Watawala wa Tanzania wanatofautiana mbinu na kiasi lakini dhamira yao ni moja

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,520
41,034
Marais wote wa Tanzania, nyakati zote, wamefanana kwa jambo moja kubwa, KUDIDIMIZA NA KUUA DEMOKRASIA.

Wakati wa mkoloni, kulikuwa na vyama vingi vya kisiasa. Mwingereza, pamoja na kwamba alikuwa mkoloni, hakuwahi kufuta au kuzuia shughuli za vyama vya siasa. Ndiyo maana kulikuwa na chama cha TAA (Tanganyika African Association).

Baada ya kupata uhuru, tofauti na matarajio ya walio wengi kuwa uhuru na demokrasia vingeongezeka, Mwalimu Nyerere aliharamisha uwepo wa vyama vingine vyote vya siasa isipokuwa chama chake cha TANU.

Tuliendelea na mfumo wa chama kimoja mpaka mabeberu walipozidisha mbinyo dhidi ya nchi zote zisizoheshimu demokrasia, ikiwemo demokrasia ya vyama vingi.

Mwalimu akaelekeza kuanza kwa mfumo wa vyama vingi. Lakini, kiuhalisia ulikuwa ni mfumo wa vyama vingi bandia. Vikosi vya jeshi vikageuzwa kuwa matawi ya CCM, na wakuu wa vikosi wakawa ndio wenyeviti wa matawi ya CCM jeshini.

Taasisi za Elimu ya juu zikafanywa kuwa matawi ya CCM, na kila mahali pa kazi palilazimishwa kuanzishwa tawi la CCM. Chini ya mfumo huo, kitu chochote cha CCM pamoja na michango vikafanywa kuwa ni lazima kwa watu wote.

Hata kujiunga chuo kikuu ulitakiwa kuwa na kadi ya CCM.

Mrema alipogombea Urais kupitia NCCR, ndipo ilipojulikana kuwa hatukuwa na mfumo wa vyama vingi, bali ni kiinimacho cha kuwahadaa mabeberu.

Kwa kutumia makada wake waliopo Polisi, CCM iliwatandika virungu waliokuwa wanamshabikia Mrema, mpaka Mwalimu Nyerere akapiga kelele kukemea. Wakati huo Mwalimu akiwa amestaafu, na Mwinyi ndiye Rais.

Mkapa alipokuwa Rais, naye hakuiacha agenda kuu ya watawala ya kuhakikisha Tanzania hatuwi na demokrasia ya kweli. Wizi wa kura ikawa jambo la kawaida. Kule Zanzibar wananchi walipotaka kuandamana kupinga wizi wa kura za Hayati Maalim Seif, walikutana na risasi za moto, watu takribani 20 wakapoteza maisha.

Kikwete alipoingia akaja na staili ya kuuma na kupuliza. Kelele za kutaka katiba mpya zilipozidi, akaunda Tume, akatengeneza Bunge la katiba, lakini lengo siyo kupata katiba mpya, ilikuwa ni kufifisha jitihada za kudai katiba.

Mwishoni wakaamua kuyaondoa yale yote yaliyo muhimu waliyoyataka Wananchi, wakijua wapinzani watachukia, ikawa hivyo, lengo likatimia, muda wa uchaguzi ukafika, uchaguzi ukafanyika bila ya katiba mpya, bila ya Tume huru ya Uchaguzi, wizi wa kura ukafanyika kama ilivyo desturi ya CCM ya nyakati zote.

Yeye naye akafanya mauaji kwenye mikutano ya wapinzani ili watu waogope kuhudhuria mikutano ya vyama vya upinzani. Waliuawa watu Arusha, Morogoro, Geita na Iringa.

Akaja Magufuli, yeye hakutaka mbinu zile za kuzunguka, akaja moja kwa moja, hakuna cha kuuma wala kupuliza, msimamo akauweka wazi kuwa CCM haitaki katiba mpya, haitaki Tume huru ya Uchaguzi, haitaki Bunge wala haitaki mahakama.

