Watu wazima, tuachane na mambo ya kitoto kwenye digital platforms

Watu wazima, tuachane na mambo ya kitoto kwenye digital platforms

NDUKI

JF-Expert Member
Joined
Jan 19, 2013
Posts
3,440
Reaction score
2,450
Unajua bwana...!

Kila jambo lina muda wake na kila jambo lina wakati wake. Unaweza ukajiuliza wakati ni nini na muda ni nini, natumai unaweza ukajijibu mwenyewe, ila kama utashindwa kujijibu itabidi ujiulize mara mbili kuweza kupata JIBU sahihi, unaweza ukapata JIBU lakini lisiwe JIBU sahihi.

Kuna mambo tulikuwa tunakutana nayo pindi tukiwa wadogo mpaka hapo ulipofikia. Mengine tunaendelea nayo mengine tunaachana nayo au hata tusipoachana nayo ila tunatakiwa kuachana nayo, tunaachana nayo kivipi...? Mi sijui. Kila mtu anatumia njia yake ya kuachana nayo, kiufupi njia huwa zinatofautiana.

Kwa mfano, wakati tunakuwa tulikutana na mchezo kama goroli, kidali poo, kucheza mpira, video games n.k. Ila kuna mengine tumeachana nayo na wengine bado wanaendelea nayo, SAWA.

Ila kwa watu wazima ambao wamekutana na hizi Digital Platforms, trendings etc 'UKUBWANI' ; sio kila Digital Platform au Trending lazma nawe U-Trend, HAPANA. Kuna mambo ya 'MSINGI' na mengine sio ya 'MSINGI' kuweza kuweka kwenye Digital Platforms. Ku-trend au kuwepo kwenye Digital Platforms sio kitu kibaya, ila ubaya unakuja kwenye 'KUANIKA' Maisha yetu binafsi, hii sio njia 'SAHIHI' ya Ku-Trend, Coz kuna watu wengi tu wana-trend, lakini huwezi kukuta popote wameweka maisha yao binafsi kwenye Digital Platforms. Kuna watu kama Maxence Mello, Millard Ayo et al, wapo On Trending bila ya kujiharibia 'REPUTATIONS' zao kisa 'TRENDING', yote hii ni kwa sababu wamejua kwenda na 'UPEPO', Kwenda na 'UPEPO' sio kufanya au ku-deal na kila kitu kwenye Digital Platforms. Mwisho wa siku mtu unajikuta unaua 'BRAND' yako au unaua mpaka Biashara za watu waliokupa 'DEALS' za matangazo, lakini pia unajiua na wewe mwenyewe coz watu watakosa 'UAMINIFU' wa kujitoa kwako na kukupa KAZI zao kwa niaba ya...!. Lakini pia hata wale waliokwishakupa 'KAZI' zao itafanya uwapunguzie wateja kwa sababu ya kuchafua jina lako kutokana tu, na kutaka 'KU-TREND'.

Ni aibu sana kama 'MTU MZIMA' kuaibishwa na vitu ambavyo sio vya msingi na kuacha vitu vya msingi vikikutazama. Nini tufanye kama watu wazima...?.

Tuachane na mambo ya 'KISASA' sio 'GARI' wala 'NYUMBA'. Sio 'TRENDING' wala sio 'NINI', tujaribu sana 'KU-FOCUS' kwenye Maisha yetu na kipi tunachotakiwa kukifanya kama watu wazima.

Ya watoto tuwaachie watoto. Kikubwa tuwasilishe tulichonacho kama wakubwa ili watoto wachukue kutoka kwetu kama 'WAKUBWA'. Tunawafunza nini watoto/wadogo zetu...?

Mitandao tuitumie vizuri kama watu wazima, kuna mambo mengi tu ya kufanya kwenye Mitandao na Digital Platforms. Sio mambo yasiyo na msingi wakuu.

YA MUNGU TUMPE MUNGU. YA KAIZARI TUMUACHIE KAIZARI.

