Watoto wangu wananifilisi

Watoto wangu wananifilisi

Mimi nafikiri hao watoto hujawalea vizuri, haiwezekani kila kitu anachotaka mtoto unampatia...sometimes inatakiwa watoto wajue kua kuna wakati vitu wanavyotaka havipatikani..ila sasa hapo hao ukiwanyima imeshakua too late..ndivyo ulivyowalea..ukisitisha tu huduma kwa mara moja...utapata shida..
 
Nakasirishwa sana na hawa watoto, wa kwanza yupo form five, wa pili form two na watatu standard seven english medium. Yaani najitahidi sana kuwalipia ada na kweli naweza na nafrahi sababu ni vipanga kila nikangalia matokeo nafurahi sana.

Huyu wa form 5 ni dada ndie anaeongoza chati yani kila siku sababu zisizoisha wa pili ni dume yeye hanaga mambo mengi anataka pesa za kucheza games na mziki mkali akirudi, haka kadogo kakiume kanapenda hela za kula chipsi na mandazi, ni kweli walimu wameniambia kanajimwaga kweli.

Plz najitahidi wanangu wana malezi mema hawajawahi nikera ila wananipiga mzinga sana inafikia mahali nataman niwaambie live sipendi hio tabia ila nafsi inakuwa ngumu plz nipeni ushauri.

Yani wewe badala ya kuwajengea msingi wa kusaka Pesa na tabia ya kusave unawaelekeza kuwa 'PONDA MALI, KUFA KWAJA?' Utakachovuna ni mimba kwa wa kike na ujambazi au ushoga kwa huyo wa kiume.

Wazazi wengine wamezidi kudekeza watoto wao. Kuwapa Pesa si kuwapenda Bali ni kuwatengenezea Kilema cha kudumu. Wafundishe jinsi ya kuvua na si uwape Samaki!!
 
Mambo hayo umewazoesha wewe xo kuwa mvumilivu tu.
Na ole wako ufilisike watakuuza na nyumba yako.
 
Duh jitahidi kubadilika wajue si kila mtu anachotaka kinapatikana kirahisi hivyo, hata kama pesa ipo jua kuwaambia leo hapana hata wanune ni kwa faida ya mbeleni...

Namshukuru Mungu sababu nakumbuka hata trip fulani fulani mtu ulikuwa unatamani duka zima ila weee, huwa siisahau maneno unaambiwa chagua mbili tatu upendacho zaidi...mkienda kwingine hivyo hivyo...kwingine unaambiwa inatosheleza..kwingine unapewa namba akili hapo inafanya kazi ya kuamua maana hutakuwa na wa kumlalamikia hata unune vipi unalo... Na etc inasaidia sana kuendeleza kwa watoto mtu.
 
Nakasirishwa sana na hawa watoto, wa kwanza yupo form five, wa pili form two na watatu standard seven english medium. Yaani najitahidi sana kuwalipia ada na kweli naweza na nafrahi sababu ni vipanga kila nikangalia matokeo nafurahi sana.

Huyu wa form 5 ni dada ndie anaeongoza chati yani kila siku sababu zisizoisha wa pili ni dume yeye hanaga mambo mengi anataka pesa za kucheza games na mziki mkali akirudi, haka kadogo kakiume kanapenda hela za kula chipsi na mandazi, ni kweli walimu wameniambia kanajimwaga kweli.

Plz najitahidi wanangu wana malezi mema hawajawahi nikera ila wananipiga mzinga sana inafikia mahali nataman niwaambie live sipendi hio tabia ila nafsi inakuwa ngumu plz nipeni ushauri.
mtoto umleavo ndivo akuavo.hili ni tatizo letu wabongo hatuwezi kuwapa watoto wetu fact ya maisha jifunzeni kwa wenzetu jamani wako wazi sana kwa watoto wao.Maana siku umebanwa huna sijui ka kitaeleweka oho we jishaue kwa wanao .
 
Watoto wako wote wa kiume wapo kwenye earl balehe kati ya umri wa miaka 13-18.Katika umri huu kuna tabia wanakuwa nazo na zinatofautiana kati ya mtoto na mtoto au rika. Kipindi hiki Mzazi anapaswa akae na mwanae kumsikiliza na yeye Mzazi kumshauri. Kwa upande wako jitahidi kumpa huyo wa pesa vitu anavyopenda badala ya pesa pia mpe budget mwambie kila anachofanyia awe anandika pesa ikiisha mfanyie evaluation anayekula usimnyime kula mpunguzie mawanga mkazanie matunda mboga na protein. Control your boys hili baadae wasije wakakusumbua usiwaone huruma punguza kuwapa pesa.
 