Na akasema atahakikisha anaua vyama vyote vya siasa vya upinzani, na aliishi katika hilo. Wapinzani vidomodomo waliuawa au kupotezwa. Wengine kuwatandika rusasi mchana kweupe. Ikawa kabla hayatekeleza kikamilifu lengo lake la kuua vyama vya upinzani, akafa yeye, vyama vya upinzani akiviacha bado vipo, licha ya udikteta wote aliovifanyia.

Akaja Rais Samia, yeye akapokea ushauri, anaendesha utawala wake kwa mbinu za Kikwete, za kuuma na kupuliza, lakini anahakikisha hatoki kwenye lengo kuu la watawala wa CCM, la kuhakikisha Tanzania HAIPATI DEMOKRASIA YA KWELI. Jiulize mpaka leo hii:

1) Magufuli alikataa suala la katiba mpya, Samia ameleta katiba mpya? HAPANA. Anatumia mbinu ile ile ya Kikwete, kuunda kamati, mpaka utafika wakati wa uchaguzi, atakuwa anaongelea tu masuala ya mapendekezo ya kamati.

2) Magufuli hakushughulika kabisa na kuweka utaratibu wa kuhakikisha kuna uchaguzi wa kidemokrasia. Alimpachika mamluki wake kuhakikisha anapokea maagizo toka kwake, ya juu ya nani awe mbunge wapi, nani asiwe. Tangu Samia amekuwa Rais, amemwondoa Mahera?

Au amesimamia utaratibu wa kupata Tume huru ya uchaguzi? HAPANA. Anatumia style ya Kikwete, ya kuuma na kupuliza, ameunda kamati ambayo haina maendeleo yoyote. Ukifika wakati wa uchaguzi atamwelekeza Mahera, wape wapinzani, labda wabunge hamsini ili wakisema hakuna demokrasia, tutawauliza hao 50 wamepatikanaje?

3) Marehemu Magufuli alilitumia sana Jeshi la Polisi kugandamiza haki za wananchi. Rais Samia amebadilisha sheria yoyote inayosimamia utendaji wa haki na weledi wa jeshi la Polisi? HAPANA. Ameacha vile vile ili liendelee kutumika kisiasa, kuwagandamiza washindani wa CCM.

4) Marehemu Magufuli alianzisha sheria mbaya kabisa za vyombo vya habari ili kuua uhuru wa maoni.; sheria ya mitandao ili watu wasihoji chochote; na sheria ya hovyo kabisa ya vyama vya siasa ili aweze kuvifuta vyama vya upinzani kiurahisi.

Ni sheria ipi Rais Samia ameifuta katika orodha hii ya sheria gandamizi? HAKUNA. Mara chache anakemea uonevu wa Polisi lakini hagusi sheria ambayo ndiyo chimbuko la yote. Na hiyo siyo kwa bahati mbaya. Anataka kuhakikisha jeshi la polisi linaendelea kuwa chombo muhimu kabisa cha kuhakikisha NCHI HAIWI NA DEMOMRADIA YA KWELI.

5) Magufuli hakutaka mjadala na vyama vya upinzani. Samia, kwa staili ile ile ya Kikwete, ya kuwaalika wapinzani na kuwanywesha juice ikulu, amewaita mara kadhaa wapinzani ikulu, na kuonesha ukaribu. Lakini je, Rais Samia ameruhusu vyama vya siasa kufanya shughuli zake za siasa kwa mujibu wa katiba? HAPANA.

Anawavutia muda, kwa staili ile ya kupuliza na kuuma. Wapinzani watapelekwa kwa ujanja huu huu, mpaka itafika 2024, halafu wataambiwa muda ni mfupi sana, baada ya uchaguzi tutashughulikia suala la katiba.

Watanzania wamefanywa watoto wadogo, wanapozwa kwa pipi, wakati matatizo yao ya msingi yakiwa yamebakia pale pale siku zote.
 
Wapigania Uhuru wengi wa Afrika moja ya madai yao ilikuwa ni kuleta demokrasia lakini cha kushangaa baada ya wao kuwa watawala wakageuka kuwa mwiba wa kukandamiza demokrasia na mbaya zaidi wakawa hatari kuliko hata wakoloni weupe (wazungu).

