Watu wote tusipenda uovu, tunaomkiri Mungu wa Kweli, tujitenge kabisa na uchaguzi huu uliojaa uovu, unaotumika kuwahalalisha waovu.
Hivi kuna mtu asiyejua ni nani anahusika na utekaji na mauji ya watu wanaokosoa maovu?
Kuna mtu asiyejua ni chama gani kinahusika na huu uovu wa kuteka, kuua, kupoteza na kubambikia watu kesi za uwongo?
Hivi kuna mtu asiyejua ni nani walitaka kumwua Fr. Dr. Kitima kwa sababu alikemea uporwaji wa bandari zetu?
Wewe unayeamini unamwabudu Mungu wa kweli, bila ya kujali dini au dhehebu lako, kweli hujui kuwa kuteka na kuua watu ni dhambi?
Wewe unayesema unamwabudu Mungu na kufuata mafundisho yake, ina maana hujui kuwa kumbambikia mtu kesi ya uwongo, kudhulumu haki za watu ni dhambi?
Hata kama wewe siyo mkatoliki, ina maana kweli hujui kuwa tendo lile la kutaka kumwua Fr. Kitima, ambaye kwa upendo wake kwa watu, aliamua kukemea uporwaji wa rasilimalu za nchi, ilikuwa ni uharamia na dhambi kubwa?
Hivi ina maana wewe unayesema unamwabudu Mungu wa kweli, hujui kuwa kuunga mkono uovu, kuwaunga mkono waovu, kuhalalisha uovu, ni dhambi na chukizo mbele za Mungu?
Hata kama huna sauti ya kupaza, ni aheri ukae kimya, lakini jitenge mbali kabisa na michakato hii iliyojaa uovu mkubwa ambapo waovu wanataka wapate baraka zenu.
Ninyi hata mkibariki dhambi, mtambue Mungu kamwe hatabariki dhambi, nanyi nyote mliobariki dhambi mtaibeba laana ya hao wanaoteka na kuua watu kwa sababu tu wamekemea uovu wao.
Mungu ni mwingi wa huruma na tajiri wa msamaha. Enyi waovu geuzeni mienendo yenu, mtubu na kumrudia Mungu. Shetani mnayemtegemea kamwe hatawapa ushindi wa kudumu, bali atawafanyia hadaa ya muda mfupi ili apate kuwapoteza.
Hii ni sauti yenye dhamira njema iliojaa upendo kwa wanadamu wote.
Hivi kuna mtu asiyejua ni nani anahusika na utekaji na mauji ya watu wanaokosoa maovu?
Kuna mtu asiyejua ni chama gani kinahusika na huu uovu wa kuteka, kuua, kupoteza na kubambikia watu kesi za uwongo?
Hivi kuna mtu asiyejua ni nani walitaka kumwua Fr. Dr. Kitima kwa sababu alikemea uporwaji wa bandari zetu?
Wewe unayeamini unamwabudu Mungu wa kweli, bila ya kujali dini au dhehebu lako, kweli hujui kuwa kuteka na kuua watu ni dhambi?
Wewe unayesema unamwabudu Mungu na kufuata mafundisho yake, ina maana hujui kuwa kumbambikia mtu kesi ya uwongo, kudhulumu haki za watu ni dhambi?
Hata kama wewe siyo mkatoliki, ina maana kweli hujui kuwa tendo lile la kutaka kumwua Fr. Kitima, ambaye kwa upendo wake kwa watu, aliamua kukemea uporwaji wa rasilimalu za nchi, ilikuwa ni uharamia na dhambi kubwa?
Hivi ina maana wewe unayesema unamwabudu Mungu wa kweli, hujui kuwa kuunga mkono uovu, kuwaunga mkono waovu, kuhalalisha uovu, ni dhambi na chukizo mbele za Mungu?
Hata kama huna sauti ya kupaza, ni aheri ukae kimya, lakini jitenge mbali kabisa na michakato hii iliyojaa uovu mkubwa ambapo waovu wanataka wapate baraka zenu.
Ninyi hata mkibariki dhambi, mtambue Mungu kamwe hatabariki dhambi, nanyi nyote mliobariki dhambi mtaibeba laana ya hao wanaoteka na kuua watu kwa sababu tu wamekemea uovu wao.
Mungu ni mwingi wa huruma na tajiri wa msamaha. Enyi waovu geuzeni mienendo yenu, mtubu na kumrudia Mungu. Shetani mnayemtegemea kamwe hatawapa ushindi wa kudumu, bali atawafanyia hadaa ya muda mfupi ili apate kuwapoteza.
Hii ni sauti yenye dhamira njema iliojaa upendo kwa wanadamu wote.