Waumini wa dini ya Kikristo wapungua Marekani

Waumini wa dini ya Kikristo wapungua Marekani

thesym

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2012
Posts
3,866
Reaction score
4,854
Utafiti uliohusisha idadi ya watu 35000 umeonyesha kuwa 70% ya wamarekani walijitambulisha wao kama waumini wa dini ya kikristo, hali hii ni tofauti na ule utafiti wa mwaka 2007 ambapo ilionyesha 78% ya wamarekani walijitambulisha kama wakristo ikiwa ni kiwaongo cha kupungua kwa 1% kwa kila mwaka. Pew research center.

======
religion.jpg
Idadi ya Waumini wa dini ya kikristo imeendelea kuonyesha kupungua kwa mujibu wa tafiti mbalimbali huko nchini USA ambako kuna idadi kubwa ya waumini wa dini hiyo hii ni kwa mujibu wa shirika la Pew Research Center.
Zaidi mabadiliko haya yameathiri karibu dini zote huko nchini marekani na kupungua kwa idadi ya watu wanaofuata dini imeonekana zaidi likitokea katika makundi ya vijana.

Marekani ni nchi ambayo ni nyumbani kwa wakristo wengi kuliko dini nyingine yoyote lakini kwa bahati mbaya idadi ya watu walio na umri wa miaka 18 na kuendelea wanaojitambulisha kama wakristo imeendelea kupungua.

Utafiti uliohusisha idadi ya watu 35000 umeonyesha kuwa 70% ya wamarekani walijitambulisha wao kama waumini wa dini ya kikristo, hali hii ni tofauti na ule utafiti wa mwaka 2007 ambapo ilionyesha 78% ya wamarekani walijitambulisha kama wakristo ikiwa ni kiwaongo cha kupungua kwa 1% kwa kila mwaka.

Kwa mujibu wa tafiti za shirika la FaithSurvey na lile la taasisi ya 2012 Millenia Value ilionyesha 47% ya waliohujuiwa kuhusu biblia walisema ni neno la mungu lakini haupaswi kutilia umakini kila neno la kitabu hiko wakati 16% walisema ni kitabu cha hadithi za kale kilichoandikwa na watu.

Tanzania na afrika kwa ujumla ni sehemu ambayo ina waumini wengi wa dini mbalimbali kitendo cha nchi kubwa kupungua kwa waumini linatoa taswira mbaya kwa nchi zinazoendelea ukizingatia utandawazi na vijana walio wengi wanapenda kuiga mambo na kundi linaloathirika

Viongozi wa dini na watu mbalimbali hawana budi kuchukua hatua za ziada ili kuwaepusha waumini wa dini zao wasitumbukie katika janga la kutoamini uwepo wa mungu wala dini yoyote kwani si swala zuri.

Source:
America’s Changing Religious Landscape

Faith Survey | USA: Religious Surveys
 
Labda wamegundua kuwa dini za siku hizi ni biashara, wameamua kuniiga mimi kwa kuacha kusali
 
Kadri siku zinavoenda watu wanazid kushughulishwa na Dunia zaid kuliko Mungu
 
Siku za mwisho hizo zilisha tabiliwa kama ni mfuatiliaji mzuri wa injili hakuna chakushangaa sanasana kuzidi kushika imani yako na kusali.
Kwa wale Wakristo wenzangu tunao amini Yesu kristo alisulubiwa akafa msalabani akafufu na kupaa mbinguni kwaajili yetu basi tuendelee kukiri hivyo sio kuyumbishwa tofauti.
 
Siku za mwisho hizo zilisha tabiliwa kama ni mfuatiliaji mzuri wa injili hakuna chakushangaa sanasana kuzidi kushika imani yako na kusali.
Kwa wale Wakristo wenzangu tunao amini Yesu kristo alisulubiwa akafa msalabani akafufu na kupaa mbinguni kwaajili yetu basi tuendelee kukiri hivyo sio kuyumbishwa tofauti.
Keep it up paradise inawasubiri ,lakini vipi babu yako ambaye alikufa kabla mkoloni hajawaletea yesu kristo ataona mbingu kweli?
 
Siku za mwisho hizo zilisha tabiliwa kama ni mfuatiliaji mzuri wa injili hakuna chakushangaa sanasana kuzidi kushika imani yako na kusali.
Kwa wale Wakristo wenzangu tunao amini Yesu kristo alisulubiwa akafa msalabani akafufu na kupaa mbinguni kwaajili yetu basi tuendelee kukiri hivyo sio kuyumbishwa tofauti.
tangu enzi za akina mathayo wanasema dalili za mwisho,huo mwisho haufikagi tu jamani?

Polen kwa kusubiri jamani
 
Waumini wa Dini ya kikristu au mashabiki wa dini ya kikristo?
 
Back
Top Bottom