kuajiriwa huku Bara kwa mshahara wa laki 3??...ukisikia mawazo ya kimasikin ndio hayo!! ungesema mbona hawana mchango kwenye hizo ajira yaani hawana uwezo wa ku deliver ungeonekana kidogo una hoja yenye tija lakini eti kwanini wanaajiriwa bara?? kweli hilo linakukwaza?? kweli??? agghhh!!!..hizi IQ hizi!!
 
ungekuwa mwalimu alafu ukampa mwanafunzi topic ya mtoa mada kama swali alafu akajibu kama ulivyo jibu huku unatoa povu, ungempa maksi ngap? mfano uliotoa wa raia wa nje hauendani kwani wale wanaleta expertise fulani na hawaajiriwi permanently. in turn wapo watz wanaajiriwa botswana, us nk kupeleka utaalamu wao. kwani wazanzibari wanaoajiriwa huku wanaleta utaalamu ambao huku hamna wanaouweza? vilevile jibu swali kwa nn mwalimu wa kigoma haajiriwi na SMZ kama sehemu ya muungano. hii mada ckutaka kuchangia lakn umeniudhi ulivyojibu kwa mbwembwe hadi ukaponda IQ ya mleta mada wakt ww umejibu irrelevant answer
 
Wanzibar ni wanjanja mbele ya watanganyika,

Nchi ndogo kuliko hata Wilaya ya ilala , Lakini ina watumishi, mawaziri,wabunge Utitiri kuliko hata nzige na woote wanalipwa mishahara na posho na Tanganyika, Serikali ya Tanganyika ni buzi la Zanzibar inachunwa mpaka huruma na hawajitambui hadi leo.

Chao ni chao lakini cha Tanganyika ni cha woote! Huu ni muungano Analogia na wa Ajabu uliosalia Duniani, muungano wenye Rais na baraza la mawaziri kibao huku wabunge wa Zanzibar wao wanakula posho Dodoma na wanakuwa mawaziri Tanganyika lakini wabunge wa tanganyika ni marufuku huko zenji. Huu ni muungano Hasara kwani inatumika pesa nyingi sana kuubembeleza na kuwalea Utitiri wa watumishi waliojilundika huko zenji.

Tiba pekee ya hii Kero ni kuwa na Serikali moja tu Rais mmoja.

Halafu mwisho wa siku wa bara ndo wenye kuung'ang'ania Muungano? Kama muungano ungekua hauwanufaishi wabara basi wangeuvunja siku nyingi. Tanzania bara inafaidika sana na Zanzibar kwenye mambo ya utalii na vitu vingi ki ujumla. Tuwe ni wenye uwezo wa kufkiria kuliko kulalamika bila hoja wala data. Mimi ni mbara lakini nawasapoti wa zanzibari wavunje muungano ili wastarehe na zanzibar yao kama zaman. Nchi ilikua tajiri sana kabla ya muungano lakini sasa hivi imekua maskini kwa kunyonywa.
 
Watanzania wanaajiriwa marekani na Uingereza na wapo wageni kutoka nchi za nje kama US, Uk, India n.k wanaajiriwa Serikalini hapa Tanzania kama wataalamu waelekezi na wanalipwa dola za kufa mtu n.k Sembuse Mpemba kuajiriwa huku Bara kwa mshahara wa laki 3??...ukisikia mawazo ya kimasikin ndio hayo!! ungesema mbona hawana mchango kwenye hizo ajira yaani hawana uwezo wa ku deliver ungeonekana kidogo una hoja yenye tija lakini eti kwanini wanaajiriwa bara?? kweli hilo linakukwaza?? kweli??? agghhh!!!..hizi IQ hizi!!

Jamaa ni mvivu wa kufikiri.
 
Halafu mwisho wa siku wa bara ndo wenye kuung'ang'ania Muungano? Kama muungano ungekua hauwanufaishi wabara basi wangeuvunja siku nyingi. Tanzania bara inafaidika sana na Zanzibar kwenye mambo ya utalii na vitu vingi ki ujumla. Tuwe ni wenye uwezo wa kufkiria kuliko kulalamika bila hoja wala data. Mimi ni mbara lakini nawasapoti wa zanzibari wavunje muungano ili wastarehe na zanzibar yao kama zaman. Nchi ilikua tajiri sana kabla ya muungano lakini sasa hivi imekua maskini kwa kunyonywa.