Ni uwazi kwamba mkoloni mweusi ni mbaya kuliko mkoloni mweupe "kwaheri ukoloni kwaheri Uhuru"

"Ccm ni janga kwa taifa huu ni ukweli mchungu"
 
Mkuu 'Bams', ngoja nichangie kichwa cha mada kabla sijaingia kusoma ndani.

Inavyoelekea, si watawala pekee, kwa maana ya waliopo na waliokwishapita.

Dalili zinajionyesha wazi kwamba hata hawa wanaopigania kuwa watawala njia yao ni hiyo hiyo moja.

Sasa ngoja nikasome andiko lako refu.
 
Watanzania wamefanywa watoto wadogo, wanapozwa kwa pipi, wakati matatizo yao ya msingi yakiwa yamebakia pale pale
Dah!
Kukusoma kunasisimua mwili.

Mbowe anasema: "Cha msingi sana - Rais ni kwamba alinipa pole. Kwa mtu mwenye busara unaelewa kuwa Rais siyo mtu, Rais ni taasisi. Ni nani katika dunia apewe 'msamaha' na Rais na akatae huo msamaha?"

Kwa maneno haya utaona jinsi Mbowe, pengine na viongozi wengine ndani ya chama chao walivyochotwa akili na mtindo wa hadaa anaouytumia Samia.

Mtu kwa kawaida ungedhani hawa watu ni 'sophisticated' ya kutosha kuweza kujua kwamba Mbowe alikuwa hapewi fadhira na Samia. Mbowe kuwa jela lilikuwa ni kamba kwenye shingo ya Samia, sasa Mbowe anadhani alikuwa akipewa fadhira!

Haya ndiyo maajabu makubwa ya nchi yetu.
 
Baada ya kupata uhuru, tofauti na matarajio ya walio wengi kuwa uhuru na demokrasia vingeongezeka, Mwalimu Nyerere aliharamisha uwepo wa vyama vingine vyote vya siasa isipokuwa chama chake cha TANU.
Tulikuwa taifa changa mno na hiyo ilikuwa mbinu ya kujenga taifa moja lenye umoja bila itikadi za vyama zilizojaa ubaguzi mfano...


AMNUT cha kiislamu, UTP cha walowezi na mamluki wao, ANC cha Zuberi Mtemvu kilichokuwa hakiwakubali Watanganyika wenye asili ya Asia au nje ya Africa n.k
Mohamed Said Pascal Mayalla JokaKuu zitto junior

Tatizo ni kwamba demokrasia yetu ya vyama vingi toka 1992 imehodhiwa na Ccm yaani tuna demokrasia ya chama kimoja tu kiuhalisia, kwani Ccm ndio dola yenyewe.
 
Baada ya kupata uhuru, tofauti na matarajio ya walio wengi kuwa uhuru na demokrasia vingeongezeka, Mwalimu Nyerere aliharamisha uwepo wa vyama vingine vyote vya siasa isipokuwa chama chake cha TANU.
Duuh..... hawa ndio wapigania uhuru mchana usiku walikuwa wakipigania kupata madaraka tu. Kimsingi walikuwa wanaona wivu wakoloni wakishika nadaraka.

Baada ya wanafiki hao kupata madaraka woote kwa ujumla wao waligeuka madikiteta kwa uchache ni
1. Mseven
2. Kagame
3. Mobutu
4. Mugabe
5. Nyerere
6. Arapi Moi
N.k
 
Dah!
Kukusoma kunasisimua mwili.
Mbowe anasema: "Cha msingi sana - Rais ni kwamba alinipa pole. Kwa mtu mwenye busara unaelewa kuwa Rais siyo mtu, Rais ni taasisi. Ni nani katika dunia apewe 'msamaha' na Rais na akatae huo msamaha?"

Kwa maneno haya utaona jinsi Mbowe, pengine na viongozi wengine ndani ya chama chao walivyochotwa akili na mtindo wa hadaa anaouytumia Samia.
Mtu kwa kawaida ungedhani hawa watu ni 'sophisticated' ya kutosha kuweza kujua kwamba Mbowe alikuwa hapewi fadhira na Samia. Mbowe kuwa jela lilikuwa ni kamba kwenye shingo ya Samia, sasa Mbowe anadhani alikuwa akipewa fadhira!
Haya ndiyo maajabu makubwa ya nchi yetu.

