Wawania Ubunge Rukwa waanza kampeni huku viongozi wakiwa kimya

Mzee wa Twitter

JF-Expert Member
Nov 5, 2023
1,278
2,041
Wadau kitendo cha kuanza KAMPENI kabla ya Muda ni ishara tosha kuwa CCM imeshindwa kuwadhibiti wanachama wake waliojiamuliwa kuanza Kampeni kabla ya Muda wake.

Mkoani Rukwa Wanachama wa CCM wameanza kujipitisha pitisha na kufanya Mikutano ya siri kwa kukutana na Wajumbe mbalimbali.

Majimbo yalikumbwa na hizo KAMPENI HARAMU ni pamoja na JIMBO la NKASI Namanyere na Jimbo la Kwera .Kinachoshangaza ni Ushiriki kwa baadhi ya Viongozi wa CCM katika hizo Kampeni haramu.Hivi Karibuni KAIMU KATIBU MKUU wa Ccm Bw.Macha akiwa katika Jimbo la Ubungo alitoa ONYO KALI kwa wale wote wanaojipitisha kwenye Majimbo wakati Muda wake bado.

Kutokana na huo Ukiukwaji wa Sheria na taratibu za Chama baadhu ya Wananchi wametoa maoni yao na kukiomba Chama ch Mapinduzi kuwachunguza wote wanaofanya Kampeni kabla ya Muda na kuwafukuza Uanachama na wakapendekeza pia kuwa CCM itoe namba za Simu kwa Wanachama wake ili wawaripoti Wale wote wanaojipitisha ktk MAJIMBO yao kufanya Kampeni kabla ya RUHUSA ya CHAMA.

Pia Wanachama hao wakahoji Ukimya wa Viongozi wa Chama katika ngazi zote juu ya Suala la kuanza KAMPENI kabla ya Muda sahihi.

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
 
Mh.Vincent Mbogo wa Nkansi,asiwe na wasiwasi,kama anakubalika atachaguliwa tena,ilhali Mh.Deus Sangu wa Jimbo la Kwela,naye pia atulie,kama anakubalika pia,atapita.Watulie,tunawafuatilia kwa umakini.
 
Hii tabia inaongozwa na viongozi walioteuliwa kuwa ma dc na ma rc wengi wanarudi kwenye majimbo yao kutengeneza mazingira ya kugombea ubunge 2025
 
Mh.Vincent Mbogo wa Nkansi,asiwe na wasiwasi,kama anakubalika atachaguliwa tena,ilhali Mh.Deus Sangu wa Jimbo la Kwela,naye pia atulie,kama anakubalika pia,atapita.Watulie,tunawafuatilia kwa umakini.
Huyu mbogo alikuwa ex bodyguard wa jiwe
 
Wadau kitendo cha kuanza KAMPENI kabla ya Muda ni ishara tosha kuwa CCM imeshindwa kuwadhibiti wanachama wake waliojiamuliwa kuanza Kampeni kabla ya Muda wake.

Mkoani Rukwa Wanachama wa CCM wameanza kujipitisha pitisha na kufanya Mikutano ya siri kwa kukutana na Wajumbe mbalimbali.

Majimbo yalikumbwa na hizo KAMPENI HARAMU ni pamoja na JIMBO la NKASI Namanyere na Jimbo la Kwera .Kinachoshangaza ni Ushiriki kwa baadhi ya Viongozi wa CCM katika hizo Kampeni haramu.Hivi Karibuni KAIMU KATIBU MKUU wa Ccm Bw.Macha akiwa katika Jimbo la Ubungo alitoa ONYO KALI kwa wale wote wanaojipitisha kwenye Majimbo wakati Muda wake bado.

Kutokana na huo Ukiukwaji wa Sheria na taratibu za Chama baadhu ya Wananchi wametoa maoni yao na kukiomba Chama ch Mapinduzi kuwachunguza wote wanaofanya Kampeni kabla ya Muda na kuwafukuza Uanachama na wakapendekeza pia kuwa CCM itoe namba za Simu kwa Wanachama wake ili wawaripoti Wale wote wanaojipitisha ktk MAJIMBO yao kufanya Kampeni kabla ya RUHUSA ya CHAMA.

Pia Wanachama hao wakahoji Ukimya wa Viongozi wa Chama katika ngazi zote juu ya Suala la kuanza KAMPENI kabla ya Muda sahihi.

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
Mbona mwenyekiti wa chama aliianza kampeni siku ya kwanza alipoingia madarakani, ni sawa tu.
 
Huyu mbogo alikuwa ex bodyguard wa jiwe
Obvious,alikua bodyguard wa Jiwe,kama kafanya vizuri katika kipindi hiki chote alichokalia kiti cha ubunge,wala asiwe na papala,atarudishwa na wananchi wa jimbo lake la Nkansi kwa uhakika.
 
Back
Top Bottom