Watumishi hewa 515 wagundulika katika mikoa mitatu

Watumishi hewa 515 wagundulika katika mikoa mitatu

Jambo jema. Pesa hiyo iliyokua inapotea itaelekzwa kwenye huduma za kijamii.
 
Ni Hatari Sana hizo B142 zimelambwa kwa muda mrefu sana....Ni wakati wa mabadilikooo.....
 
Siku 15 zilizotolewa na Rais Magufuli kwa Wakuu Wapya wa Mikoa kuhakikisha wanawabainisha na kuwaondoa wafanyakazi hewa zimeanza kutoa picha kuhusu tatizo la wafanyakazi hewa nchini.

Mpaka sasa imebainika kuna wafanyakazi 515 katika mikoa mitatu ambayo ni Kigoma (169), Dodoma (144) na Singida (202).

Taswira hii inaonyesha jinsi ambavyo tatizo la wafanyakazi hewa linaweza kuwa ni kubwa zaidi ya ilivyofikiriwa hasa ikichukuliwa limekuwepo kwa muda mrefu huku mamilioni ya pesa za walipa kodi yakienda kwenye mifuko ya wajanja wachache.

Inakadiriwa serikali ina wafanyakazi zaidi 500,000 na inalipa mishahara takriban Sh. bilioni 549 kwa mwezi, ambayo kati ya fedha hizo kuna malipo ya wafanyakazi hewa.

Katika repoti yake ya mwaka 2013/14, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alibainisha kuna zaidi ya Sh141.4bn zimelipwa kwa wafanyakazi hewa katika mwaka wa fedha.

Kwa nini tatizo hili halikushughulikiwa mapema zaidi endapo CAG alisharipoti serkalini, na wabunge pia wakijua tangu 2013? RCs wamepeleka stadi gani za kipekee ambazo wakurugenzi na wahasibu wao hawana za kubaini wafanya kazi hewa? Pesa zote hutoka Hazina, na wafanyakazi serkalini wanajulikana na Utumishi; sasa kwa nini uchunguzi huu usianze huko Dar? Si bure, kuna mengi hapa hatuambiwi zaidi ya chama cha siasa kutumia pesa zetu uma kuwalipa makada wake, tayari kwa 2020!
 
Haya yote JK aliyajua ila hakua na utashi wa kuyafanyia maamuzi manake alijua kwa kiasi kikumbwa wanaojilipa ni hao hao watu wa system na makada wa chama,inasikitisha jinsi alivyofanya nchi shamba la bibi kila mtu anachota anaondoka zake.Kuna haja ya kufuta kinga ya Raisi kushitakiwa kwy katiba mpya ya Magu km alivyoahidi ili haki itendeke.Km Zambia iliwezekana hata bongo inawezekana.
 
Nilikuwa iramba jaman ilikuwa salary slip kwa salary slip jina kwa jina sura kwa sura. Kiukwel wale wadau walikuwa makini. Tunangoja impact sasa
 
Angalizo lako ninakubaliana nalo 101%

Hakuna kitu kinachonichukiza kama kuwa na bunge lenye wabunge wa viti maalum ili tu kuweka uwiano katika jinsia. Haya ni matumizi mabaya ya pesa za walipa kodi.
Hata Mimi nawashangaa sana Hawa viti maalum
 
Wasiishie tu kubaini wafanyakazi hewa,bali waliohusika pia waadhibiwe na ikiwezekana warudishe hizo pesa
 
Haya yote unaoyaona na matokeo ya Kikwete kuanzisha system ya kuyabaini hayo, jisomee:

Katika repoti yake ya mwaka 2013/14, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alibainisha kuna zaidi ya Sh141.4bn zimelipwa kwa wafanyakazi hewa katika mwaka wa fedha.
Kapewa taarifa 2013/14 hadi kaondoka madarakani hajafanya chochote na tatizo bado sugu, halafu wewe unaandika upupu hapa. Kweli wewe zuzu.
 
Ningemwita Kikwete shujaa angetuambia Escrow ya nani na nani alihusika, bila kupepesa na kwa kumuogopa Mungu from his heart.

Ardhi itapasuka siku akifanya hilo yeye JK au huyu Magu
 
Haya yote unaoyaona na matokeo ya Kikwete kuanzisha system ya kuyabaini hayo, jisomee:

Katika repoti yake ya mwaka 2013/14, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alibainisha kuna zaidi ya Sh141.4bn zimelipwa kwa wafanyakazi hewa katika mwaka wa fedha.
Wewe Mazaa niaje? Unatetea mpaka wafu? Alichukua hatua gani??? Kuzuia wafanyakazi hewa?????
 
Hongera Rais maana kuna vijana wengi wako mtaani na wana vyeti vizuri ni muda wao wa kupata nafasi za kazi kuchukua nafasi.
 
Haya yote unaoyaona na matokeo ya Kikwete kuanzisha system ya kuyabaini hayo, jisomee:

Katika repoti yake ya mwaka 2013/14, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alibainisha kuna zaidi ya Sh141.4bn zimelipwa kwa wafanyakazi hewa katika mwaka wa fedha.
yaan we bibi ni mdini kupitiliza akitajwa wa dini yako tu lazima umtetee ht kama ni jipu kweli.
 
yaan we bibi ni mdini kupitiliza akitajwa wa dini yako tu lazima umtetee ht kama ni jipu kweli.

Huo udini maana yake nini? Au kumtaja mafanikio ya Kikwete ni udini?

Roho zinawauma akitajwa Kikwete sijui kawakosea nini?

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
 
Kapewa taarifa 2013/14 hadi kaondoka madarakani hajafanya chochote na tatizo bado sugu, halafu wewe unaandika upupu hapa. Kweli wewe zuzu.

2014 tayari kumebaki mwaka mmoja tu ufanyike uchaguzi wa Rais mpya, Kikwete ni mtu wa mahesabu makali, akautumia mwaka huo kumtafuta mtu ambae atakuja shika hatamu na kuwashughulikia, kumbuka hilo.

Sasa mnalo.
 
Huo udini maana yake nini? Au kumtaja mafanikio ya Kikwete ni udini?

Roho zinawauma akitajwa Kikwete sijui kawakosea nini?

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?


Kuna watu inabidi uwazoee maana kwenye komenti yako sikuona sehemu ulipotaja dini, ila kusifia utawala wa kikwete alipaswa akosoe kile ulichosifia kwa hoja kama hakibaliani na hoja yako
 
Back
Top Bottom