.. Kalamu naamini umekosea hapo uliponukuu kauli ya Mbowe.

..hiyo kauli ya Mbowe umeitoa wapi? je, ulichukua muda kusikiliza hotuba ya Mh.Mbowe?

..naomba usikilize kuanzia dakika 38:00 ili kujiridhisha kama ulichoandika ni sahihi au la.

 
Tulikuwa taifa changa mno na hiyo ilikuwa mbinu ya kujenga taifa moja lenye umoja bila itikadi za vyama zilizojaa ubaguzi mfano...


AMNUT cha kiislamu, UTP cha walowezi na mamluki wao, ANC cha Zuberi Mtemvu kilichokuwa hakiwakubali Watanganyika wenye asili ya Asia au nje ya Africa n.k
Mohamed Said Pascal Mayalla JokaKuu zitto junior

Tatizo ni kwamba demokrasia yetu ya vyama vingi toka 1992 imehodhiwa na Ccm yaani tuna demokrasia ya chama kimoja tu kiuhalisia, kwani Ccm ndio dola yenyewe.
Ninakupongeza sana kwa mstari huo wa mwanzo uliouandika hapo.
Hawa watu wengine wanajiandikia tu bila kutafakariw wanachoandika.

Hata hivyo, waseme ni wapi kwenye nchi hizi zilizopata uhuru wake walipoendelea na huo mtindo wa vyama vingi ndani ya bara la Afrika.

Hawafikirii pia hali ya dunia ya wakati ule, wakati wa 'Cold War' ilivyokuwa inalazimisha hali iwe hivyo.

Ni yale yale ya akina Mbowe, leo hii kubwatuka na kulaumu "Ujamaa" kwa hali ya Tanzania leo, huko hatoi mfano hai unaoonyesha mafanikio makubwa yaliyopatikana katika nchi ambazo hapakuwa na ujamaa. Inashangaza sana haelewi 'concept' ya ujamaa ililenga nini kwa wakati husika.

Hata hivyo, kwa hali ya leo hii iliyopo hapa, inamsaidia kitu gani kuhusisha ujamaa na hali duni iliyopo hapa chini ya CCM ambayo iko mbali kabisa na ujamaa miaka mingi sasa!
 
.. Kalamu naamini umekosea hapo uliponukuu kauli ya Mbowe.

..hiyo kauli ya Mbowe umeitoa wapi? je, ulichukua muda kusikiliza hotuba ya Mh.Mbowe?

..naomba usikilize kuanzia dakika 38:00 ili kujiridhisha kama ulichoandika ni sahihi au la.


Nimeinyanyua vile vile ilivyo toka katika kilicholetwa hapa jukwaani kuwa ndiyo hotuba aliyoitoa, alipokuwa akihutubia diaspora. Sijaongeza kitu, labda iwe imenukuliwa vibaya.
Tazama kwenye mada ya mkuu, Master Legendary, yenye kichwa cha mada: Nilitaka kumuelewa Mbowe....

Mchango husika ni ule aliouweka mkuu 'Ichumu lya', #15

Nitaisikiliza nitakapopata muda mzuri wa kufanya hivyo.
 
Marais wote wa Tanzania, nyakati zote, wamefanana kwa jambo moja kubwa, KUDIDIMIZA NA KUUA DEMOKRASIA.

Wakati wa mkoloni, kulikuwa na vyama vingi vya kisiasa. Mwingereza, pamoja na kwamba alikuwa mkoloni, hakuwahi kufuta au kuzuia shughuli za vyama vya siasa. Ndiyo maana kulikuwa na chama cha TAA (Tanganyika African Association).

Baada ya kupata uhuru, tofauti na matarajio ya walio wengi kuwa uhuru na demokrasia vingeongezeka, Mwalimu Nyerere aliharamisha uwepo wa vyama vingine vyote vya siasa isipokuwa chama chake cha TANU.

Tuliendelea na mfumo wa chama kimoja mpaka mabeberu walipozidisha mbinyo dhidi ya nchi zote zisizoheshimu demokrasia, ikiwemo demokrasia ya vyama vingi.

