Inapiga kwenye simu yako kwa kubip zaidi ya mara moja. Niliishtukia nikawapigia voda-100 (huduma kwa wateja) kuwaulizia kuhusu hii namba. majibu yamenishtua. watu wengi wamepiga kuulizia hii namba. Wengine wamedai wakiipiga baada ya kwabip haina majibu ila ukienda kuangalia balance yako unakuta ni zero na hela yote imekombwa. Nimewaulizza Vodacom wanachukua hatua gani na wamejibu bado wanafuatilia hii namba na watajulisha wateja kwa sms wakipata majibu. Najiuliza- hivi mapaka wateja walalamike ndo wachukue hatua. Je ikiwa na madhara hata kwa M Pesa account si tutalizwa wengi? Tafadhali chukua hatua. Ushauri wa Vodacom ni kuwa usipokee hiyo namba na wala usiipige wala kutuma mesage. Ipuuzie.