Acha uongo.

Muungano wanafaidi viongozi wa pande zote mbili. Raia hawafaidiki na kitu chochote.

Hizo kazi Wasichana 32% Wanaume 68%

Tungejadili jinsi ya kuongeza rate ya kinadada ingependeza zaidi.
 
kuna tatizo mzanzibari kufanya kazi kwenye wizara inayohusiana na muungano, mkuu elimu ni mambo ya muungano tanzania
 
Issue hapa ni je, wazanzibari wanahaki ya kuajiriwa Tanzania bara katika taasisi au idara ambazo si za muungano? jibu swali acha kukurupuka.
Kabla ya kuuliza swali hili, unatakiwa ujiulize mwenyewe ambapo ndio msingi wa majibu aliyokupa Pasco. Je Watanganyika ni wazanzibari? Je wazanzibari ni watanzania? Je sifa za kazi unazosema ni sharti uwe Mtanzania? As long as mzanzibari ni mtanzania, hoja yako iko wapi?

Mimi binafsi sioni tatizo. Hoja yako itakuwa na maana kama kutakuwa na nchi na serikali inayoitwa TANGANYIKA. Lakini kwa kuwa hii nchi na serikali yenye jina hilo haipo, badala yake iko nchi ya Tanzania na kila mzanzibari ni mtanzania, hakuna utata hapo.
 
Last edited by a moderator:
Kama kuna kitu kinatufanya Watanzani wengi (Kama sio Waafrica) ni ugonjwa wa kukariri, tukisha jua NENO ubaguzi basi tunafanya application ya hilo NENO popote tu, ungejiuliza, suala la elimu from chekechea to secondary school ni la muungano? Nina hakika usingeandika ulicho kiandika! Wazanzibari wanaye waziri wao wa elimu, hivi wakiwa BARA na kufundisha shule zetu (hawakuanadaliwa mazingira ya elimu ya bara) watakua wana report kwa waziri wa elimu wa Zanzibar au wa bara?
Kwanini unaandika vitu usivyovijua kwa kujiamini?
Kwani mfanyakazi huwa anaripoti kwa nani? Kwa nchi au mfumo wa elimu alikosomea au analikoajiriwa?

Nani alikwambia mfumo wa elimu wa zanzibar haumuwezeshi mhitimu kufundisha Bara? Zanzibar wanasoma darasa la 1 hadi la 12 (bila kuruka darasa la 8) kisha wanafanya mtihani mmoja huohuo (NECTA); kwa kuzingatia sifa zilezile za kujiunga kidato cha 5 za bara na zanzibar ndio hizohizo. Wanasoma miaka 2 A level na wanafanya mtihani mmoja, siku moja na saa moja na mhitimu wa kiwango hicho wa Bara, kisha wanajiunga na vyuo vikuu vyovyote ima vya Tanzania au nje ya nchi. Wapi kuna tofauti ya mhitimu hapo?
 
Acha uongo.

Muungano wanafaidi viongozi wa pande zote mbili. Raia hawafaidiki na kitu chochote.

Hizo kazi Wasichana 32% Wanaume 68%

Tungejadili jinsi ya kuongeza rate ya kinadada ingependeza zaidi.

Sasa mimi nimetaja mtu au? Nkisema Tanzania Bara namaanisha Serekali na sio watu binafsi. Kiu jumla raia wa Tanzania wote hawafaidiki na nchi yao. Hamna cha kujadili, hio ni siasa zaidi, huwezi kupata muafaka kwenye suala la kuondoa umaskini kama waliowekwa serekalini hawana hima ya kuumaliza umaskini. Think!
 
