Kuna mdada tulisoma nae, tulifahamiana Ila hatukua karibu kivile.
Siku hiyo naona amenitext messenger ananisalimia Kisha akaniambia amenimiss sana alikua anaikubali personality yangu, nikashangaa kidogo kwa sababu yeye kitabia alikua ni introvet kwa hiyo sikuwahi waza kama angekua anatazama watu wengine wapoje.
Basi tukachat kidogo kisha tukabadilishana namba za simu, akanipigia tukazungumza habari ya maisha nikamwambia Mimi bado ramani hazisomi mjini.
Akashangaa na kujilaumu Kwa Nini alichelewa kunitafuta, akaniambia kwenye kampuni Yao (miongoni mwa kampuni kubwa zaidi za kutoa huduma na uzalishaji nchini) nafasi zinatokeaga Ila hazitangazwagi nje na kwakuwa yeye alishakua na wadhifa tayari basi niandae CV yangu nimtumie atashughulikia.
Kesho yake akanipigia tena kunikumbusha sasa kulikua na ishu imenikamata kwa wakati huo nikawa naona aibu kumsalimia hivi hivi bila kukamilisha alivyoniambia nimuandalie.
Zikapita wiki mbili, nikawa nimekamilisha nikamtumia, hajajibu.. nikarudi messenger msg hajibu, najaribu kupiga simu haipatikani nikahisi labda amesafiri nje ya nchi, whatApp msg zimeenda Ila hazisomwi, nikahisi amenifanyia kusudi kwa nini anidanganye, nikakasirika sana nikaanza kukumbuka jinsi watu walivyokua wanamsema anaringa (kisa hajichanganyi) nikaona sasa ndio ananionyesha maringo yenyewe basi siku nikawa namuhadithia rafiki yangu yaliyonikuta akasema doh, kumbe hukusikia... Mbona huyu mtu ameshazikwa wiki ya pili Sasa... Mmhh.. yaani siku tuliyoongea Mara ya mwisho au kesho take yaani maumivu niliyosikia kama nimepoteza ndugu yangu wa damu.Hadi leo hii nikimkubuka namuombea tuu, nawaza tuu kilimsukuma nini from no where akanitafuta na kuanza kuniongelesha hali ya kuwa yupo safarini.