Superbug
JF-Expert Member
- Jan 31, 2018
- 12,417
- 30,927
Serikali isijifanye inaziba masikio juu ya kwanini watu hawajiandikishi kupiga kura sababu Ni hizi
1.Kauli za rais
Kauli alizotoa mh rais kwamba ole wake mkurugenzi atakaemtangaza mpinzani wakati anamlipa mshahara anampa gari na walinzi ole wake hii inawafanya watanzania waone hakuna umuhimu maana matokeo yatatangazwa kibabe hata Kama si chaguo lao.
2.Kuunga mkono juhudi
Haya yalikuwa Ni maigizo ya kimbumbumbu Sana yaliyochukiwa na watanzania na hakika hapa ndipo walipowadharau wanasiasa mtu anajiuliza niache kwenda shamba nikapange foleni kumchagua mtu ambae kesho atanisaliti kirahisirahisi kwasababu za kipumbavu za kuunga mkono juhudi za rais never.
3.Kuzuiwa mikutano halali ya kisiasa.
Kimsingi hili nalo limechangia Sana kwasababu Ni ukweli kabisa kwamba CCM haipendwi Tena Tanzania Sasa unapowazuia vyama vya upinzani wasikutane na watu wao unapunguza uzito unaoshamirisha siasa nchini watu wanataka kuwaona kina
Halima mdee
Tundu lisu
Freeman mbowe
Mch msigwa
Godbless lema
Joseph Mbilinyi
John mnyika
Joseph selasini
Ester matiko
Nk
Sasa unapowanyima Hawa watu freedom ya kwenda popote kufanya siasa kimsingi unauhujumu upinzani na siasa Safi za taifa unazihujumu
Kwa manufaa ya CCM ambayo watu hawaioni Tena Ni mkombozi ila Ni kikundi Cha madikteta.
4. Fujo
Siasa za Tanzania toka serikali ya awamu ya tano ishike madaraka zimenasibishwa na fujo na uvunjifu wa amani matukio ya kuuwawa wapinzani kama jaribio la kumuua tundu lisu na mauwaji ya akwilin akwilina yamewafanya watanzania kutokujiona salama Tena katika Mambo ya siasa.kiufupi watanzania wamegawanyika katika makundi mawili A. Wanaoipenda ccm wanajiona wako salama na wanalindwa na dola B.Wanaoipinga CCM wanajiona hawako salama na Ni victims wa uhalifu unaofanywa na dola. Taifa limegawanyika huo ndio ukweli.
5. Hofu
Kwasasa wananchi wamejawa na hofu kujihusisha na Mambo ya siasa hata Kama Yana tija kwao sababu ya hofu hiyo Ni hiyo namba nne hapo juu. (Fujo na vurugu) watanzania wamekata tamaa na siasa zao zilizonawiri enzi za JK wakibishana kwa hoja taifa lilichangamka punde nchi ikaingia gizani awamu ya tano.
Mwisho
Wanufaika wakubwa wa Hali hii Ni CCM watanzania wasidhani kususa kwao wanaikomoa CCM hapana CCM inafurahia hii Hali ya political Injustice wananufaika nayo // ngoja tuone mwisho wa haya yote Mungu ibariki Tanzania!!
1.Kauli za rais
Kauli alizotoa mh rais kwamba ole wake mkurugenzi atakaemtangaza mpinzani wakati anamlipa mshahara anampa gari na walinzi ole wake hii inawafanya watanzania waone hakuna umuhimu maana matokeo yatatangazwa kibabe hata Kama si chaguo lao.
2.Kuunga mkono juhudi
Haya yalikuwa Ni maigizo ya kimbumbumbu Sana yaliyochukiwa na watanzania na hakika hapa ndipo walipowadharau wanasiasa mtu anajiuliza niache kwenda shamba nikapange foleni kumchagua mtu ambae kesho atanisaliti kirahisirahisi kwasababu za kipumbavu za kuunga mkono juhudi za rais never.
3.Kuzuiwa mikutano halali ya kisiasa.
Kimsingi hili nalo limechangia Sana kwasababu Ni ukweli kabisa kwamba CCM haipendwi Tena Tanzania Sasa unapowazuia vyama vya upinzani wasikutane na watu wao unapunguza uzito unaoshamirisha siasa nchini watu wanataka kuwaona kina
Halima mdee
Tundu lisu
Freeman mbowe
Mch msigwa
Godbless lema
Joseph Mbilinyi
John mnyika
Joseph selasini
Ester matiko
Nk
Sasa unapowanyima Hawa watu freedom ya kwenda popote kufanya siasa kimsingi unauhujumu upinzani na siasa Safi za taifa unazihujumu
Kwa manufaa ya CCM ambayo watu hawaioni Tena Ni mkombozi ila Ni kikundi Cha madikteta.
4. Fujo
Siasa za Tanzania toka serikali ya awamu ya tano ishike madaraka zimenasibishwa na fujo na uvunjifu wa amani matukio ya kuuwawa wapinzani kama jaribio la kumuua tundu lisu na mauwaji ya akwilin akwilina yamewafanya watanzania kutokujiona salama Tena katika Mambo ya siasa.kiufupi watanzania wamegawanyika katika makundi mawili A. Wanaoipenda ccm wanajiona wako salama na wanalindwa na dola B.Wanaoipinga CCM wanajiona hawako salama na Ni victims wa uhalifu unaofanywa na dola. Taifa limegawanyika huo ndio ukweli.
5. Hofu
Kwasasa wananchi wamejawa na hofu kujihusisha na Mambo ya siasa hata Kama Yana tija kwao sababu ya hofu hiyo Ni hiyo namba nne hapo juu. (Fujo na vurugu) watanzania wamekata tamaa na siasa zao zilizonawiri enzi za JK wakibishana kwa hoja taifa lilichangamka punde nchi ikaingia gizani awamu ya tano.
Mwisho
Wanufaika wakubwa wa Hali hii Ni CCM watanzania wasidhani kususa kwao wanaikomoa CCM hapana CCM inafurahia hii Hali ya political Injustice wananufaika nayo // ngoja tuone mwisho wa haya yote Mungu ibariki Tanzania!!