Watu huwa tunakwama wapi linapokuja suala la ndoa?

Watu huwa tunakwama wapi linapokuja suala la ndoa?

gasgas

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2015
Posts
1,098
Reaction score
994
Habari za asubuhi.
Leo nimekaa nikawa natafakari watu huwa tunakwama wapi linapokuja suala la ndoa.

Utakuta watu wawili katika uchumba wanapendana sana, wanaweka pamoja mipango ya maisha ya ndoa na kuchukua hatua stahiki hadi kukamilisha hili agano.

Wanafunga ndoa, harusi kali inayofana vilivyo lakini wakiingia ndoani na kukaa miaka miwili, minne, tano unaanza kusikia visivyo.
Mara mmoja anampiga mwingine, mmoja amekuwa mlevi wa kupindukia, mmoja au wote wanachepuka n.k

Shida iko wapi wakubwa. Ni kwamba wanakuwa hawajui ndoa ni nini na huingia kichwa kichwa mwishowe kustaajabu yaliyomo ndani?

Kwa nini watu wanashindwa kuwa humble, kujishusha na kutengeneza ndoa impendezayo Mungu.
Kwa nini watu hawataki kuinvest effort and time kuimarisha haya mahusiano na wanaona rahisi zaidi kubomoa agano hili takatifu. Nini huwa kinatokea na kusababisha kukata tamaa?

N.B Mimi ni kijana wa kiume, mid 20's, bado sijaoa. Nilipanga nioe within 2 years sema nimesogeza mbele zaidi hadi niwe na uhakika na mtu na hatua nnayoenda kuchukua.

Eti, shida iko wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hao ni watu wawili waliolelewa kwenye mazingira tofauti(kwa maana ya familia zenye malezi tofauti) so kipindi cha uchumba kila mmoja hujitahidi kuonyesha tabia itakayompendeza mwenzie kwa kuficha makucha (tabia yake halisi). Hiyo tabia ya kuficha makucha hukoma pale kila mmoja atakapomzoea mwenzie na hatimaye kila mmoja kuonyesha tabia yake halisi na inapofikia hatua hiyo kila mmoja humuona mwenzie kumbe haikuwa chaguo sahihi na migogoro huanzia hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndoa haina tofauti na kushea matatizo yako na mtu mwenye matatizo yake sasa hapo inategemeana na mfanano wa matatizo yenu
 
Lkn pia kuna version nyingine wanaokuwa wapenzi wanapendana kuamua kuona, harusi kufana na kuishi kwa amani na upendo kwenye ndoa na ndiyo wengi, hao uliowataja ni wachache na ni kawaida katika maisha.
 
Ajali zinatokea Kila siku. Lakini haifanyi watu waache kuendesha magari.

Sio ndoa zote zina hizo changamoto.

Heshima , utu, upendo na Hekima ndio inahitajika kujenga misingi imara baina ya wanandoa.

Nakushauri fanya huo uhakika na uoe Mapema.

Ukishaianza 30s. Unakuwa ushakomaa na kuwa mbaba na upambane na majukumu.
 
Nakushauri usioe kabisa
Habari za asubuhi.
Leo nimekaa nikawa natafakari watu huwa tunakwama wapi linapokuja suala la ndoa.

Utakuta watu wawili katika uchumba wanapendana sana, wanaweka pamoja mipango ya maisha ya ndoa na kuchukua hatua stahiki hadi kukamilisha hili agano.

Wanafunga ndoa, harusi kali inayofana vilivyo lakini wakiingia ndoani na kukaa miaka miwili, minne, tano unaanza kusikia visivyo.
Mara mmoja anampiga mwingine, mmoja amekuwa mlevi wa kupindukia, mmoja au wote wanachepuka n.k

Shida iko wapi wakubwa. Ni kwamba wanakuwa hawajui ndoa ni nini na huingia kichwa kichwa mwishowe kustaajabu yaliyomo ndani?

Kwa nini watu wanashindwa kuwa humble, kujishusha na kutengeneza ndoa impendezayo Mungu.
Kwa nini watu hawataki kuinvest effort and time kuimarisha haya mahusiano na wanaona rahisi zaidi kubomoa agano hili takatifu. Nini huwa kinatokea na kusababisha kukata tamaa?

N.B Mimi ni kijana wa kiume, mid 20's, bado sijaoa. Nilipanga nioe within 2 years sema nimesogeza mbele zaidi hadi niwe na uhakika na mtu na hatua nnayoenda kuchukua.

Eti, shida iko wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuamka na mtu kila siku for the rest of your lives sio rahis. Ndugu tu wakikaa pamoja hawakosi kugombana sembuse mke na mume.

Give each other a space, have your own hobbies, saidianeni kazi and 'Talk'.
 
Lkn pia kuna version nyingine wanaokuwa wapenzi wanapendana kuamua kuona, harusi kufana na kuishi kwa amani na upendo kwenye ndoa na ndiyo wengi, hao uliowataja ni wachache na ni kawaida katika maisha.
Yeah lakini nikibase kwa experience especially ndugu wa karibu naona shida hiyo ipo kwa sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom