Watu wengi wa Dar wamekaa kidili dili tu

Watu wengi wa Dar wamekaa kidili dili tu

ibesa mau

JF-Expert Member
Joined
Sep 17, 2015
Posts
2,109
Reaction score
1,705
Nimeamua kuwapa onyo watu wa mikoani baada ya kuona kwa mda mrefu watu wa mikoani wanatapeliwa sana na jamaa zao au ndugu zao waishio dar-es- salaam.

Ninayo mifano mingi lakini leo nitaeleza mitatu tu. Kuna jamaa yangu wa kwanza alikuwa anataka gari akaenda Dar kwa ndugu yake ili akanunue lakini jamaa yake akamtafutia gari la milioni kumi na gari hilo lilisafiri hadi kufika nyumbani kwake ( mkoani) na kufa moja kwa moja.

Lakini mfano wa pili mnamo miezi kama minne iliyopita jamaa mwingine tena alienda dar kununua gari na alipofika kwa mwenyeji wake akamwambia anahitaji gari la milioni kumi na sita, jamaa akamwambia atamsaidia kupata gari nzuri matokeo yake ela amechukua amempiga kalenda jamaa amerudi bila gari na analalamika ametapeliwa na jamaa yake.

Na tatu niliitwa na rafiki yangu akiniomba kwenda kusuruhisha mgogoro na mke wake akidai kwamba walikopa fedha benki ili anunue gari na akaenda Dar kununua gari. Cha ajabu amerudi bila gari na fedha yote milioni 22 ametapeliwa na rafiki yake ambaye aliahidi kumsaidia kupata Harrier nzuri na mpaka anaondoka rafiki yake ameondoka nyumbani na kwenye simu hapatikani, akimuuliza mke wake mume wako yupo wapi anasema hajui wakati usiku wanapigiana simu na wanawasiliana.

Kwa kuwa jamaa alimwachia mke na nyumba alichoamua baada ya kugundua rafiki yake amekimbia na fedha zake ni kumgegeda mke wa rafiki yake siku nne na kuamua kurudi kwake mkoani huku akiumia makato ya deni kwenye mshahara kwa miaka mitano mbele.

Hivi nyie watu wa Dar watu wa mikoani mnawaonaje? Yaani nyie kila kitu dili, mtu unavunja undugu kwa ajili ya fedha. Acheni hizo bwana sisi tunatafuta fedha kwa shida, watu wanalima mwaka mzima halafu kipato chote unamwibia.

Ndio maana mimi mtu wa Dar huwa simwamini hata kidogo hata awe mkwe.
 
Ukitaka kujua uzuri au ubaya wa mtu jaribu kumkabidhi pesa
 
Hii ndo Dar es salaam bana hili jua linapochoma ubongo ndo athari inapotokea mtu hajui kutofautisha huyu rafiki, jamaa, ndugu, mzazi wote anachanganya spana za utu zimepigwa na jua mpaka zimekatika..
 
Kwanza usikariri maisha, halafu hapa town ulitaka watu waishi vp na kazi hawana
 
Dar ni kweli kabisa watu wanaishi kiujanja ujanja tu.

Na pia waongo sana watu wa dar maneno mengi sana.
 
Kuna rafiki yangu alikuwa anaishi uku atwn akaja pata kaz uko dar lakin sasa ivi simwamin kabisa.


Hakiwa uku atwn alikuwa mkweli sana ukimkopesha atarudisha tu.

Lakin toka aingie jiji la dar namdai kama 4m ivi kila wakati ni ananipiga kiswahili ni mwaka sasa unepita nimeamua tu nimwachie simdai tena.

Pia hata ukaribu umepungua kabisa,unakuta anaulizia marafiki wangu wa atwn kama nipo aten au nje ya nchi.

Lakin before nikisafir lazima nimletee zawadi kama rafiki wa karibu sana.
 
Wanawaona mafal.a.....Wewe utampaje mtu hela kirahisirahisi??!!! Hata nduguyo lazima uwe na tahadhari. Halafu watu kibao wako mikoani tunafanya nao biashara hatujuani hata sura, na jana kuna mtu wa mkoa fulani kwa mara ya kwanza ndio kaniona na kufika ofisini kwangu na nimefanya nae biashara za hela nyingi karibu miaka miwili sasa na kuna wengine wengi tu hata hatujawahi kuonana.

Kwahio futa hio kauli yako...SIO WATU WOTE,wewe umekutana na rafiki/ndugu zako/zenu matapeli na kwa ufa.la wako/wenu wamekunyoosha!!!

mkuu kama hayo uyasemayo ni kweli na yanatoka moyoni Mungu akubariki sana na uendelee na tabia hiyo. Ila uwe unawashauri na wenzako wa dar waache utapeli waige tabia yako ya uaminifu.
 
Mkapa aliposema wa Tanzania ni malofa alikua anamaanisha watu wa mikoani na si wa daslam.
 
hamna aisee mbona tupo wengine waaminifu kama mimi sijawai kumtapeli mtu kama yupo aseme hapa
 
Hahahahah hapo eti alimgegeda mke jamaa take kufidia mshiko wake daah .


Sasa taste ya mgegedo imeweza kuyeyusha machungu ya pesa aliyotapeliwa
 
Pata pesa tujue tabia yako...Mjin hapa watu wanaishi kwa akili...Bongo Dar es salaam Utapeli kitu cha kawaida sana
 
Back
Top Bottom