YA NGOSWE TUMUACHIE NGOSWE.

NIWATAKIE MAISHA MEMA WAKUU.

AHSANTENI.
 
Mkuu umenena kiutu uzima. Unaweza ukakuta Mzee wa miaka 55 anapost vitu vya ajabu hadi aibu wanaona watu wengine, hebu assume mtu kama Mamndenyi anapost vitu vya ajabu ili apate tu kutrend, hakika utaona aibu kwa niaba yake.
Hakika kiongozi kuna vitu vingine yabidi tu kuviacha ili kulinda heshima zetu na familia zetu kwa jumla, sio kila kitu ni cha kuweka kwenye Digital Platforms vingine ni vya kuacha kwa sababu sio vitu vya msingi mkuu.
 
Naona mnasema manara
Hapana sio manara wako wengi sana wenye hiyo tabia.
Tena afadhali manara yeye kwa nature ya kazi zake ananufaika zaidi akijianika mitandaoni kuliko watu wengine wanajianika kwa show off tu za kijinga na hawanufaiki na chochote
 
Hakika kiongozi kuna vitu vingine yabidi tu kuviacha ili kulinda heshima zetu na familia zetu kwa jumla, sio kila kitu ni cha kuweka kwenye Digital Platforms vingine ni vya kuacha kwa sababu sio vitu vya msingi mkuu.
Yap, mkuu watu wazima wengine wanaharibu sana wanafanya watoto wa 2000 wasiwape heshima wanayostahili
 
Hapana sio manara wako wengi sana wenye hiyo tabia.
Tena afadhali manara yeye kwa nature ya kazi zake ananufaika zaidi akijianika mitandaoni kuliko watu wengine wanajianika kwa show off tu za kijinga na hawanufaiki na chochote
Real talk my brother...!
 
Yap, mkuu watu wazima wengine wanaharibu sana wanafanya watoto wa 2000 wasiwape heshima wanayostahili
Kabisa kiongozi ambapo sio sawa, hawa watoto tunawaita wa 2000 unaweza ukakuta kwa asilimia fulani hao watu wazima wamechangia kwa njia Moja au nyingine hao watoto kuwa hivyo.

Kama wanaona wakubwa zao wanafanya mambo ya hovyo unadhani vya kurithi itakuaje...? Vinazidi mkuu. Watu wabadilike wasiende na 'UPEPO' mwishowe wakapelekwa na 'UPEPO'.
 
Kabisa kiongozi ambapo sio sawa, hawa watoto tunawaita wa 2000 unaweza ukakuta kwa asilimia fulani hao watu wazima wamechangia kwa njia Moja au nyingine hao watoto kuwa hivyo.

Kama wanaona wakubwa zao wanafanya mambo ya hovyo unadhani vya kurithi itakuaje...? Vinazidi mkuu. Watu wabadilike wasiende na 'UPEPO' mwishowe wakapelekwa na 'UPEPO'.
Mtu mwenye umri mkubwa anaweza kuwashawishi watoto wa 2000 kwa aurahisi.

Watoto wetu wanaangamia mkuu.
 
Mtu mwenye umri mkubwa anaweza kuwashawishi watoto wa 2000 kwa aurahisi.

Watoto wetu wanaangamia mkuu.
Ni shida sana kiongozi kuna pahala tulikosea kama wakubwa na kuja kurekebisha itatugharimu kwa muda mrefu sana mkuu.
 
Kuna memba anajiita jr humu.sikuhizi anamambo yakitoto hadi namhurumia
Ukim-challenge kdg tuu anazira anakuweka kwenye ignore list au hakujibu kitu 😂 ana wafuasi wengi humu amewashika vichwa hvy ukimpa changamoto na wafuasi wake nao wanakuchukia, kumbe wote hawana akili.

Na sio mwingine bali ni Mbaga Jr 😂
 
Back
Top Bottom