Nimejaribu kufuatilia mwenendo wa watumishi wengi wa serikali katika kipindi hiki nimegundua watumishi walio wengi hawampendi mh.
Wengi wao wamekua wakitumia msemo wa HAPA KAZI TU kuwanyanyasa watu wanaohitaji huduma kutoka ofisi za serikali.
Kwa mfano, walimu wakiwa wanatoa adhabu kwa wanafunzi wanasema hapa kazi tu. Kuonyesha kwamba hapa kazi tu ni adhabu.
Madaktari na Manesi ndo usiseme.
Askari nao hali ni the same.
Nini tatizo la watumishi?
Hawapendi uwajibikaji?
Karibu tujadili
Mimi nadhani labda wale watumishi wenye madai ya muda mrefu ambao walikuwa wanahitaji mafao yako yalipwe. Hebu fikiria nesi au mwalimu ambaye hana nyumba waliyopewa kazini, hana rent allowance, hana posho ya nauli halafu anapanda gari mbili afike kazini, na anatakiwa afike saa1:30as. mpaka 10 alasiri. hivi huyu atafurahia usimamizi mkali wakati mshahara ni finyu na inamlazimu afanye shughuli nyingine ile amudu mahitaji ya familia?
Naamini falsafa ya Rais wetu mpendwa itazingatia pia maslahi na hali za wafanyakazi.
Ndugu yangu kama unasubiri hadi upandishiwe mshara ndio utoe huduma nzuri hapo kwa kweli hatutafika mbali. Nadhani alikua ni Raisi keneddy wa USA aliwaambia wananchi wake "usielize serikali ikufanyie nini, jiulize wewe itaifanyia nini serikali na nchi yako"
Niko sweden na ni nchi ya kitajiri lakini miaka 90 iliopita ilikua nchi ya kimaskini hadi baadhi ya wananchi wakakimbilia USA.
Mzee mmoja alinielezea maisha yake alipokua kijana na alikua anafanya kazi yukuendesha treni. Anasema hali ilikua ngumu mshahara mdogo kiasi kwamba alikua hana uwezo wa kununua socksi ndefu kwa ajili ya baridi akawa anatumia magazeti akichomeka ndani ya suruali lakini walifanya kazi kwa bidii na upendo wakijua ipo siku maisha yatabadilika na ndio maisha tunayo yaona leo ya Sweden.
Hapo hospitalini jinsi manesi wanavyo fanya kazi inasikitisha, ni wajeuri kupita kiasi. Kwa hiyo inamaana hadi mshahara upandishwe ndio atoe huduma nzuri??
Raisi wetu ameanza vizuri, tumpongeze na tumpe moyo ili naye azidikupata nguvu
Izo ni shoo tu za kisukuma. Ngoja ngoma inoge kama ajaanza kuweweseka kama aliemtanguliaaisee msukuma ni noma sana.. na bado wale wazembe "atalala nao mbele"
ni hapo kwenu lakini wengi hawampendi,tena hapa kwetu tokea kampeni,wanasema atawapelekesha sana,Watanzania hawapendi kufanya kazi aise,inaniuma sana ,watu wanataka wakae tu ,kisha wabebe mshahara na kula rushwa,kama hatutabadilika kila mmoja, kamwe Tanzania itabaki hapahapa hata aje Malaika kutuongoza..Acha uongo mbona ofisini kwetu shangwe tu hao watumishi labda siyo hawa wa tanzania.
Muongo wewe
ni hapo kwenu lakini wengi hawampendi,tena hapa kwetu tokea kampeni,wanasema atawapelekesha sana,Watanzania hawapendi kufanya kazi aise,inaniuma sana ,watu wanataka wakae tu ,kisha wabebe mshahara na kula rushwa,kama hatutabadilika kila mmoja, kamwe Tanzania itabaki hapahapa hata aje Malaika kutuongoza..
Wewe unatembeza pichu huko mtaani halafu unakurupuka kusema Watumishi wa Serikali hawampendi Mhe. Magufuli!!!! Huo utafiti wako wa mahesabu ya pichu umeufanyia wapi? mbona sisi tuko huku na hatujakuona??? Acha ubwege na uchonganishi wewe!!!! Loh!!! Aibu yako hata wewe?????
wengi wanampenda isipokuwa wale wenye makandokando.
Wafanyakazi wengi ni wazembeee
Wanaogopa speed ya msukumaaa
Kumuogopa Magufuli mi sawa kumuogopa polisi. kwanini uogope pole kama we si mhalifu?
Acha uongo mbona ofisini kwetu shangwe tu hao watumishi labda siyo hawa wa tanzania.
Wasiompenda ni WEZI, WABADHIRIFU, MAFISADI, WANAPITISHA DILI ZA WASIOLIPA KODI, wapo wengi na uzuri wanafahamiks.Nimejaribu kufuatilia mwenendo wa watumishi wengi wa serikali katika kipindi hiki nimegundua watumishi walio wengi hawampendi mh.
Wengi wao wamekua wakitumia msemo wa HAPA KAZI TU kuwanyanyasa watu wanaohitaji huduma kutoka ofisi za serikali.
Kwa mfano, walimu wakiwa wanatoa adhabu kwa wanafunzi wanasema hapa kazi tu. Kuonyesha kwamba hapa kazi tu ni adhabu.
Madaktari na Manesi ndo usiseme.
Askari nao hali ni the same.
Nini tatizo la watumishi?
Hawapendi uwajibikaji?
Karibu tujadili