Wazamiaji wa miaka ya 90

Wazamiaji wa miaka ya 90

Kuna rafiki yangu mmoja, kati ya mwishoni mwa miakaya 90 na mwanzoni mwa mwaka wa 2000 alizamia kwenda Ulaya. Safari za kipindi hicho ilikuwa za kibabe kweli mtu anaanza safari hana hata passport. Safari ilimpeleka mpaka Libya lengo ni kwamba ilikuwa aingie Morroco then wavushwe kuelekea Spain.
Katika safari hiyo alikutana na majanga mengi sana sana. Amenusurika kufa zaidi ya mara 20 tena akiwa ameshaona kaburi.

Sasa anadai akiwa Libya, anadai walibya ni wabaguzi sana hasa kwa waafrika wenzao weusi. Anadai ukipanda usafiri wa umma wanawake walikuwa wanaziba pua. Anasema muda mwingine ulikuwa ukipita mtaani unaona mama anaokota jiwe anampa mwanae akurushie.

Anadai sasa kimbembe uje ukutane na vijana walikuwa wanajiita Aska Boys (sina hakika kama nimewapatia). Anasema walikuwa wanatabia wanakuja na magari wanakuweka mtu kati, wanafungua boot wanatoa marungu, watakupiga mpaka ufe.

Sasa anasema akiwa libya, alikuwa hana pesa kabisa na kutoka libya ili uvushwe uende Morocco mpaka upande boat kuendelea na safari, ilikuwa inahitajika pesa nyingi. Yeye kwa muda huo aliikuwa ashageuka kuwa kama chokoraa. Na kipindi hicho mauaji kwa wageni yakawa yameongezeka.

Anadai katika kundi lao allikuwepo jamaa katoka Ethiopia ni Muorthodox alikuwa akisali sana sana. Jamaa akamfuata akamwambia amsaidie pesa kidogo ili aweze kuondoka pale maana wenzake walikuwa wengi wao wana mpango wa kuondoka baada ya hali kuwa mbaya.

Jamaa eti akamuuliza, huna mtu anayeweza kukutumia pesa. Jamaa akamwambia sina ila kuna kaka yangu ana pesa nyingi sana ila hawezi kunipatia pesa maana hata hii safari nimeianza kwa kumkumbia yeye alikuwa anataka kuniua. Jamaa akamwambia, usiku njoo nikufanyie maombi, lakini iwe saa tisa usiku.

Kweli usiku wa saa tisa akaenda, eti jamaa akachora chora mviringo sakafuni akamwambia aingie kati, kisha wakaanza kumuombea yeye na wenzake.
Baada ya maombi akamwambia asubuhi kampigie simu kaka yako, mwambie akutumie dollar 2000, atakutumia. Usipunguze na wala usiongeze. Jamaa anadai kesho yake akaenda sehemu ya kupiga simu akampigia simu kaka yake, alipomueleza hakubisha kabisa ila akamwambia atamtumiaje ile pesa.

Kipindi hicho anasema libya kulikuwa hakuna huduma za western union, wala money gram. Anadai watu walipokuwa wakitaka kupokea pesa, kulikuwa na mzungu raia wa spain pale ana ofisi iko kisiwa cha Lampedusa, hivyo pesa inatumwa kwenda Lampedusa, akiconfirm imefika kule unaenda kwake anakupa cash pale Libya.

Basi jamaa akawa ametumiwa pesa akaondoka pale. Japo huko mbele alipata majanga mengine.

Jamaa alifanikiwa fika Mexico, Equidor na huko pia alipata majanga hadi akapoteza korodani baada ya kuanguka mikononi mwa drug dealers.
Duu...mkuu jamaa alifikaje Mexico wakati hakuwa na passport? na kwa hilo la ubaguzi wa libya nakubaliana na wewe mkuu,,....hadi sasa ni wabaguzi sana Mkuu... Kuna jamaa yng wa kinigeria alishapia hapo,,2016.,hyo njia ya Nigeria,,Niger,,Libya,,Italy..
aliishi hapo Libya kwa miezi 6 kabla ya kuelekea Italy anapoishi hadi sasa,,,,,

anasema iliwachukuwa masaa 18 kutoka bahari ya Libya hadi kuikuta blue sea,,,bahari ya Italy,,,

pia anakwambiya ktk hyo network ya human traffic ni kubwa sana,,,na inaanzia huko nigeria,,senegal niger,,
kuna watu wana contacts za jamaa wa libya,,,wanasema wanakusanywa watu zaidi ya 500 au 400 kila mtu atatoa dola zisizopunguwa 1000 halafu wananunuwa boat wanaweka mashine,,,

halafu yule boat man,,,anakuwa among migrants nae anakuwa hatoi pesa za usafiri lakini kazi yake ni kuendesha boat ile,,,sasa anakwambiya wanapotoka lazima wawataarifu baadhi ya askari on duty wa libya wa majini ili wawaache watoke eneo la libya,,,,
kwani wasipotaarifu na kuwapa pesa ,,jamaa wakiwafukuzia na boat zao ni too speed...

