Watu wangu wanaangamia kwa kukosa Maarifa

Watu wangu wanaangamia kwa kukosa Maarifa

badison

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2015
Posts
1,449
Reaction score
2,818
Utulivu ni muhimu kwenye nafsi zenu wote.

Husika na kichwa cha habari hapo juu. Wajuzi wa mambo wanasema ukweli unashangaza sana kuliko uhalisia wa mambo. Asilimia 100% ya vitu vinavyo tuzunguka na kuviona, kula pamoja na kuvisikia sio kweli ni uongo mtupu na vingine haviliwi.

Toka mtu anazaliwa mpaka anakufa kama hakuweza kuwa mtawazwa wa kikundi flani cha elimu ya siri atakufa ilihali amepoteza muda wake hapa duniani bila kujifunza kitu chochote cha kumsaidia nguvu pale atakapo fungua mlango wa pili kwani knowledge is power.

Lengo la ujinga huu ninao andika sio kumfungua mwerevu akili bali kuwa funzo kwa wachache wenye kufikiri. Kwani werevu ni watu wabishi sana na mimi sina muda wa kubishana na mtu mwerevu ajuae kila kitu.

Maisha yetu yote toka tumezaliwa tumekuta watu wanakula nyama ya mbuzi, ng’ombe, kondoo, nguruwe nk pia tumekuta watu wanafuga paka, mbwa na kadhalika.

Maisha yetu toka tumezaliwa tumekuta watu wanakula mahindi(ugali), wali, ngano, viazi ulaya nk

Nataka leo nikupe siri kuwa hao wanyama wote hapo ni wanyama wasioliwa na hawana nafsi (spirit) kwa kuweza msisitizo hao wanyama ni hybrids hawajaumbwa na mungu bali ni genetics manipulation au kucheza na vinasaba.

Kama mnavyojua toka umezaliwa hujawahi kuona paka anaishi kwenye mbuga yoyote mda wote anazunguka kwenye makazi ya wanadamu.

Toka unezaliwa hujawahi kuona wala kusikia ngo’mbe wanapatikana msitu wowote duniani au hukawahi kuona wawindaji wanaenda kuwinda ngo’ombe porini. Muda wote mnyama huyu yupo katika makazi ya watu.

Toka umezaliwa hujawahi kuona nguruwe (pink hybrids) ambao ni genetic manipulation ya wild boars wanapatikana kwenye msitu wowote. Utawakuta wapo tu kwenye mazingira ya watu hata huwezi kuona katoroka anarudi msituni kama wafanyavyo ngiri au mnyama youote wa asili aliye umbwa na Mungu.

Toka umezaliwa hata uende msitu wowote iwe serengeti amazoni au misitu ya congo huwezi kukuta hao wanyama niliokutajia hapo kwani sio product ya nature.

Hayo maviumbe watu wanayokula yalitengenezwa na aliens kwa lengo lakuzima 3rd eye ya mwanadamu na kumuondoa nguvu zake za asili.

Jiulize ukienda msitu wowote duniani utakuta swala simba mbwa mwitu nyani tumbili hata ukiwachukua na kuwapeleka zoo ya maonyesho ya wanyama hupenda kutoroka na kurudi porini kwani ndio asili yao je ulishaona wanyama kama mbwa ngombe mbuzi kondoo na nguruwe wanatoroka na kurudi porini? Au wanapenda kuishi katika mazingira ya watu.?

Kwanini watawala wa dunia hawataki watu wale nyama pori? Sababu ni moja ukila nyama pori utafanya kitu kinaitwa DNA activation jiulize watu matajiri wanatoka ulaya na uarabuni kuwinda wanyama huku kwanini?

Mchele, ngano mahindi na mazao mengi yaliletwa kwetu na wazungu pamoja na wareno sisi tulikiwa hatuli ugali kwasababu unadumaza akili ndo mana wao ugali ( steep porridge) ni chakula cha nguruwe. Kama kuna mtu anaushahidi haya mazao hayakuletwa na wazungu aweke hapa. Azibitishe kuwa yalikuwepo kabla ya wazungu kuja.

Wale wanyama pori ndo Mungu ametuwekea tule kama chakula, pamoja na asali ya nyuki na mizizi viazi vitamu mihogo na matunda pamoja na samaki. Ukila chakula hiki utaweza kufungua DNA yako. Lakini ukila hayo mambuzi kondoo na ngombe jua unazimaliza nguvu zako pamoja na kuoata magonjwa kama gauti na kuwa na akili za kingo’mbe. Usidhani watu waliosema mtu ana sura ya mbuzi wanatania. Ni kweli Mbuzi ni mnyama aliyetokana na DNA ya binadamu ndo mana ana ndevu ( chunguza sana picha ya mbuzi) na kwanini mbuzi anahusishwa na devil au shetani?