Sasa unataka wampige nani mizinga?

Sijui wengine lakini mimi ikija kwa Kisura huwa nafanya kufuru.

Chochote atakacho anapata tu.

Ndo wajibu wangu huo na kamwe siwezi kulalamika.

Na furaha yake ndo faraja yangu.
Ngabu katika ubora wako

Angalia usijekosa nauli ya kurudi USA baby
 
Tena watoto wa umri wakianza kujua pesa kama miaka 8 au wengine 10 unaanza hata kuwa fungulia akaunti benki wanajua pocket money inabidi iende huko...kufunza..mzazi mwenyewe utafufahia ukiona inajaa...pesa ndogo baada ya miaka inakuwa tamu na watoto unawafundisha kujua kana kusevu na kutumiaje...esp kama wanataka kitu kikubwa unasema si una pesa haya hiyo atoe kiasi fulani ajinunulie... kuna hiki na kile

Mengine ni kufanya ya kusubiri siku ya kuzaliwa hata kama miezi 11 bado atasubiri tu, huku mtu ukikazania masomo wasomeeeeeee.... Na sikukuu kama krismasi santa awaletee majonjo wanayomuomba...inafundiaha subira...

Ila ya pesa hakuna kuna ya hiki na hiki ya hicho hakuna...wakilia weee watanyamaza, watanuna ila faida mbeleni kubwa na nzuri maishani mwao...ni kwendana na kufunza mengi...
 
Nakasirishwa sana na hawa watoto, wa kwanza yupo form five, wa pili form two na watatu standard seven english medium. Yaani najitahidi sana kuwalipia ada na kweli naweza na nafrahi sababu ni vipanga kila nikangalia matokeo nafurahi sana.

Huyu wa form 5 ni dada ndie anaeongoza chati yani kila siku sababu zisizoisha wa pili ni dume yeye hanaga mambo mengi anataka pesa za kucheza games na mziki mkali akirudi, haka kadogo kakiume kanapenda hela za kula chipsi na mandazi, ni kweli walimu wameniambia kanajimwaga kweli.

Plz najitahidi wanangu wana malezi mema hawajawahi nikera ila wananipiga mzinga sana inafikia mahali nataman niwaambie live sipendi hio tabia ila nafsi inakuwa ngumu plz nipeni ushauri.
Hayo sio malezi kama unavyodai. Unawaogopa wanao. Pole sana.
 
Ni sawa kuwahudumia watoto lakini sio sawa kuwaharibu. Wafundishe watoto wako ku-earn anything they desire. Yaani wekeaneni targets (afu hako kadume ka chips unaniogopesha. Kafundishe kula healthy bwana). Hata Kama wanafaulu sana Shule wasukume kuchukua extra lessons ama kufanya kazi za nyumbani Kama kusaidia familia. Waambie anaetaka play station 3 alime bustani, au afanye usafi nyumba nzima, apange kabati lake, or anything. Raising spoiled brats is suicidal
 
Ni sawa kuwahudumia watoto lakini sio sawa kuwaharibu. Wafundishe watoto wako ku-earn anything they desire. Yaani wekeaneni targets (afu hako kadume ka chips unaniogopesha. Kafundishe kula healthy bwana). Hata Kama wanafaulu sana Shule wasukume kuchukua extra lessons ama kufanya kazi za nyumbani Kama kusaidia familia. Waambie anaetaka play station 3 alime bustani, au afanye usafi nyumba nzima, apange kabati lake, or anything. Raising spoiled brats is suicidal
Hahaaa umenikumbusha mbali.....

Ingawa nilikulia mwanza mjini lakini nyumbani kulikuwa na eneo la wastani la ziada hivyo, mama alikuwa akitengeneza chochote kizuri lakini huli hadi ulime matuta ya bustani .tulikuwa tunaona kama game fulani zuri hivi lakini nilipokua ndipo nilikuja kuelewa ni nini walikuwa wakimaanisha....

Malezi ya kiafrika yalikuwa mazuri
 
Inaelekea wewe hukuwahi kuwa na tabia hizo na wala huna hizo tabia. Sasa wamezitoa wapi?
Kawapime DNA mzee, inawezekana si wako hao.
Ukienda kuwapima, neno langu litakuwa limetimia
 
Back
Top Bottom