nyumba kubwa
JF-Expert Member
- Oct 8, 2010
- 10,309
- 8,369
Nimekumbuka kisa kimoja. Kuna kijana ameoa mzungu. Mzungu yuko Ok sana ana kazi ya maana kweli kweli na ni dada kijana. Sasa huyo kijana alizaa na binti akiwa secondari. Kwa sasa jamaa anaishi nje ya nchi. Alimwahidi yule binti alozaa nae kuwa atamuoa akimaliza masomo yake but bahati mbaya au nzuri kijana kapata dada wa kidhungu kaoa. Sasa shughuli ni kwamba yule binti alozaa nae amegoma kata kata kumruhusu kijana amchukue mtoto aende kuishi nae majuu. Basi yule mke wa jamaa (mdhungu) kamwambia jamaa basi si neno tumwamishe mtoto akasome international school hapo hapo Tz. Binti bado kaweka ngumu anasema eti huyu mtoto atasoma hapa hapa kijijini saint kanumba kwani ndizo zilizomsomesha baba yake. Yani wamechanganyikiwa kwani kijana anaona life ya mwanae (tena wa kiume) inaharibika hivi hivi kwa ligi ya mamake kisa alitaka amuoe kamuacha kwenye mataa. Hata kumuona mtoto inawabidi waende shule kwani mama yake hataki na amesema atawarogelea mbali. Nilicheka sana mdhungu anaongelea kurogwa.
(mdhungu ni shoga yangu ndiye aliyenipa details si kijana)
(mdhungu ni shoga yangu ndiye aliyenipa details si kijana)
hapo kwenye kukomoana hapo,...mnh...Mwj1 pamoja na mapenzi yangu kwako, kina mama wengi wamejaaliwa hilo.
Kuna kina mama wachache waliojaaliwa mioyo ya huruma, mfanoi weye Mwj1 wangu, ...lol...(ulishaanza kununa ee?)