Usifuge paka au mbwa nyumbani kwako ni hatari sana viumbe hawa ni spy au majasusi. Kama unafuga wafukuze au wauwe.

Viumbe hawa ndo wanasifika kwamba wanauwezo wa kuona wachawi. Hiyo ni kwa sababu hivi viumbe havina nafsi na mchawi ni mtu aliyeuza nafsi hivo ni rahisi sana kiumbe cha nguvu za giza kumuingia paka au mmbwa bila wewe kujua na kukuchunguza maisha yako yote kama kamera.

Huwezi kumuona mchawi kama wewe sio mmoja wao ndo haya maviumbe mnayoweka nyumbani kwenu na kuyapa chakula cha bure. Mbwa ni viumbe rahisi sana utiifu wao upo kwa mtu anaye wapa chakula tu na kama usipo mpa chakula atakugeuka.

Nataka niandike vitu vingi lakini nimechoka. Kwani unaweza kuandika kitu cha kusaidia jamii mtu mwerevu akaona mbali na kujibu mitano tena ili kuficha elimu. Sifa kubwa ya watu wasiokuwa na akili iliyo komaa ni kupenda sana Mizaha.

Mwsho namalizia kwa kusema binadamu wa kweli na asili ni watu weusi kutoka Africa pamoja na bara la Australia ukijumlisha na red Indias waliokuwa wanaishi North America. Wazungu sio product ya mungu ni hybrids na wanyama niliokutajia hapo ni kwaajili ya wazungu ndo mana wanapenda Ma mbwa kiasi wanalala nayo na paka akiwamo.

Sitaweza kujibu kila maoni ya mtu soma alafu achana nayo sikukazimishi ukiamini nilichoandika. Fanya yako.

Badi.
 
Mie navuta bangi.
Nakula mihogo
Nakula njiwa na dege wadogo wadogo.
Nakula majani ya aina nyingi sanaaa.
Kunde, mahind kidogooo, ndizi za kupika,
Nyama za porini nazo najitahid japo sio sana.

Vip mleta mada, yawezekana ndio siri ya Hekima zangu nyingi. 😂😂😂

Ila ulipoanza habari za uchawi, HAPO NDO UMETUDANGANYA TU, wafuga paka na mbwa unawaonea. 😥
 
Mie navuta bangi.
Nakula mhoga za majani.
Nakula njiwa na dege wadogo wadogo.
Nakula majani ya aina nyingi sanaaa.
Kunde, mahind kidogooo, ndizi za kupika,
Nyama za porini nazo najitahid japo sio sana.

Vip mleta mada, yawezekana ndio siti ya Hekima zangu nyingi.

Ila ulipoanza habari za uchawi, HAPO NDO UMETUDANGANYA TU, wafuga paka na mbwa unawaonea.

Hapana sijadanganya mkuu. hao wanyama ni hatari sana macho yao yanaona mbali
 
Hapana sijadanganya mkuu. hao wanyama ni hatari sana macho yao yanaona mbali
Sindio fresh sasa.
Kuna sauti mbwa akibweka, najua tu kuna wachawi wanajipitisha kwangu.

Na Jibwa la kichawi mbwa wa kawaida huwa wanamuogopa vibaya sana.

Sasa huoni hiyo inakua msaada kwangu kutambua mambo kwa urahis.
WANADAMU TUMEPEWA KUTAWALA BWANAA
 
Sindio fresh sasa.
Kuna sauti mbwa akibweka, najua tu kuna wachawi wanajipitisha kwangu.

Na Jibwa la kichawi mbwa wa kawaida huwa wanamuogopa vibaya sana.

Sasa huoni hiyo inakua msaada kwangu kutambua mambo kwa urahis.
WANADAMU TUMEPEWA KUTAWALA BWANAA

Soma vizuri asili ya mnyama mbwa chanzo chake sio mungu. Ndio mana huwezi kwenda mwituni ukakuta mbwa. Je wametoka wapi asili yao?
 
Soma vizuri asili ya mnyama mbwa chanzo chake sio mungu. Ndio mana huwezi kwenda mwituni ukakuta mbwa. Je wametoka wapi asili yao?
Polini mbwa mbona wapo, tena wengi tu.
Tofauti tofauti.
Ila hasa misitu ya wenzetu kule.

Alafu kingine, Mungu aliumbwa wanyama wa mwituni na wakufuga.

Wakufuga hawezi patikana msituni, maisha ya huko hayawezi.
 
Polini mbwa mbona wapo, tena wengi tu.
Tofauti tofauti.
Ila hasa misitu ya wenzetu kule.