Kabla ya kuuliza swali hili, unatakiwa ujiulize mwenyewe ambapo ndio msingi wa majibu aliyokupa Pasco. Je Watanganyika ni wazanzibari? Je wazanzibari ni watanzania? Je sifa za kazi unazosema ni sharti uwe Mtanzania? As long as mzanzibari ni mtanzania, hoja yako iko wapi?

Mimi binafsi sioni tatizo. Hoja yako itakuwa na maana kama kutakuwa na nchi na serikali inayoitwa TANGANYIKA. Lakini kwa kuwa hii nchi na serikali yenye jina hilo haipo, badala yake iko nchi ya Tanzania na kila mzanzibari ni mtanzania, hakuna utata hapo.

Nimekupata Mh. Mipangomingi; ni ukweli wazanzibari ni watanzania na watanzania bara si wazanzibari. Kwa logic ni sahihi wazanzibari kupewa ajira Tanzania bara katika mambo yasiyohusu muungano. Je, misingi ya kisheria inaruhusu jambo hilo kutendeka?
 

Mkuu ujinga ni kutojua, hivyo mtu kuambiwa ni mjinga kwa kutokujua, akiishajulishwa akajua, ujinga unamtoka na kumuingizia werevu, hivyo kwenyi hili wewe ni mjinga.

Naomba kuchukua fursa hii, kukuelewesha ili kukutoa huo ujinga wako, hivyo hutakuwa mjinga tena!.

Kila Mzanzibari, kwanza ni Mzanzibari, mwenye haki zote Zanzibar, kisha ni Mtanzania mwenye haki zote Tanzania. Hakuna mahali popote ambapo Mzanzibari anaweza kunyimwa ajira mahali popote Tanzania kama haki yake ya Utanzania, ila kwenye zile Taasisi za Muungano, Zanzibar ina quota yake ambapo lazima idadi ya watumishi fulani wawe Wanzanzibar.

Mfano wizara ya Elimu sio ya muungano, Watanzania wote wenye sifa za kuajiriwa wizara ya Elimu, wakiwemo Wanzanzibari wako huru kuomba kazi na wakikizi vigezo, wanaajiriwa kama Mtanzania mwingine yoyote!.

Hii inamaanisha nafasi za kazi zikitangazwa kwenye taasisi yoyote ya Tanzania iwe ya muungano au isiwe, Wazanzibari wenye sifa, wako huru kuomba nafasi hizo, ikitokea hakuna Mzanzibari yoyote mwenye sifa, then sii lazima kwa Mzanzibari kuajiriwa kwenye taaisi ambazo sio za Muungano.

Lakini kwenye taasisi za muungano, zikitangazwa kazi, pia Watanzania wote wenye sifa, wako huru kuomba, wakiwemo Wanzanzibari, ikitokea hakuna Mzanzibari mwenye sifa, then atatafutwa hata Mzanzibari asiye na sifa, hivyo kujengewa uwezo hadi kupata sifa na kukidhi vigezo, kwa sababu kwenye taasisi hizo, lazima asilimia fulani ya watumishi wake wawe Wazanzibari. Mfano ni Benki Kuu ya Tanzania, ni taasisi ya Muungano, kwenye set up yake, inaongozwa na gavana, na chini yake, wako ma deputy gavana watatu na mmoja wao, lazima awe ni Mzanzibari. Gavana ni Mtanzania, lakini kwa kipindi kirefu, alikosekana Mzanzibari, mwenye sifa za Deputy Governor, hivyo nafasi hiyo ilibaki wazi hadi alipopatikana Mzanzibari mwenye sifa hizo, Bw. Juma Reli, kwa sababu hiyo ni nafasi ya quota ya Zanzibar.

Gavana huyu aliyepo akimaliza muda wake na nafasi kubaki wazi, kama kuna Mzanzibari mwenye sifa za kuwa gavana, anaweza kuteuliwa kuwa gavana kwa mujibu wa Utanzania wake na sio Uzanzibari wake kwa sababu Kila Mzanzibari pia ni Mtanzania, ila sio kila Mtanzania ni Mzanzibari.

Natumaini umeelimika!.

Pasco
Pasco katoa somo zuri sana kwa wenye kuelewa watakuwa wameelewa
 
Back
Top Bottom