Mwalimu akaelekeza kuanza kwa mfumo wa vyama vingi. Lakini, kiuhalisia ulikuwa ni mfumo wa vyama vingi bandia. Vikosi vya jeshi vikageuzwa kuwa matawi ya CCM, na wakuu wa vikosi wakawa ndio wenyeviti wa matawi ya CCM jeshini.

Taasisi za Elimu ya juu zikafanywa kuwa matawi ya CCM, na kila mahali pa kazi palilazimishwa kuanzishwa tawi la CCM. Chini ya mfumo huo, kitu chochote cha CCM pamoja na michango vikafanywa kuwa ni lazima kwa watu wote.

Hata kujiunga chuo kikuu ulitakiwa kuwa na kadi ya CCM.

Mrema alipogombea Urais kupitia NCCR, ndipo ilipojulikana kuwa hatukuwa na mfumo wa vyama vingi, bali ni kiinimacho cha kuwahadaa mabeberu.

Kwa kutumia makada wake waliopo Polisi, CCM iliwatandika virungu waliokuwa wanamshabikia Mrema, mpaka Mwalimu Nyerere akapiga kelele kukemea. Wakati huo Mwalimu akiwa amestaafu, na Mwinyi ndiye Rais.

Mkapa alipokuwa Rais, naye hakuiacha agenda kuu ya watawala ya kuhakikisha Tanzania hatuwi na demokrasia ya kweli. Wizi wa kura ikawa jambo la kawaida. Kule Zanzibar wananchi walipotaka kuandamana kupinga wizi wa kura za Hayati Maalim Seif, walikutana na risasi za moto, watu takribani 20 wakapoteza maisha.

Kikwete alipoingia akaja na staili ya kuuma na kupuliza. Kelele za kutaka katiba mpya zilipozidi, akaunda Tume, akatengeneza Bunge la katiba, lakini lengo siyo kupata katiba mpya, ilikuwa ni kufifisha jitihada za kudai katiba.

Mwishoni wakaamua kuyaondoa yale yote yaliyo muhimu waliyoyataka Wananchi, wakijua wapinzani watachukia, ikawa hivyo, lengo likatimia, muda wa uchaguzi ukafika, uchaguzi ukafanyika bila ya katiba mpya, bila ya Tume huru ya Uchaguzi, wizi wa kura ukafanyika kama ilivyo desturi ya CCM ya nyakati zote. Yeye naye akafanya mauaji kwenye mikutano ya wapinzani ili watu waogope kuhudhuria mikutano ya vyama vya upinzani. Waliuawa watu Arusha, Morogoro, Geita na Iringa.

Akaja Magufuli, yeye hakutaka mbinu zile za kuzunguka, akaja moja kwa moja, hakuna cha kuuma wala kupuliza, msimamo akauweka wazi kuwa CCM haitaki katiba mpya, haitaki Tume huru ya Uchaguzi, haitaki Bunge wala haitaki mahakama. Na akasema atahakikisha anaua vyama vyote vya siasa vya upinzani, na aliishi katika hilo. Wapinzani vidomodomo waliuawa au kupotezwa. Wengine kuwatandika rusasi mchana kweupe. Ikawa kabla hayatekeleza kikamilifu lengo lake la kuua vyama vya upinzani, akafa yeye, vyama vya upinzani akiviacha bado vipo, licha ya udikteta wote aliovifanyia.

Akaja Rais Samia, yeye akapokea ushauri, anaendesha utawala wake kwa mbinu za Kikwete, za kuuma na kupuliza, lakini anahakikisha hatoki kwenye lengo kuu la watawala wa CCM, la kuhakikisha Tanzania HAIPATI DEMOKRASIA YA KWELI. Jiulize mpaka leo hii:

1) Magufuli alikataa suala la katiba mpya, Samia ameleta katiba mpya? HAPANA. Anatumia mbinu ile ile ya Kikwete, kuunda kamati, mpaka utafika wakati wa uchaguzi, atakuwa anaongelea tu masuala ya mapendekezo ya kamati.

