Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,129
- 35,147
Tayari raia mbalimbali wa Zanzibar wameanza kuhoji zilipo zile bilioni 200 ambazo naibu waziri wa fedha wa Tanzania alisema wiki iliyopita bungeni kuwa ni sehemu ya fedha katika zile Trilioni 1.5 ambazo kwenye ripoti ya CAG zimesemwa hazijulikani zimetumika wapi katika bajeti ya serikali.
Wanataka wabunge kutoka Zanzibar waliopo ndani ya bunge la Muungano kulivalia njuga suala hilo. Pia wanataka wajumbe wa baraza la wawakilishi kuibana serikali ya mapinduzi Zanzibar kuzitolea maelezo ya kina kuhusu hizo pesa zao kutoka katika ile Trilioni 1.5 ya Tanzania.
Shauku ya wazanzibar wengi ni kutaka kujua na kuchukuliwa kwa umakini mambo haya...
1/Utaratibu huo wa 'Ukarimu' wa serikali ya muungano kuwakusanyia mapato yao hayo ulianza lini hasa?(Hata wakati ambapo waziri wa Fedha alikuwa kutoka Zanzibar(Saada Mkuya) bado Zanzibar ilikuwa ikiambulia patupu katika baadhi ya mapato tata ya kimuungano)
2/Ni vyanzo vipi hasa vya kizanzibar vilivyopo upande wa Tanganyika vyenye kuingiza hizo Bilioni 200 kwa mwaka?
3/Kwanini Serikali ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ) na Baraza la wawakilishi la Zanzibar halikuwahi kuweka wazi utaratibu huo, mchanganuo wa mapato na matumizi hayo kila mwaka?
4/Ni vyema utaratibu wa 'ukarimu wa kukusanyiwa mapato na serikali ya Muungano wa kiasi kisichopungua bilioni 200 kwa mwaka(Ambapo ni sawa na wastani wa Milioni 547 kwa siku) ukawa Rasmi na Endelevu ili Zanzibar iendelee kuvuna haki zake za kimapato zilizopo Tanzania bara.
5/Na mwisho wengine wanahoji kwanini pesa zao zikusanywe kimya kimya na serikali ya Tanzania bila CAG kuzikagua. Usalama na uaminifu wa mapato yao uko wapi?
Wanataka wabunge kutoka Zanzibar waliopo ndani ya bunge la Muungano kulivalia njuga suala hilo. Pia wanataka wajumbe wa baraza la wawakilishi kuibana serikali ya mapinduzi Zanzibar kuzitolea maelezo ya kina kuhusu hizo pesa zao kutoka katika ile Trilioni 1.5 ya Tanzania.
Shauku ya wazanzibar wengi ni kutaka kujua na kuchukuliwa kwa umakini mambo haya...
1/Utaratibu huo wa 'Ukarimu' wa serikali ya muungano kuwakusanyia mapato yao hayo ulianza lini hasa?(Hata wakati ambapo waziri wa Fedha alikuwa kutoka Zanzibar(Saada Mkuya) bado Zanzibar ilikuwa ikiambulia patupu katika baadhi ya mapato tata ya kimuungano)
2/Ni vyanzo vipi hasa vya kizanzibar vilivyopo upande wa Tanganyika vyenye kuingiza hizo Bilioni 200 kwa mwaka?
3/Kwanini Serikali ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ) na Baraza la wawakilishi la Zanzibar halikuwahi kuweka wazi utaratibu huo, mchanganuo wa mapato na matumizi hayo kila mwaka?
4/Ni vyema utaratibu wa 'ukarimu wa kukusanyiwa mapato na serikali ya Muungano wa kiasi kisichopungua bilioni 200 kwa mwaka(Ambapo ni sawa na wastani wa Milioni 547 kwa siku) ukawa Rasmi na Endelevu ili Zanzibar iendelee kuvuna haki zake za kimapato zilizopo Tanzania bara.
5/Na mwisho wengine wanahoji kwanini pesa zao zikusanywe kimya kimya na serikali ya Tanzania bila CAG kuzikagua. Usalama na uaminifu wa mapato yao uko wapi?