Alafu kingine, Mungu aliumbwa wanyama wa mwituni na wakufuga.

Wakufuga hawezi patikana msituni, maisha ya huko hayawezi.

Mbwa waliopo porini ni wakali sana kiasi kwamba hawawezi kuishi na binadamu mfano ni fox au mbwa mwitu.

Mbwa mwitu ndiyo mnyama wa asili hawa wa nyumbani DNA zao ni hybrids. Ukitaka mbwa kama buldog utaenda msitu gani kumpata ? cha zaidi utaambiwa tafuta mbegu hizo mbegu ndo DNA manipulation
 
Hii mada kama haujala chakula unaweza pata ulcers aisee

Nambi niulize kidogo na sio kwamba nataka kutofautiana na wewe ila naamini a good theory must have critics

1. Kuna ushahidi wowote unaosema aliens walileta hawa wanyama?

2. Story za paka kuhusishwa na mambo ya kichawi ama kishirikina zipo sana ya mwisho niliona juzi wakati simba wanacheza na platinum... lakini pia kama ulishawahi ona movie ya The Mummy kuna sehemu lile lijini likakutana na paka likasepa faster.
Point yangu hapa ni kwamba sio kila paka ama mbwa anaweza tumika katika kufanya ushirikiana wengine huzuia.

3. Je kuna tofauti gani katika nutrients zinazopatikana kwenye nyama ya ng’ombe wa kufungwa na ng’ombe poli? Akiwa ng’ombe wakufugwa hajawahi pewa dawa ama chanjo ila amefugwa!

4. Aliens hawa wanahusishwa na mambo mengi sana katika dunia ya sasa. Naomba ufafanue kidogo wanamahusiano gani na ushirikina /uchawi/ ushetani.
 
Mbwa waliopo porini ni wakali sana kiasi kwamba hawawezi kuishi na binadamu mfano ni fox au mbwa mwitu.

Mbwa mwitu ndiyo mnyama wa asili hawa wa nyumbani DNA zao ni hybrids. Ukitaka mbwa kama buldog utaenda msitu gani kumpata ? cha zaidi utaambiwa tafuta mbegu hizo mbegu ndo DNA manipulation
Husomi neno la Mungu ndio maana hata unaogopa mchawi.
Mwanzo 1:24-25
24) Mungu akasema, Nchi na izae kiumbe hai kwa jinsi zake, mnyama wa kufugwa, nacho kitambaacho, na wanyama wa mwitu kwa jinsi zake; ikawa hivyo. 25) Mungu akafanya mnyama wa mwitu kwa jinsi zake, na mnyama wa kufugwa kwa jinsi zake, na kila kitu kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.

Wakufuga usilazimishe kumkuta msituni.
Hayawezi maisha ya uko.
Mungu alifanya wa kufuga toka kuanza kwa Adamu
 
Hii mada kama haujala chakula unaweza pata ulcers aisee

Nambi niulize kidogo na sio kwamba nataka kutofautiana na wewe ila naamini a good theory must have critics

1. Kuna ushahidi wowote unaosema aliens walileta hawa wanyama?

2. Story za paka kuhusishwa na mambo ya kichawi ama kishirikina zipo sana ya mwisho niliona juzi wakati simba wanacheza na platinum... lakini pia kama ulishawahi ona movie ya The Mummy kuna sehemu lile lijini likakutana na paka likasepa faster.
Point yangu hapa ni kwamba sio kila paka ama mbwa anaweza tumika katika kufanya ushirikiana wengine huzuia.

3. Je kuna tofauti gani katika nutrients zinazopatikana kwenye nyama ya ng’ombe wa kufungwa na ng’ombe poli? Akiwa ng’ombe wakufugwa hajawahi pewa dawa ama chanjo ila amefugwa!

4. Aliens hawa wanahusishwa na mambo mengi sana katika dunia ya sasa. Naomba ufafanue kidogo wanamahusiano gani na ushirikina /uchawi/ ushetani.

Swali zuri sana na pia Asante kwa kuelewa mada yangu. Ushahidi kuwa aliens wameleta hawa wanyama upo wazi sana. Wazungu sio watu wa asili wa dunia yetu ndio mana wako mbele sana kwenye upande wa teknolojia. Lengo la teknolojia ni kurahisisha maisha.

Kwa leo sitaweza kuelezea kwa undani sana kuhusiana na reptilian technology but nitakudhibitishia hayo kwa kupitia biblia fanya utafiti wa nabii nuhu na safina kwanini aliambiwa achague wanyama safi dume na jike katika kila mnyama. Aliambiwa hivo kwa sababu kuna aina ya wanyama ambao hawakuwa safi.