anasema wakikamatwa kabla ya kuingie the blue sea,,basi adhabu yao ni kurudishwa Libya,,, na kipigo juu huko gerezani,,pia adhabu yake ni euro 500 kila mmoja ndy unaachiwa huru...tena unapewa simu uwapigie ndugu zako huko walipo wakutumie pesa,,

kuna Ethiopians,, Somali,,Nigerians, senegalis na waafrica weusi wengi tu kwnye magereza yao hapo Libya ktk suala ka kukamatwa baharini.,,,,,

jamaa anakwambiya sometimes hao migrants wanaona ni bora kujitosa baharini kuliko kukamatwa na askari wa libyakurudishwa Libya,,,

jamaa anasemaa hiyo njia mtu akipita na kufika salama Italy,,,basi ni Mungu tu ametenda,miujiza,,lakini ni nusu kifo njia nzima,,,na anakwambiya hapo Libya kuna kundi la walibya weupe linabaka wanawake weusi wa Africa,,,,

mfano wakiona mwanaume mweusi anaingia chumbani na mwanamke muarabu wa Libya basi hao jamaa Wanakuja,,,na haijulikani wanapewa taarifa na nani,,pengine ni jukumu la kila raia mwarabu mwenye roho ya kibaguzi,,,,

kutoa taarifa kwa kundi hilo kuja kuteka watu,,basi anakwambiya wakija wanakupiga na kumchukuwa Dada yao wa kiarabu,,,
kama ni mweusi basi atabakwa mbele yako,,huku wewe ukipokonywa Mali zako,,,

nilishasema siku moja kuwa mwafrika ni yule mweusi tiiii,,,na sio hawa waarabu wa Africa,,,ni hawa wazungu ndy waliowaweka upande wetu,,,lakini sio wenzetu..kabisa,,,
 
Duu...mkuu jamaa alifikaje Mexico wakati hakuwa na passport? na kwa hilo la ubaguzi wa libya nakubaliana na wewe mkuu,,....hadi sasa ni wabaguzi sana Mkuu... Kuna jamaa yng wa kinigeria alishapia hapo,,2016.,hyo njia ya Nigeria,,Niger,,Libya,,Italy..aliishi hapo Libya kwa miezi 6 kabla ya kuelekea Italy anapoishi hadi sasa,,,,,anasema iliwachukuwa masaa 18 kutoka bahari ya Libya hadi kuikuta blue sea,,,bahari ya Italy,,,pia anakwambiya ktk hyo network ya human trafic ni kubwa sana,,,na inaanzia huko nigeria,,senegal niger,,kuna watu wana contacts za jamaa wa libya,,,wanasema wanakusanywa watu zaidi ya 500 au 400 kila mtu atatoa dola zisizopunguwa 1000 halafu wananunuwa boat wanaweka mashine,,,halafu yule boat man,,,anakuwa among migrants nae anakuwa hatoi pesa za usafiri lakini kazi yake ni kuendesha boat ile,,,sasa anakwambiya wanapotoka lazima wawataarifu baadhi ya askani on duty wa libya wa majini ili wawaache watoke eneo la libya,,,,kwani wasipotaarifu na kuwapa pesa ,,jamaa wakiwafukuzia na boat zao ni too speed...anasema wakikamatwa kabla ya kuingie the blue sea,,basi adhabu yao ni kurudishwa Libya,,, na kipigo juu huko gerezani,,pia adhabu yake ni euro 500 kila mmoja ndy unaachiwa huru...tena unapewa simu uwapigie ndugu zako huko walipo wakutumie pesa,,kuna Ethiopians,, Somali,,Nigerians, senegalis na waafrica weusi wengi tu kwnye magereza yao hapo Libya ktk suala ka kukamatwa baharini.,,,,,jamaa anakwambiya sometimes hao migrants wanaona ni bora kujitosa baharini kuliko kukamatwa na askari wa libyakurudishwa Libya,,,jamaa anasemaa hiyo njia mtu akipita na kufika salama Italy,,,basi ni MUNGU tu ametenda,miujiza,,lakini ni nusu kifo njia nzima,,,na anakwambiya hapo Libya kuna kundi la walibya weupe linabaka wanawake weusi Wa Africa,,,, mfano wakiona mwanaume mweusi anaingia chumbani na mwanamke muarabu wa Libya basi hao jamaa Wanakuja,,,na haijulikani wanapewa taarifa na nani,,pengine ni jukumu la kila raia mwarabu mwenye roho ya kibaguzi,,,, kutoa taarifa kwa kundi hilo kuja kuteka watu,,basi anakwambiya wakija wanakupiga na kumchukuwa Dada yao wa kiarabu,,,kama ni mweusi basi atabakwa mbele yako,,huku wewe ukipokonywa Mali zako,,, nilishasema siku moja kuwa mwafrika ni yule mweusi tiiii,,,na sio hawa waarabu wa Africa,,,ni hawa wazungu ndy waliowaweka upande wetu,,,lakini sio wenzetu..kabisa,,,
Yah ndicho kinachoendela na anadai pia wanaija wanauza madada zao huko wanawatoa Nigeria wanawadanganya kuwa wanawapeleka spain na Italy wakifika Libya wanaishia kuwa sex slave.
Jamaa kwanza alienda Equotorial guinea kapata passport ya huko. Jamaa hakusafiri moja kwa moja yani alipotoka libya alizonguka nchi kadhaa kwa miaka kadhaa kabla ya kwenda nje ya bara la afrika. Alienda Equatorial Gunnea, Guinea Bissau, Mali, Ivory Coast, alifungwa miaka mitatu kwenye gereza la Bukina fasso ambapo anakwambia kuna magangwe hatari mle kusurvive hiyo miaka ilikuwa muujiza.
 
