Kivumishi Kielezi
JF-Expert Member
- Nov 1, 2019
- 1,028
- 2,448
Nawasalimu kwa jina la JMT!
Tangu Bi. Samia ashike hatamu ya kiti cha urais wa nchi, basi kumezuka mengi ya kushangaza, kusisimua na kufurahisha.
Sijui watu wanamuonaje Mama Samia?
Kila mtu sasa amegeuka kuwa mshauri wa Samia kuhusu maswala mbalimbali yahusuyo nchi!
Wengine wamegeuka kuwa washauri-nasaha, wengine washauri-koko. Basi ilimradi tu fujo na vurumai kutoka pande zote.
Kila mtu anataka kumuongoza na kumuelekeza Rais kwa kadiri ya matakwa yake binafsi.
Chadema wanalilia maandamano, wengine wanalilia sijui mabadiliko ya kitu gani! Kila mtu anataka lake!
Naamini kuna ajenda za kitaifa, dira ya nchi, sera, ilani, katiba ya nchi, vipaumbele na miongozo mbalimbali.
Tumuache mama huyu atimize wajibu wake kwa kadiri inavyompasa. Tusimuandame na kumzonga zonga.
Msifikiri ni mpole kiasi hicho, maana siku atakapoamua kutumia rungu lake ipasavyo, mtaparaganyika na kukimbia.
Tuache kumzonga zonga Rais! Tunaweza kumshauri lakini tusimzonge zonge!
Ramadhan Kareem!
Tangu Bi. Samia ashike hatamu ya kiti cha urais wa nchi, basi kumezuka mengi ya kushangaza, kusisimua na kufurahisha.
Sijui watu wanamuonaje Mama Samia?
Kila mtu sasa amegeuka kuwa mshauri wa Samia kuhusu maswala mbalimbali yahusuyo nchi!
Wengine wamegeuka kuwa washauri-nasaha, wengine washauri-koko. Basi ilimradi tu fujo na vurumai kutoka pande zote.
Kila mtu anataka kumuongoza na kumuelekeza Rais kwa kadiri ya matakwa yake binafsi.
Chadema wanalilia maandamano, wengine wanalilia sijui mabadiliko ya kitu gani! Kila mtu anataka lake!
Naamini kuna ajenda za kitaifa, dira ya nchi, sera, ilani, katiba ya nchi, vipaumbele na miongozo mbalimbali.
Tumuache mama huyu atimize wajibu wake kwa kadiri inavyompasa. Tusimuandame na kumzonga zonga.
Msifikiri ni mpole kiasi hicho, maana siku atakapoamua kutumia rungu lake ipasavyo, mtaparaganyika na kukimbia.
Tuache kumzonga zonga Rais! Tunaweza kumshauri lakini tusimzonge zonge!
Ramadhan Kareem!