Kuhusiana na paka kuna kipindi walikuwa wanaabudiwa na wanadamu kama miungu wanaitwa Bastet Gods wakiaminiwa kama sio viumbe wa kawaida hapa duniani

Ngombe pamoja na kundi la wanyama wa nyumbani hawana nutrition ambazo zipo kwa wanyama pori kama umewahi kula swala utaweza kuona tofauti ya ladha na mionzi ( energy) baada ya kula.
 
Husomi neno la Mungu ndio maana hata unaogopa mchawi.
Mwanzo 1:24-25
24) Mungu akasema, Nchi na izae kiumbe hai kwa jinsi zake, mnyama wa kufugwa, nacho kitambaacho, na wanyama wa mwitu kwa jinsi zake; ikawa hivyo. 25) Mungu akafanya mnyama wa mwitu kwa jinsi zake, na mnyama wa kufugwa kwa jinsi zake, na kila kitu kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.

Wakufuga usilazimishe kumkuta msituni.
Hayawezi maisha ya uko.
Mungu alifanya wa kufuga toka kuanza kwa Adamu

Hapana siogopi uchawi ila naheshimu mipaka iliyowekwa kati yetu binadamu wa kawaida na hao wachawi. Kuna sheria za ulimwengu za kuwaongoza wao na zipo za kutuongoza sisi wateule ( chosen ones) biblia sio absolute book sababu kuna vitabu ambavyo vinaelezea hayo niliyoandika hapo lakini viliondolewa . Soma the book of enoch utaelewa.

Kuhusiana na wanyama wa kufugwa kwanini tusifuge swala punda milia au pofu tujikute binadamu wote duniani tunafunga mbuzi na ngombe tuu hujiulizi Kwanini wao tu?
 
Umenena! Watu wenye maarifa "hasa ya ulimwengu wa roho " ndio waliotoboa hapa duniani. Hao wanaojua matumizi ya mbwa na paka katika ulimwengu wa roho huku wakipasua sala kwa unafiki. Wazungu "aliens " wamevamia hii duniani kutoka sayari za mbali za aliens, wana siri ya maendeleo. Angalia wanavyotupumbaza na dini. Eti funga macho usali!
 
Hapana siogopi uchawi ila naheshimu mipaka iliyowekwa kati yetu binadamu wa kawaida na hao wachawi. Kuna sheria za ulimwengu za kuwaongoza wao na zipo za kutuongoza sisi wateule ( chosen ones) biblia sio absolute book sababu kuna vitabu ambavyo vinaelezea hayo niliyoandika hapo lakini viliondolewa . Soma the book of enoch utaelewa.

Kuhusiana na wanyama wa kufugwa kwanini tusifuge swala punda milia au pofu tujikute binadamu wote duniani tunafunga mbuzi na ngombe tuu hujiulizi Kwanini wao tu?
Wewe jamaa unakichwa kigumu.

Nakwambia suruali ni suruali na shati ni shati.

Unashonewa shati unalazimisha kuivaa kama chupi?
 
Wewe jamaa unakichwa kigumu.

Nakwambia suruali ni suruali na shati ni shati.

Unashonewa shati unalazimisha kuivaa kama chupi?

Mkuu sijakataa ulichokiandika sema unatakiwa ujue kuwa kuna viumbe tofauti na mungu pia ambavyo vina uwezo wa kutengeneza wanyama dume na jike na kuchafua uumbaji. Soma vizuri hoja yangu kisha soma hadithi ya nuhu na safina
 
Umenena! Watu wenye maarifa "hasa ya ulimwengu wa roho " ndio waliotoboa hapa duniani. Hao wanaojua matumizi ya mbwa na paka katika ulimwengu wa roho huku wakipasua sala kwa unafiki. Wazungu "aliens " wamevamia hii duniani kutoka sayari za mbali za aliens, wana siri ya maendeleo. Angalia wanavyotupumbaza na dini. Eti funga macho usali!
Kweli mzee hii duniania ilisha vamiwa ndio maana kuna vitu vingine watu wengine wanaweza kufanya halafu sisi hatuwezi.
 
point yako ni nini kwani? kwahyo nasisi tukaishi na simba huko porini maana kumbe sisi ni ndugu,......na simba analitambua hilo kuwa sisi ni ndugu hatoning'ata?......
 
point yako ni nini kwani? kwahyo nasisi tukaishi na simba huko porini maana kumbe sisi ni ndugu,......na simba analitambua hilo kuwa sisi ni ndugu hatoning'ata?......
Hujaelewa, soma vizuri point ya mtoa mada hapo juu, hajalenga unachokisema
 
Back
Top Bottom