Mwanzi1
JF-Expert Member
- Sep 19, 2016
- 6,000
- 4,586
Ina stajabisha kuona wakenya leo wanalia lia eti watanzania wamejaa kwenye uwanja wao. Tumekuja hapa kutokana na kenjeli, dharau, na uwongo ambao wakenya mlikuwa mnausambaza duniani kupitia uwanja huu wa JF. Na sio hapa tu, hata kwenye majukwa mengine ya mitandaoni, wakenya wamekuwa wakipotosha ulimwengu kuhusu Tanzania. Mkitaka haya yaishe, na nyinyi mjirekebishe, mjue kama Tanzania ni nchi na inahitaji kuheshimiwa. Watanzania wazalendo hawatasita kuitetea nchi yao mpaka jasho la mwisho.