Siku hizi mambo yamekuwa rahisi kwasababu ya science na technology. Mana kipindi kile hata simu zilikuwa adimu. Information pia ilikuwa limited, siku hizi unaweza ingia internet ukapata taarifa ya uendakohata kabla hujafika.
Yeah nakubaliana na wewe mkuu, though science & technology hiyo ya sasa pia imeleta ugumu kwa namna fulani kwa wazamiaji wa sasa kwenye kuzamia, mambo yamekuwa computerized sasa hata taarifa zako once zipo kwenye system basi zinaweza kufika sehemu yoyote refer kesi za zamani watz kujilipua ni wasomali sasa ni mwendo wa electronic passport ukipita airport tayari taarifa zako zinakusanywa, zile janja janja za kizamani hakuna sasa, kadri teknolojia inavyokuwa ndio wazamiaji nao wanakuwa more advanced na mbinu kali zaidi 😅
 
Hiyo tunamuita ni BAHARIA wa inchi kavu...salute kwake...maana wanakwambiya jela ni shule pia..
Yah ndicho kinachoendela na anadai pia wanaija wanauza madada zao huko wanawatoa Nigeria wanawadanganya kuwa wanawapeleka spain na Italy wakifika Libya wanaishia kuwa sex slave.
Jamaa kwanza alienda Equotorial guinea kapata passport ya huko. Jamaa hakusafiri moja kwa moja yani alipotoka libya alizonguka nchi kadhaa kwa miaka kadhaa kabla ya kwenda nje ya bara la afrika. Alienda Equatorial Gunnea, Guinea Bissau, Mali, Ivory Coast, alifungwa miaka mitatu kwenye gereza la Bukina fasso ambapo anakwambia kuna magangwe hatari mle kusurvive hiyo miaka ilikuwa muujiza.
 
Hiyo tunamuita ni BAHARIA wa inchi kavu...salute kwake...maana wanakwambiya jela ni shule pia..
Alikamatwa akiwa na mwenzake ila akaamua kubeba msala wote jamaa abaki nje huenda atamsaidia. Jamaa alipoachiwa akakimbia hakuwa kumsikia mpaka alipokutana naye mwaka juzi facebook jamaa anaishi Germany ana familia na watoto. Jamaa mpaka elo anammaindi.
 
Haaaaa Haaaaa, uwe na hela ya maana umtafute black kule mfunge ndoa huku then akualike kule kama mke wake,
Baadaye mapeana divorce,. Maisha yanaendelea.
Kule kazi zipo sana, hela inaingia vizuri maana Unaweza fanya kazi mbili tofauti
Kimbembe kufungia ndoa huku😆😆!
 
Mkuu story zake zinatisha mfano jamaa kuna kipindi alikuwa stuck kwenye jangwa la Kufra. Hana pesa, hana chakula hana pa kulala. Anakwambia hilo eneo hadi nzi ni masikini wa kutupa wanategemea waje wafyonze maji maji kwenye macho ya binadamu iliku survive
Duh, nasikia hii Kufra ipo katikat kabisa ya jangwa la Sahara.. kuna watu wamepitia mikasa sana sana aisee
 
Duh, nasikia hii Kufra ipo katikat kabisa ya jangwa la Sahara.. kuna watu wamepitia mikasa sana sana aisee
Yah ni kati ya mikoa ya libya ambapo 91% ni jangwa. Jamaa anakwambia ukiwa katika lile jangwa hujui N, S, E, W ni wapi. Anakwambia maisha ya wakazi wa pale ambao nao ni wachache wamejenga vijumba vya udongo ni magumu sana sana sana. Ndiyo maana anasema hata nzi wa pale ni masikini sana. Anakwambia kuna mbuzi na kondoo chache nao wanaishi kwa kula karatasi na vitu vya ajabu na ajabu kusurvive
 
Back
Top Bottom