2) Magufuli hakushughulika kabisa na kuweka utaratibu wa kuhakikisha kuna uchaguzi wa kidemokrasia. Alimpachika mamluki wake kuhakikisha anapokea maagizo toka kwake, ya juu ya nani awe mbunge wapi, nani asiwe. Tangu Samia amekuwa Rais, amemwondoa Mahera? Au amesimamia utaratibu wa kupata Tume huru ya uchaguzi? HAPANA. Anatumia style ya Kikwete, ya kuuma na kupuliza, ameunda kamati ambayo haina maendeleo yoyote. Ukifika wakati wa uchaguzi atamwelekeza Mahera, wape wapinzani, labda wabunge hamsini ili wakisema hakuna demokrasia, tutawauliza hao 50 wamepatikanaje?

3) Marehemu Magufuli alilitumia sana Jeshi la Polisi kugandamiza haki za wananchi. Rais Samia amebadilisha sheria yoyote inayosimamia utendaji wa haki na weledi wa jeshi la Polisi? HAPANA. Ameacha vile vile ili liendelee kutumika kisiasa, kuwagandamiza washindani wa CCM.

4) Marehemu Magufuli alianzisha sheria mbaya kabisa za vyombo vya habari ili kuua uhuru wa maoni.; sheria ya mitandao ili watu wasihoji chochote; na sheria ya hovyo kabisa ya vyama vya siasa ili aweze kuvifuta vyama vya upinzani kiurahisi. Ni sheria ipi Rais Samia ameifuta katika orodha hii ya sheria gandamizi? HAKUNA. Mara chache anakemea uonevu wa Polisi lakini hagusi sheria ambayo ndiyo chimbuko la yote. Na hiyo siyo kwa bahati mbaya. Anataka kuhakikisha jeshi la polisi linaendelea kuwa chombo muhimu kabisa cha kuhakikisha NCHI HAIWI NA DEMOMRADIA YA KWELI.

5) Magufuli hakutaka mjadala na vyama vya upinzani. Samia, kwa staili ile ile ya Kimwete, ya kuwaalika wapinzani na kuwanyesha juice ikulu, amewaita mara kadhaa wapinzani ikulu, na kuonesha ukaribu. Lakini je, Rais Samia ameruhusu vyama vya siasa kufanya shughuli zake za siasa kwa mujibu wa katiba? HAPANA. Anawavutia muda, kwa staili ile ya kupuliza na kuuma. Wapinzani watapelekwa kwa ujanja huu huu, mpaka itafika 2024, halafu wataambiwa muda ni mfupi sana, baada ya uchaguzi tutashughulikia suala la katiba.

Watanzania wamefanywa watoto wadogo, wanapozwa kwa pipi, wakati matatizo yao ya msingi yakiwa yamebakia pale pale siku zote.
Dawa ni moja tu.
Kuwanyima kura CCM wakajipange kufanya siasa.

Wao madaraka ni kuula na siyo dhamana ndiyo maana wanaongoza kwa kutoa rushwa
 
Nimeinyanyua vile vile ilivyo toka katika kilicholetwa hapa jukwaani kuwa ndiyo hotuba aliyoitoa, alipokuwa akihutubia diaspora. Sijaongeza kitu, labda iwe imenukuliwa vibaya.
Tazama kwenye mada ya mkuu, Master Legendary, yenye kichwa cha mada: Nilitaka kumuelewa Mbowe....

Mchango husika ni ule aliouweka mkuu 'Ichumu lya', #15

Nitaisikiliza nitakapopata muda mzuri wa kufanya hivyo.

..huyu uliyemnukuu amekupotosha, na imepelekea umeharibu maana nzima ya alichokisema Mh.Mbowe.
 
..huyu uliyemnukuu amekupotosha, na imepelekea umeharibu maana nzima ya alichokisema Mh.Mbowe.
Nitajiridhisha nitakapoisikiliza hiyo hotuba, lakini kutokana na mwelekeo wa mengine yote yanayojadiliwa humu kuhusu hotuba hiyo, sidhani kuwa itabadili mwelekeo mzima wa msimamo wa Mbowe na mkitadha uliopo sasa. Kama chama hicho kitafuata mwelekeo wa Mwenyekiti wake ulivyo sasa, sidhani kuwa kutakuwa na jipya tena.
 
