Acha uongo na unafiki wewe, mbona Makonda hawajamkamata. Hakuna cha ugaidi wala nini, wanataka kilio cha katiba mpya kife kwa sababu hii katiba ya ccm ndio roho yao.Hii issue ya Mbowe ni tofauti na huko ulikotolea mifano.
Issue hii pia sio ya kumlaumu Mama.
Hapa kuna kazi ya Majasusi wa Magharibi. Ndio maana wanakuambia hawana rafiki wa kudumu au adui wa kudumu. Wakati wa JPM walimuita Dikteta wakawa na akina Mbowe ilimradi JPM aondoke madarakani. Majasusi wao wakawa wanawapa mbinu akina Mbowe za nini wafanye ili wamuondoe JPM.
JPM alipofariki wakawa bega kwa bega na Mama na kuwageuka akina Mbowe. Majasusi wanamuambia Mama Mbinu ambazo akina Mbowe wanazitumia bila kujali wao Ndio waliwafundisha. LEO hii Mbowe Yuko korokoroni wao wamekaa kimya, hawaoni tena udikteta hapa nchini.
hutamsikia yule Barozi akitoa tamko tena, hutasikia matishio ya kukatiwa misaada tena; kwanini? kwasababu yote haya wanayafanya wao