ibesa mau
JF-Expert Member
- Sep 17, 2015
- 2,109
- 1,705
Nimeamua kuwapa onyo watu wa mikoani baada ya kuona kwa mda mrefu watu wa mikoani wanatapeliwa sana na jamaa zao au ndugu zao waishio dar-es- salaam.
Ninayo mifano mingi lakini leo nitaeleza mitatu tu. Kuna jamaa yangu wa kwanza alikuwa anataka gari akaenda Dar kwa ndugu yake ili akanunue lakini jamaa yake akamtafutia gari la milioni kumi na gari hilo lilisafiri hadi kufika nyumbani kwake ( mkoani) na kufa moja kwa moja.
Lakini mfano wa pili mnamo miezi kama minne iliyopita jamaa mwingine tena alienda dar kununua gari na alipofika kwa mwenyeji wake akamwambia anahitaji gari la milioni kumi na sita, jamaa akamwambia atamsaidia kupata gari nzuri matokeo yake ela amechukua amempiga kalenda jamaa amerudi bila gari na analalamika ametapeliwa na jamaa yake.
Na tatu niliitwa na rafiki yangu akiniomba kwenda kusuruhisha mgogoro na mke wake akidai kwamba walikopa fedha benki ili anunue gari na akaenda Dar kununua gari. Cha ajabu amerudi bila gari na fedha yote milioni 22 ametapeliwa na rafiki yake ambaye aliahidi kumsaidia kupata Harrier nzuri na mpaka anaondoka rafiki yake ameondoka nyumbani na kwenye simu hapatikani, akimuuliza mke wake mume wako yupo wapi anasema hajui wakati usiku wanapigiana simu na wanawasiliana.
Kwa kuwa jamaa alimwachia mke na nyumba alichoamua baada ya kugundua rafiki yake amekimbia na fedha zake ni kumgegeda mke wa rafiki yake siku nne na kuamua kurudi kwake mkoani huku akiumia makato ya deni kwenye mshahara kwa miaka mitano mbele.
Hivi nyie watu wa Dar watu wa mikoani mnawaonaje? Yaani nyie kila kitu dili, mtu unavunja undugu kwa ajili ya fedha. Acheni hizo bwana sisi tunatafuta fedha kwa shida, watu wanalima mwaka mzima halafu kipato chote unamwibia.
Ndio maana mimi mtu wa Dar huwa simwamini hata kidogo hata awe mkwe.
Ninayo mifano mingi lakini leo nitaeleza mitatu tu. Kuna jamaa yangu wa kwanza alikuwa anataka gari akaenda Dar kwa ndugu yake ili akanunue lakini jamaa yake akamtafutia gari la milioni kumi na gari hilo lilisafiri hadi kufika nyumbani kwake ( mkoani) na kufa moja kwa moja.
Lakini mfano wa pili mnamo miezi kama minne iliyopita jamaa mwingine tena alienda dar kununua gari na alipofika kwa mwenyeji wake akamwambia anahitaji gari la milioni kumi na sita, jamaa akamwambia atamsaidia kupata gari nzuri matokeo yake ela amechukua amempiga kalenda jamaa amerudi bila gari na analalamika ametapeliwa na jamaa yake.
Na tatu niliitwa na rafiki yangu akiniomba kwenda kusuruhisha mgogoro na mke wake akidai kwamba walikopa fedha benki ili anunue gari na akaenda Dar kununua gari. Cha ajabu amerudi bila gari na fedha yote milioni 22 ametapeliwa na rafiki yake ambaye aliahidi kumsaidia kupata Harrier nzuri na mpaka anaondoka rafiki yake ameondoka nyumbani na kwenye simu hapatikani, akimuuliza mke wake mume wako yupo wapi anasema hajui wakati usiku wanapigiana simu na wanawasiliana.
Kwa kuwa jamaa alimwachia mke na nyumba alichoamua baada ya kugundua rafiki yake amekimbia na fedha zake ni kumgegeda mke wa rafiki yake siku nne na kuamua kurudi kwake mkoani huku akiumia makato ya deni kwenye mshahara kwa miaka mitano mbele.
Hivi nyie watu wa Dar watu wa mikoani mnawaonaje? Yaani nyie kila kitu dili, mtu unavunja undugu kwa ajili ya fedha. Acheni hizo bwana sisi tunatafuta fedha kwa shida, watu wanalima mwaka mzima halafu kipato chote unamwibia.
Ndio maana mimi mtu wa Dar huwa simwamini hata kidogo hata awe mkwe.