Nitajiridhisha nitakapoisikiliza hiyo hotuba, lakini kutokana na mwelekeo wa mengine yote yanayojadiliwa humu kuhusu hotuba hiyo, sidhani kuwa itabadili mwelekeo mzima wa msimamo wa Mbowe na mkitadha uliopo sasa. Kama chama hicho kitafuata mwelekeo wa Mwenyekiti wake ulivyo sasa, sidhani kuwa kutakuwa na jipya tena.

..naelewa hoja yako.

..lakini kama umeamua kumnukuu mtu yeyote yule, hudhani kama ni haki ukamnukuu kwa usahihi?

..suala la kumnukuu mtu kimakosa wewe halikusumbui?
 
..naelewa hoja yako.

..lakini kama umeamua kumnukuu mtu yeyote yule, hudhani kama ni haki ukamnukuu kwa usahihi?

..suala la kumnukuu mtu kimakosa wewe halikusumbui?
Dah!
Mkuu 'Joka', labda huelewi ninachosema hapa.

Nimenukuu nilichoona kimewekwa hapa JF kuwa ndicho kilichosemwa katika hotuba ya Mbowe. Nilikuwa sijapata 'source' husika ya moja kwa moja toka kinywani mwa Mbowe.

Sasa nitasikiliza hiyo hotuba, nijiridhishe kuwa ile iliyowekwa kimaandishi na mkuu 'Ichumu' haikuwa sahihi.
Sasa sioni kosa langu ni lipi hasa, ulitaka nisubiri hadi hapo itakapowekwa hotuba yenyewe kama ilivyowasilishwa na Mbowe?

Kama kuna kosa, kama unavyosema, siyo kosa langu, ni kosa la aliyewasilisha hiyo hotuba na kudai ndiyo aliyoitoa Mbowe. Kwa bahati mbaya sana, JF hakuna mchujo wa kujua sahihi na kosa ni lipi katika yanayowekwa hapa.
 
Dah!
Mkuu 'Joka', labda huelewi ninachosema hapa.
Nimenukuu nilichoona kimewekwa hapa JF kuwa ndicho kilichosemwa katika hotuba ya Mbowe. Nilikuwa sijapata 'source' husika ya moja kwa moja toka kinywani mwa Mbowe.
Sasa nitasikiliza hiyo hotuba, nijiridhishe kuwa ile iliyowekwa kimaandishi na mkuu 'Ichumu' haikuwa sahihi.
Sasa sioni kosa langu ni lipi hasa, ulitaka nisubiri hadi hapo itakapowekwa hotuba yenyewe kama ilivyowasilishwa na Mbowe?

Kama kuna kosa, kama unavyosema, siyo kosa langu, ni kosa la aliyewasilisha hiyo hotuba na kudai ndiyo aliyoitoa Mbowe. Kwa bahati mbaya sana, JF hakuna mchujo wa kujua sahihi na kosa ni lipi katika yanayowekwa hapa.

..hotuba ya Mbowe hii hapa nimekuwekea.

..huna haja ya kusikiliza hotuba yote.

..sikiliza toka dakika ya 38:00 ujiridhishe kama umemnukuu kwa usahihi au la.

 
..hotuba ya Mbowe hii hapa nimekuwekea.

..sikiliza toka dakika ya 38:00 ujiridhishe kama umemnukuu kwa usahihi au la.


EeenHeee!
Mkuu 'JokaKuu', naona hatuelewani kabisa, sijui kwa nini inakuwa hivi!

Hivi unanisoma kweli, au unashikilia tu msimamo bila ya kusoma ninayoandika.

Sina sababu hata chembe ya kupindisha chochote alichosema Mbowe. Sina.

Sijatunga hayo maneno niliyonukuu hapo, mimi nimeyanyanyua tu toka kwa mtu mwingine aliyeyawasilisha nikiamini kuwa ndiyo yaliyosemwa na Mbowe.

Nimeeleza hapa mara mbili, nitasikiliza mwenyewe alichosema Mbowe toka kwenye hiyo clip uliyoweka.

Sielewi sasa nifanyeje tena!
 
Back
Top Bottom